Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 24.16
Bible en Swahili de l’est


Règne de Joas

1 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba alipoanza kutawala; akatawala miaka arobaini huko Yerusalemu; na jina la mamaye aliitwa Sibia wa Beer-sheba.
2 Rois 11.21-12.15 1 Chroniques 3.11
2 Yoashi akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana siku zote za Yehoyada kuhani.
2 Chroniques 25.2 2 Chroniques 26.4-26.5 Psaumes 106.12-106.13 2 Chroniques 24.17-24.22 2 Rois 12.2
3 Yehoyada akamwoza wake wawili, naye akazaa wana na binti.
Genèse 21.21 Genèse 24.4 Matthieu 19.4-19.8 Genèse 4.19 2 Chroniques 24.15
4 Ikawa baada ya haya, Yoashi alikuwa na nia ya kuitengeneza nyumba ya Mungu.
5 Akawakusanya makuhani na Walawi, akawaambia, Nendeni mijini mwa Yuda, mkakusanye katika Israeli wote fedha, ili kuitengeneza nyumba ya Mungu wenu mwaka kwa mwaka, mkafanye bidii kuliharakisha neno hili. Walakini Walawi hawakuliharakisha.
2 Chroniques 29.3 2 Rois 12.4-12.7 2 Chroniques 34.8-34.9 2 Chroniques 21.2
6 Mfalme akamwita Yehoyada mkuu wao, akamwambia, Mbona hukuwataka Walawi waitoze Yuda na Yerusalemu kodi ya Musa mtumishi wa Bwana, na ya kusanyiko la Israeli, kwa ajili ya hema ya ushuhuda?
Exode 30.12-30.16 Nombres 1.50 Nombres 17.7-17.8 Actes 7.44 Nombres 18.2
7 Kwa kuwa wana wa Athalia, yule mwanamke mwovu, walikuwa wameibomoa nyumba ya Mungu; na vitakatifu vyote vya nyumba ya Bwana wamewapatia mabaali.
2 Chroniques 21.17 Daniel 5.23 Ezéchiel 16.17-16.21 2 Chroniques 28.22-28.24 Deutéronome 32.15-32.17
8 Basi mfalme akaamuru, nao wakafanyiza kasha, wakaliweka nje langoni pa nyumba ya Bwana.
2 Rois 12.8-12.9 Marc 12.41
9 Wakapiga mbiu katika Yuda na Yerusalemu, kumletea Bwana kodi aliyoiweka Musa mtumishi wa Mungu, juu ya Israeli jangwani.
2 Chroniques 24.6 Matthieu 17.24-17.27
10 Wakafurahi maakida wote na watu wote, wakaleta na kutia ndani ya kasha, hata wakaisha.
1 Chroniques 29.9 2 Corinthiens 8.2 2 Corinthiens 9.7 Esaïe 64.5 Actes 2.45-2.47
11 Ikawa wakati walipoletewa kasha wasimamizi wa mfalme kwa mkono wa Walawi, nao wakaona ya kwamba kuna fedha nyingi, huja karani wa mfalme, na msimamizi wake kuhani mkuu, wakatoa yaliyomo kashani, kisha hulichukua kasha, na kulirudisha mahali pake. Ndivyo walivyofanya siku kwa siku, wakakusanya fedha tele.
2 Rois 12.10-12.12 1 Corinthiens 16.2
12 Na mfalme na Yehoyada waliwapa hao waliofanya kazi ya utumishi wa nyumba ya Bwana; nao wakawaajiri waashi na maseremala ili kuitengeza nyumba ya Bwana, na hao pia wafuao chuma na shaba ili kuitengeza nyumba ya Bwana.
2 Chroniques 34.9-34.11 1 Rois 5.15
13 Hivyo mafundi wakafanya kazi yao, nao wakaimaliza, wakaisimamisha nyumba ya Mungu kama ilivyopasa, wakaifanya imara.
Aggée 2.3 1 Chroniques 22.5 Néhémie 4.7 Marc 13.1-13.2
14 Nao walipokwisha, wakaleta mbele ya mfalme na Yehoyada fedha iliyobaki, vikafanyizwa kwayo vyombo vya nyumba ya Bwana, vyombo vya utumishi, navyo vya kutolea, na miiko, na vyombo vya dhahabu na fedha. Wakatoa sadaka za kuteketezwa katika nyumba ya Bwana, daima, siku zote za Yehoyada.
Nombres 28.2-28.29 2 Rois 12.13-12.14 Exode 29.38-29.42 Proverbes 27.22 1 Rois 7.50
15 Lakini Yehoyada akawa mzee, mwenye umri mwingi, akafa; alipokufa alikuwa na umri wa miaka mia na thelathini.
Job 5.26 Psaumes 90.10 Genèse 15.15 1 Chroniques 23.1 Genèse 47.9
16 Wakamzika katika mji wa Daudi kati ya wafalme, kwa sababu ametenda mema katika Israeli, na kwa Mungu, na katika nyumba yake.
2 Chroniques 31.20 Néhémie 13.14 Hébreux 6.10 1 Samuel 2.30 2 Chroniques 23.1-23.21
17 Hata baada ya kufa kwake Yehoyada, wakuu wa Yuda wakamwendea mfalme, wakamsujudia. Naye mfalme akawasikiliza maneno yao.
Deutéronome 31.27 2 Pierre 1.15 2 Chroniques 22.3-22.4 Proverbes 26.8 2 Chroniques 10.8-10.10
18 Wakaiacha nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zao; wakatumikia maashera na sanamu; ghadhabu ikawajia Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hiyo hatia yao.
Josué 22.20 2 Chroniques 24.4 2 Chroniques 19.2 2 Chroniques 29.8 2 Chroniques 28.13
19 Hata hivyo akawapelekea manabii, ili kuwarudisha kwa Bwana; nao wakawashuhudia; lakini hawakukubali kuwasikiliza.
Jérémie 44.4-44.5 Jérémie 25.4-25.5 Matthieu 13.9 Luc 16.31 Esaïe 55.3
20 Na roho ya Mungu ikamjia Zekaria, mwana wa Yehoyada, kuhani; naye akasimama juu ya watu, akawaambia, Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za Bwana, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha Bwana, yeye naye amewaacha ninyi.
2 Chroniques 20.14 Nombres 14.41 2 Chroniques 15.1-15.2 Matthieu 23.35 1 Chroniques 12.18
21 Basi, wakafanya shauri juu yake, wakampiga kwa mawe kwa amri ya mfalme katika ua wa nyumba ya Bwana.
Actes 7.58-7.59 Néhémie 9.26 Matthieu 21.35 Jérémie 11.19 Matthieu 23.34-23.37
22 Basi hivyo mfalme Yoashi hakuukumbuka wema, ambao Yehoyada, baba yake, alimfanyia, bali alimwua mwanawe. Naye alipokufa, alisema, Bwana na ayaangalie haya, akayatakie kisasi.
Genèse 9.5 2 Timothée 4.14 Proverbes 17.13 Luc 17.15-17.18 Jean 10.32
23 Ikawa mwisho wa mwaka, wakakwea juu yake jeshi la Washami; wakafika Yuda na Yerusalemu, wakawaangamiza wakuu wa watu wote miongoni mwa watu, wakamletea mfalme wa Dameski nyara zao zote.
2 Rois 12.17-12.18 Psaumes 82.6-82.7 1 Rois 20.22 2 Chroniques 24.17-24.18 Deutéronome 32.35
24 Maana wakaja jeshi la Washami watu haba; Bwana akatia mikononi mwao jeshi kubwa mno, kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao. Hivyo wakamfanyia Yoashi hukumu.
2 Chroniques 22.8 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.8 Esaïe 30.17 Lévitique 26.25
25 Hata walipoondoka kwake, (nao walimwacha ameshikwa sana na maradhi,) watumishi wake mwenyewe wakamfanyia fitina kwa ajili ya damu ya mwana wa Yehoyada kuhani, wakamwua kitandani pake, akafa; wakamzika mjini mwa Daudi, lakini hawakumzika katika makaburi ya wafalme.
2 Chroniques 24.21-24.22 2 Chroniques 28.27 2 Chroniques 24.16 Psaumes 10.14 2 Chroniques 22.6
26 Na hawa ndio waliomfanyia fitina, Zabadi mwana wa Shimeathi mwanamke Mwamoni, na Yehozabadi mwana wa Shimrithi mwanamke Mmoabi.
2 Rois 12.21
27 Basi kwa habari ya wanawe, na ukubwa wa mizigo aliolemewa, na majengo ya nyumba ya Mungu, tazama, hayo yameandikwa katika maelezo ya kitabu cha wafalme. Na Amazia mwanawe akatawala mahali pake.
1 Chroniques 3.12 2 Chroniques 20.34 2 Rois 12.18 2 Chroniques 24.12 2 Chroniques 13.22

Cette Bible est dans le domaine public.