Préparatifs pour la construction du temple
 1 Ndipo Daudi akasema, Hii ndiyo nyumba ya Bwana Mungu, na hii ndiyo madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa Israeli.
2 Chroniques 3.1  1 Chroniques 21.18-21.28  Genèse 28.17  2 Rois 18.22  2 Chroniques 32.12  
 2 Basi Daudi akaamuru wakusanyike wageni waliokuwa katika nchi ya Israeli; akaweka waashi wachonge mawe ili kujenga nyumba ya Mungu.
1 Rois 5.17-5.18  2 Chroniques 2.17  1 Rois 9.20-9.21  2 Chroniques 8.7-8.8  Ephésiens 2.19-2.22  
 3 Daudi akaweka akiba tele ya chuma kwa misumari ya tarabe za malango, na kwa mafungo; na ya shaba akiba tele isiyo na uzani;
1 Chroniques 22.14  1 Chroniques 29.2  1 Rois 7.47  1 Chroniques 29.7  Jérémie 52.20  
 4 na mierezi isiyo na idadi; kwa kuwa Wasidoni na watu wa Tiro wakamletea Daudi mierezi tele.
1 Rois 5.6-5.10  2 Chroniques 2.3  Esdras 3.7  2 Samuel 5.11  
 5 Daudi akasema, Sulemani mwanangu akali ni mchanga bado, na mwororo, nayo nyumba atakayojengewa Bwana haina budi kuwa nzuri mno, yenye sifa na yenye fahari katika nchi zote; kwa hiyo mimi nitaiwekea akiba. Basi Daudi akaweka akiba tele kabla hajafa.
1 Rois 3.7  1 Chroniques 29.1  Esaïe 64.11  2 Chroniques 2.5  Luc 21.5  
 6 Ndipo akamwita Sulemani mwanawe, akamwagiza amjengee Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba.
Matthieu 28.18-28.20  2 Timothée 4.1  Nombres 27.23  Actes 1.2  1 Timothée 6.13-6.17  
 7 Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Kwangu mimi nia yangu ilikuwa kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Bwana, Mungu wangu.
Psaumes 132.5  Deutéronome 12.5  Deutéronome 12.11  1 Chroniques 17.1-17.15  1 Chroniques 28.2-28.21  
 8 Lakini neno la Bwana likanijia, kusema, Wewe umemwaga damu nyingi, na vita vikubwa umevifanya; wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu;
1 Chroniques 28.3  1 Rois 5.3  2 Samuel 7.5-7.11  1 Chroniques 17.4-17.10  Nombres 31.24  
 9 tazama, utazaliwa mwana, atakayekuwa mtu wa kustarehe; nami nitamstarehesha mbele ya adui zake pande zote; kwani jina lake litakuwa Sulemani, nami nitawapa Israeli amani na utulivu siku zake ;
1 Rois 4.25  1 Rois 5.4  1 Rois 4.20  2 Samuel 12.24-12.25  2 Samuel 7.12-7.13  
 10 huyo ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu; naye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa babaye; nami nitakifanya imara milele kiti cha ufalme wake juu ya Israeli.
Hébreux 1.5  2 Samuel 7.13-7.14  Psaumes 89.26  1 Rois 8.19-8.20  1 Chroniques 28.6-28.7  
 11 Sasa mwanangu, Bwana na awe pamoja nawe; ukafanikiwe, na kuijenga nyumba ya Bwana, Mungu wako, kama alivyonena kwa habari zako.
1 Chroniques 22.16  2 Timothée 4.22  Romains 15.33  Matthieu 1.23  Esaïe 26.12  
 12 Bwana na akupe busara na akili, akakuagizie juu ya Israeli; ili uishike torati ya Bwana, Mungu wako.
2 Chroniques 1.10  1 Rois 3.9-3.12  Psaumes 72.1  1 Jean 2.3  Proverbes 14.8  
 13 Ndipo utakapofanikiwa, ukiangalia kuzitenda amri, na hukumu, Bwana alizomwagizia Musa juu ya Israeli; uwe hodari, na wa moyo mkuu; usiogope wala usifadhaike.
1 Chroniques 28.7  Josué 1.6-1.9  1 Chroniques 28.20  Josué 1.18  Galates 6.2  
 14 Basi sasa, tazama, katika shida yangu, nimeiwekea akiba nyumba ya Bwana, talanta elfu mia za dhahabu, na talanta elfu elfu za fedha; na shaba na chuma isiyo na uzani; kwa vile zilivyo tele; miti tena na mawe nimeweka akiba, nawe utaweza kuongeza.
1 Chroniques 22.3  1 Rois 10.14  2 Rois 25.16  Jérémie 52.20  1 Chroniques 29.4-29.7  
 15 Tena kwako kuna mafundi wengi, wenye kuchonga na kufanyiza kazi ya mawe na miti, na kila aliye mstadi kwa kazi yo yote;
Exode 28.6  Exode 35.32  Exode 31.3-31.5  Exode 35.35  1 Rois 7.14  
 16 ya dhahabu, ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, hapana hesabu; basi inuka ushike kazi, naye Bwana na awe pamoja nawe.
1 Chroniques 22.11  1 Chroniques 22.3  Josué 7.10  Josué 1.5  1 Chroniques 22.14  
 17 Tena Daudi akawaamuru wakuu wote wa Israeli, kwamba wamsaidie Sulemani mwanawe, akisema,
1 Chroniques 28.1-28.6  1 Chroniques 28.21  1 Chroniques 29.6  Romains 16.2-16.3  Philippiens 4.3  
 18 Je! Si Bwana, Mungu wenu, aliye pamoja nanyi? Na kuwastarehesha pande zote? Kwa kuwa wenyeji wa nchi amewatia mkononi mwangu; nayo nchi imetiishwa mbele za Bwana, na mbele ya watu wake.1 Chroniques 23.25  1 Chroniques 22.9  2 Samuel 7.1  Josué 23.1  Romains 8.31  
 19 Basi sasa jitieni moyo na nia kumtafuta Bwana, Mungu wenu; inukeni basi, mkamjengee Bwana Mungu mahali patakatifu, ili kulileta sanduku la agano la Bwana, na vyombo vitakatifu vya Mungu, ndani ya nyumba itakayojengwa kwa ajili ya jina la Bwana.
1 Chroniques 28.9  2 Chroniques 5.7  Deutéronome 4.29  1 Rois 8.6  1 Chroniques 22.7