Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 22
Bible en Swahili de l’est


Préparatifs pour la construction du temple

1 Ndipo Daudi akasema, Hii ndiyo nyumba ya Bwana Mungu, na hii ndiyo madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa Israeli.
2 Chroniques 3.1 1 Chroniques 21.18-21.28 Genèse 28.17 Deutéronome 12.11 2 Samuel 24.18
2 Basi Daudi akaamuru wakusanyike wageni waliokuwa katika nchi ya Israeli; akaweka waashi wachonge mawe ili kujenga nyumba ya Mungu.
2 Chroniques 2.17 1 Rois 9.20-9.21 1 Rois 5.17-5.18 1 Rois 6.7 Ephésiens 2.12
3 Daudi akaweka akiba tele ya chuma kwa misumari ya tarabe za malango, na kwa mafungo; na ya shaba akiba tele isiyo na uzani;
1 Chroniques 22.14 1 Chroniques 29.2 1 Rois 7.47 1 Chroniques 29.7 Jérémie 52.20
4 na mierezi isiyo na idadi; kwa kuwa Wasidoni na watu wa Tiro wakamletea Daudi mierezi tele.
1 Rois 5.6-5.10 2 Chroniques 2.3 Esdras 3.7 2 Samuel 5.11
5 Daudi akasema, Sulemani mwanangu akali ni mchanga bado, na mwororo, nayo nyumba atakayojengewa Bwana haina budi kuwa nzuri mno, yenye sifa na yenye fahari katika nchi zote; kwa hiyo mimi nitaiwekea akiba. Basi Daudi akaweka akiba tele kabla hajafa.
1 Rois 3.7 1 Chroniques 29.1 2 Chroniques 13.7 2 Pierre 1.13-1.15 2 Chroniques 7.21
6 Ndipo akamwita Sulemani mwanawe, akamwagiza amjengee Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba.
Deutéronome 31.23 Actes 20.25-20.31 Deutéronome 31.14 1 Timothée 5.21 Matthieu 28.18-28.20
7 Daudi akamwambia Sulemani mwanawe, Kwangu mimi nia yangu ilikuwa kujenga nyumba kwa ajili ya jina la Bwana, Mungu wangu.
Psaumes 132.5 Deutéronome 12.5 Deutéronome 12.11 2 Chroniques 2.4 Deutéronome 12.21
8 Lakini neno la Bwana likanijia, kusema, Wewe umemwaga damu nyingi, na vita vikubwa umevifanya; wewe hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu, kwa sababu umemwaga damu nyingi juu ya nchi machoni pangu;
1 Chroniques 28.3 1 Rois 5.3 2 Samuel 7.5-7.11 Nombres 31.24 Nombres 31.20
9 tazama, utazaliwa mwana, atakayekuwa mtu wa kustarehe; nami nitamstarehesha mbele ya adui zake pande zote; kwani jina lake litakuwa Sulemani, nami nitawapa Israeli amani na utulivu siku zake ;
1 Rois 4.25 1 Rois 5.4 1 Rois 4.20 2 Samuel 12.24-12.25 Psaumes 72.7
10 huyo ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya jina langu; naye atakuwa mwanangu, nami nitakuwa babaye; nami nitakifanya imara milele kiti cha ufalme wake juu ya Israeli.
2 Samuel 7.13-7.14 Hébreux 1.5 Esaïe 9.7 1 Rois 5.5 Psaumes 89.36-89.37
11 Sasa mwanangu, Bwana na awe pamoja nawe; ukafanikiwe, na kuijenga nyumba ya Bwana, Mungu wako, kama alivyonena kwa habari zako.
1 Chroniques 22.16 Matthieu 1.23 Esaïe 26.12 Matthieu 28.20 1 Chroniques 28.20
12 Bwana na akupe busara na akili, akakuagizie juu ya Israeli; ili uishike torati ya Bwana, Mungu wako.
2 Chroniques 1.10 1 Rois 3.9-3.12 Psaumes 72.1 Proverbes 2.6-2.7 1 Rois 11.1-11.10
13 Ndipo utakapofanikiwa, ukiangalia kuzitenda amri, na hukumu, Bwana alizomwagizia Musa juu ya Israeli; uwe hodari, na wa moyo mkuu; usiogope wala usifadhaike.
1 Chroniques 28.20 1 Chroniques 28.7 Josué 1.6-1.9 Psaumes 119.6 1 Rois 2.3
14 Basi sasa, tazama, katika shida yangu, nimeiwekea akiba nyumba ya Bwana, talanta elfu mia za dhahabu, na talanta elfu elfu za fedha; na shaba na chuma isiyo na uzani; kwa vile zilivyo tele; miti tena na mawe nimeweka akiba, nawe utaweza kuongeza.
1 Chroniques 22.3 Jérémie 52.20 1 Chroniques 29.4-29.7 2 Corinthiens 8.2 1 Rois 10.14
15 Tena kwako kuna mafundi wengi, wenye kuchonga na kufanyiza kazi ya mawe na miti, na kila aliye mstadi kwa kazi yo yote;
Exode 35.32 Exode 31.3-31.5 Exode 35.35 1 Rois 7.14 Exode 28.6
16 ya dhahabu, ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, hapana hesabu; basi inuka ushike kazi, naye Bwana na awe pamoja nawe.
1 Chroniques 22.11 Josué 1.2 1 Corinthiens 15.58 2 Chroniques 20.17 1 Samuel 17.37
17 Tena Daudi akawaamuru wakuu wote wa Israeli, kwamba wamsaidie Sulemani mwanawe, akisema,
1 Chroniques 28.1-28.6 1 Chroniques 29.6 Romains 16.2-16.3 Philippiens 4.3 3 Jean 1.8
18 Je! Si Bwana, Mungu wenu, aliye pamoja nanyi? Na kuwastarehesha pande zote? Kwa kuwa wenyeji wa nchi amewatia mkononi mwangu; nayo nchi imetiishwa mbele za Bwana, na mbele ya watu wake.
1 Chroniques 23.25 1 Chroniques 22.9 2 Samuel 7.1 Josué 23.1 Deutéronome 12.10-12.11
19 Basi sasa jitieni moyo na nia kumtafuta Bwana, Mungu wenu; inukeni basi, mkamjengee Bwana Mungu mahali patakatifu, ili kulileta sanduku la agano la Bwana, na vyombo vitakatifu vya Mungu, ndani ya nyumba itakayojengwa kwa ajili ya jina la Bwana.
1 Chroniques 28.9 1 Chroniques 22.7 2 Chroniques 5.7 Deutéronome 4.29 1 Rois 8.6

Cette Bible est dans le domaine public.