Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 75
Bible en Swahili de l’est


1 Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu. 2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki. 3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake. 4 Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe. 5 Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi. 6 Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima. 7 Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu. 8 Maana mkononi mwa Bwana mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa. 9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo. 10 Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.

Cette Bible est dans le domaine public.