Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 46.8

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 46

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 45 Chapitre 47

Dieu, le souverain refuge

1 Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
2 Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.
3 Maji yake yajapovuma na kuumuka, Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.
4 Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu, Patakatifu pa maskani zake Aliye juu.
5 Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa; Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
6 Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki; Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka.
7 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
8 Njoni myatazame matendo ya Bwana, Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
9 Avikomesha vita hata mwisho wa dunia; Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.
10 Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu, Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.
11 Bwana wa majeshi yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 46.8 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.