Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ruth 3
Bible en Swahili de l’est


Mariage de Ruth et Boaz

1 Kisha Naomi akamwambia mkwewe, Je! Mwanangu, si vizuri nikutafutie raha, ili upate mema?
Ruth 1.9 Genèse 40.14 Deutéronome 4.40 Psaumes 128.2 Jérémie 22.15-22.16
2 Basi na huyu Boazi, je! Siye wa mbari yetu, ambaye ulikuwapo pamoja na wasichana wake? Tazama, usiku wa leo atakuwa akipepeta shayiri pale ugani.
Ruth 2.8 Ruth 2.20-2.23 Hébreux 2.11-2.14 Deutéronome 25.5-25.10 Ruth 2.1
3 Basi wewe oga, ujipake mafuta ujivike mavazi yako, kisha uende kwenye uga; walakini usijionyeshe kwake mtu yule, ila atakapokwisha kula na kunywa.
2 Samuel 14.2 Ecclésiaste 9.8 Psaumes 104.15 1 Timothée 2.9-2.10 Esther 5.1
4 Nayo itakuwa wakati atakapolala, utapaangalia mahali alalapo, nawe uingie, uifunue miguu yake ujilaze hapo; na yeye atakuambia utakalofanya.
1 Thessaloniciens 5.22
5 Akamwambia, Hayo yote unenayo mimi nitayafanya.
Ephésiens 6.1 Colossiens 3.20
6 Basi akashuka mpaka ugani; akafanya yote kama vile mkwewe alivyomwagiza.
Proverbes 1.8 Exode 20.12 Jean 2.5 Jean 15.14
7 Ikawa huyo Boazi alipokwisha kula na kunywa, na moyo wake umekunjuka, alikwenda kulala penye mwisho wa chungu ya nafaka; na huyo mwanamke akaja taratibu, akaifunua miguu yake, akajilaza papo hapo.
Juges 19.6 Juges 19.9 Esther 1.10 2 Samuel 13.28 Juges 19.22
8 Na ikawa usiku wa manane yule mtu akasituka, akajigeuza; na kumbe! Yupo mwanamke amelala miguuni pake.
9 Akasema, Ama! Ni nani wewe? Akamjibu, Ni mimi, Ruthuu, mjakazi wako; uitande nguo yako juu ya mjakazi wako; kwa kuwa ndiwe wa jamaa aliye karibu.
Ezéchiel 16.8 Ruth 2.20 Ruth 3.12 Luc 14.11 Ruth 2.10-2.13
10 Akamwambia, Mwanangu, ubarikiwe na Bwana; umezidi kuonyesha fadhili zako mwisho kuliko mwanzo, kwa vile usivyowafuata vijana, kama ni maskini kama ni matajiri.
Ruth 2.20 Ruth 1.8 Ruth 2.4 1 Corinthiens 13.4-13.5
11 Basi, mwanangu, usiogope; mimi nitakufanyia yote uyanenayo; kwa maana mji wote pia wa watu wangu wanakujua ya kwamba u mwanamke mwema.
Proverbes 31.10 Proverbes 12.4 Proverbes 31.29-31.31
12 Tena ndiyo kweli ya kuwa mimi ni wa jamaa yako aliye karibu; lakini kuna mtu wa jamaa aliye karibu kuliko mimi.
Ruth 4.1 Matthieu 7.12 1 Thessaloniciens 4.6
13 Wewe ungoje usiku huu; kisha, asubuhi, kama akikubali kukufanyia impasavyo jamaa, haya, na akufanyie; lakini ikiwa hataki yeye, basi mimi nitakufanyia impasavyo jamaa; Bwana aishivyo. Ulale wewe hata asubuhi.
Jérémie 4.2 Juges 8.19 Ruth 4.5 Matthieu 22.24-22.27 Ruth 2.20
14 Hivyo huyo mwanamke akalala miguuni pake hata asubuhi; akaondoka mapema asijaweza mtu kumtambua mwenziwe; maana Boazi amesema, Isijulikane kabisa ya kuwa mwanamke alifika penye uga.
2 Corinthiens 8.21 Romains 14.16 1 Pierre 2.12 1 Thessaloniciens 5.22 Ecclésiaste 7.1
15 Tena alisema, Lete hapa shela yako uliyoivaa, uishike; naye akaishika; naye akampimia vipimo sita vya shayiri akamtwika; kisha huyo mwanamke akaenda zake mjini.
Galates 6.10 Esaïe 32.8
16 Basi alipofika kwa mkwewe, huyo akamwuliza, Je! Mwanangu, imekuwaje? Akamwambia yote yule mtu aliyomfanyia.
17 Akasema, Na vipimo hivi sita vya shayiri amenipa; maana akaniambia, Usiende kwa mkweo mikono mitupu.
18 Naye mkwewe akasema, Basi, mwanangu, tulia; hata utakapojua jinsi litakavyotukia jambo hili; kwa sababu mtu huyu hataridhika, asipolimaliza jambo hilo leo.
Psaumes 37.3-37.5 Esaïe 28.16 Esaïe 30.7

Cette Bible est dans le domaine public.