Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Thessaloniciens 3.3
Bible en Swahili de l’est


1 Basi kwa hiyo, tulipokuwa hatuwezi kuvumilia zaidi, tuliona vema kuachwa Athene peke yetu.
Actes 17.15 1 Thessaloniciens 3.5 1 Thessaloniciens 2.17 Jérémie 20.9 2 Corinthiens 2.13
2 Tukamtuma Timotheo ndugu yetu, mtumishi wa Mungu katika Injili ya Kristo, ili kuwafanya ninyi imara na kuwafariji kwa habari ya imani yenu;
Actes 14.22-14.23 Ephésiens 6.21-6.22 Philippiens 1.25 Romains 16.21 2 Corinthiens 8.23
3 mtu asifadhaishwe na dhiki hizi; maana ninyi wenyewe mnajua ya kuwa twawekewa hizo.
Actes 14.22 Actes 9.16 Actes 21.13 Luc 21.12 Matthieu 24.9-24.10
4 Kwa kuwa tulipokuwapo kwenu tulitangulia kuwaambia kwamba tutapata dhiki, kama ilivyotukia, nanyi mwajua.
1 Thessaloniciens 2.14 1 Thessaloniciens 2.2 Actes 20.24 Actes 17.13 2 Corinthiens 8.1-8.2
5 Kwa hiyo mimi nami nilipokuwa siwezi kuvumilia tena, nalituma mtu ili niijue imani yenu, asije yule mjaribu akawajaribu, na taabu yetu ikawa haina faida.
Matthieu 4.3 Philippiens 2.16 Jacques 1.13-1.14 Ephésiens 4.14 2 Corinthiens 2.11
6 Lakini Timotheo alipotujia hivi sasa kutoka kwenu, alituletea habari njema za imani yenu na upendo wenu, na ya kwamba mnatukumbuka vema siku zote; mkitamani kutuona sisi vile vile kama sisi kuwaona ninyi.
1 Corinthiens 11.2 Proverbes 25.25 Actes 18.5 1 Thessaloniciens 1.3 Esaïe 52.7
7 Kwa sababu hiyo, ndugu, tulifarijiwa kwa habari zenu, katika msiba na dhiki yetu yote, kwa imani yenu.
2 Corinthiens 1.4 2 Corinthiens 11.23-11.28 2 Corinthiens 7.6-7.7 1 Corinthiens 4.9-4.13 Actes 17.4-17.10
8 Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.
1 Corinthiens 16.13 Colossiens 1.23 Actes 11.23 Ephésiens 3.17 Philippiens 1.27
9 Maana ni shukrani gani tuwezayo kumlipa Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha ile yote tunayoifurahia, kwa sababu yenu mbele za Mungu wetu;
2 Corinthiens 9.15 2 Samuel 7.18-7.20 1 Thessaloniciens 3.7-3.8 Deutéronome 16.11 Psaumes 71.14-71.15
10 usiku na mchana tunapoomba kwa juhudi tupate kuwaona nyuso zenu, na kuyatengeneza mapungufu ya imani yenu?
2 Timothée 1.3 2 Corinthiens 13.9 Romains 1.10-1.12 2 Corinthiens 1.24 2 Thessaloniciens 1.11
11 Basi Mungu mwenyewe, Baba yetu, na Bwana wetu Yesu, atuongoze njia yetu tufike kwenu.
2 Thessaloniciens 2.16 1 Thessaloniciens 3.13 Proverbes 3.5-3.6 Luc 12.32 Romains 1.3
12 Bwana na awaongeze na kuwazidisha katika upendo, ninyi kwa ninyi, na kwa watu wote, kama vile sisi nasi tulivyo kwenu;
Philippiens 1.9 2 Thessaloniciens 1.3 1 Thessaloniciens 4.9-4.10 1 Thessaloniciens 5.15 1 Jean 3.11-3.19
13 apate kuifanya imara mioyo yenu iwe bila lawama katika utakatifu mbele za Mungu, Baba yetu, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu pamoja na watakatifu wake wote.
1 Thessaloniciens 5.23 1 Thessaloniciens 2.19 Colossiens 1.22 Ephésiens 5.27 1 Corinthiens 1.7-1.8

Cette Bible est dans le domaine public.