Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Cantique 2.15
Bible en Swahili de l’est


1 Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.
Osée 14.5 Esaïe 35.1-35.2 Cantique 5.13 Esaïe 57.15 Cantique 6.3

Le jeune homme

2 Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti.
1 Pierre 2.12 Philippiens 2.15-2.16 Matthieu 10.16 Esaïe 55.13 Matthieu 6.28-6.29

La jeune femme

3 Kama mpera kati ya miti ya msituni, Kadhalika mpendwa wangu kati ya vijana. Naliketi kivulini mwake kwa furaha, Na matunda yake naliyaonja kuwa matamu.
Cantique 8.5 Esaïe 25.4 Esaïe 32.2 Hébreux 1.1-1.6 Psaumes 57.1
4 Akanileta mpaka nyumba ya karamu, Na bendera yake juu yangu ni mapenzi.
Cantique 1.4 Psaumes 20.5 Psaumes 84.10 Esaïe 11.10 Apocalypse 3.20
5 Nishibisheni zabibu, niburudisheni kwa mapera, Kwa maana nimezimia kwa mapenzi.
Cantique 5.8 Osée 3.1 2 Samuel 6.19 2 Samuel 13.1-13.2 Psaumes 63.1-63.3
6 Mkono wake wa kushoto uko chini ya kichwa changu, Nao wa kuume unanikumbatia!
Sophonie 3.17 Esaïe 54.5-54.10 Jérémie 32.41 Proverbes 4.8 Cantique 8.3-8.5

Le jeune homme

7 Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu, Kwa paa na kwa ayala wa porini, Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha, Hata yatakapoona vema yenyewe.
Cantique 3.5 Cantique 8.4 Cantique 1.5 Cantique 5.8-5.9 Proverbes 5.19

La jeune femme

8 Sikiliza! Ni mpendwa wangu! Tazama, anakuja, Akiruka milimani, akichachawa vilimani.
Cantique 5.2 Esaïe 44.23 Esaïe 49.11-49.13 Jean 10.27 Luc 3.4-3.6
9 Mpendwa wangu ni kama paa, au ayala. Tazama, asimama nyuma ya ukuta wetu, Achungulia dirishani, atazama kimiani.
Cantique 8.14 Cantique 2.17 1 Corinthiens 13.12 Hébreux 9.8-9.9 Apocalypse 19.10
10 Mpendwa wangu alinena, akaniambia, Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako,
Cantique 2.13 2 Corinthiens 6.17-6.18 Cantique 2.8 Matthieu 4.19-4.22 Psaumes 85.8
11 Maana tazama, kaskazi imepita, Masika imekwisha, imekwenda zake;
Esaïe 12.1-12.2 Matthieu 5.4 Esaïe 40.2 Ecclésiaste 3.11 Esaïe 54.6-54.8
12 Maua yatokea katika nchi, Wakati wa kupelea umefika, Na sauti ya mwigo husikiwa kwetu.
Psaumes 148.7-148.13 Psaumes 89.15 Esaïe 35.1-35.2 Esaïe 55.12 Esaïe 42.10-42.12
13 Mtini wapevusha tini zake, Na mizabibu inachanua, Inatoa harufu yake nzuri; Ondoka, mpenzi wangu, mzuri wangu, uje zako.
Cantique 2.10 Esaïe 61.11 2 Corinthiens 5.20 Esaïe 18.5 Luc 13.6-13.7
14 Hua wangu, mafichoni mwa jabali, Katika sitara za magenge, Nitazame uso wako, nisikie sauti yako, Maana sauti yako ni tamu na uso wako mzuri.
Cantique 1.5 Cantique 8.13 Exode 3.6 Exode 33.22-33.23 Esdras 9.5-9.6
15 Tukamatie mbweha, Wale mbweha wadogo, Waiharibuo mizabibu, Maana mizabibu yetu yachanua.
Apocalypse 2.2 2 Pierre 2.1-2.3 Cantique 2.13 Luc 13.32 Cantique 7.12
16 Mpendwa wangu ni wangu, na mimi ni wake; Hulisha kundi lake penye nyinyoro.
Cantique 6.3 Cantique 7.10 Cantique 4.5 Cantique 2.1 Galates 2.20
17 Hata jua lipunge, na vivuli vikimbie, Unigeukie, mpendwa wangu, Nawe uwe kama paa, au ayala, Juu ya milima ya Betheri.
Cantique 4.6 Cantique 2.8-2.9 2 Pierre 1.19 Cantique 8.14 Romains 13.12

Cette Bible est dans le domaine public.