Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 78.50
Bible en Swahili de l’est


Fidélité de Dieu au cours de l’histoire d’Israël

1 Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.
Esaïe 51.4 Esaïe 55.3 Proverbes 8.4-8.6 2 Chroniques 15.1-15.16 Psaumes 74.1
2 Na nifunue kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale.
Psaumes 49.4 Proverbes 1.6 Matthieu 13.34-13.35 Marc 4.34 Matthieu 13.11-13.13
3 Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, Ambayo baba zetu walituambia.
Psaumes 44.1 Exode 12.26-12.27 Psaumes 48.8 Exode 13.8 Exode 13.14-13.15
4 Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za Bwana, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
Deutéronome 11.19 Joël 1.3 Deutéronome 6.7 Psaumes 145.4-145.6 Josué 4.6-4.7
5 Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao,
Psaumes 147.19 Psaumes 81.5 Deutéronome 4.45 Ephésiens 6.4 Romains 3.2
6 Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao
Psaumes 102.18 Esther 9.28 Psaumes 71.18 Deutéronome 4.10 Joël 1.3
7 Wamwekee Mungu tumaini lao. Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, Bali wazishike amri zake.
Deutéronome 5.29 Deutéronome 4.9 Psaumes 146.5 1 Corinthiens 11.24 1 Pierre 1.21
8 Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.
Psaumes 78.37 Exode 32.9 Ezéchiel 20.18 Deutéronome 31.27 2 Rois 17.14
9 Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, Walirudi nyuma siku ya vita.
Psaumes 78.57 Juges 20.39 1 Chroniques 12.2 Juges 9.28 1 Samuel 4.10
10 Hawakulishika agano la Mungu; Wakakataa kuenenda katika sheria yake;
Deutéronome 31.20 Néhémie 9.26-9.29 2 Rois 17.14-17.15 Juges 2.10-2.12 Deutéronome 31.16
11 Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.
Psaumes 106.13 Psaumes 106.21-106.22 Deutéronome 32.18 Jérémie 2.32 Psaumes 78.7
12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.
Nombres 13.22 Esaïe 19.11 Ezéchiel 30.14 Exode 7.1-12.51 Esaïe 19.13
13 Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
Exode 15.8 Exode 14.21 Psaumes 66.6 Esaïe 63.13 Psaumes 136.13-136.15
14 Akawaongoza kwa wingu mchana, Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
Psaumes 105.39 Exode 14.24 Exode 13.21-13.22 Exode 40.35-40.38 Néhémie 9.12
15 Akapasua miamba jangwani; Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
Exode 17.6 Psaumes 114.8 1 Corinthiens 10.4 Psaumes 105.41 Nombres 20.11
16 Akatokeza na vijito gengeni, Akatelemsha maji kama mito.
Psaumes 105.41 Deutéronome 9.21 Nombres 20.8 Deutéronome 8.15 Nombres 20.10-20.11
17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi, Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
Esaïe 63.10 Psaumes 95.8-95.10 Hébreux 3.16-3.19 Psaumes 106.13-106.32 Psaumes 78.32
18 Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
Nombres 11.4 1 Corinthiens 10.9 Deutéronome 6.16 1 Corinthiens 10.6 Psaumes 95.9
19 Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
Nombres 21.5 Nombres 11.4 Exode 16.8-16.10 Nombres 11.13 Exode 16.3
20 Tazama, aliupiga mwamba; Maji yakabubujika, ikafurika mito. Pia aweza kutupa chakula? Atawaandalia watu wake nyama?
Nombres 20.11 Genèse 18.12-18.14 Nombres 11.21-11.23 Exode 17.6-17.7 Psaumes 78.41
21 Hivyo Bwana aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
Psaumes 78.31 1 Corinthiens 10.5 Hébreux 12.29 Nombres 11.10 Deutéronome 32.22
22 Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, Wala hawakuutumainia wokovu wake.
Hébreux 3.18-3.19 1 Jean 5.10 Psaumes 106.24 Hébreux 3.12 Jude 1.5
23 Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
Genèse 7.11 Malachie 3.10 2 Rois 7.19 Psaumes 33.9 Esaïe 5.6
24 Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.
Exode 16.4 Psaumes 105.40 1 Corinthiens 10.3 Deutéronome 8.3 Jean 6.31-6.71
25 Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
Psaumes 103.20 Exode 16.8 Matthieu 14.20 Matthieu 15.37
26 Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
Nombres 11.31 Psaumes 135.7
27 Akawanyeshea nyama kama mavumbi, Na ndege wenye mbawa, Kama mchanga wa bahari.
Exode 16.12-16.13 Nombres 11.18-11.19 Nombres 11.32
28 Akawaangusha kati ya matuo yao, Pande zote za maskani zao.
29 Wakala wakashiba sana; Maana aliwaletea walivyovitamani;
Psaumes 106.15 Nombres 11.19-11.20
30 Hawakuachana na matakwa yao. Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao
Luc 16.19-16.23 Proverbes 1.32 Nombres 22.20-22.22 Nombres 11.33-11.34
31 Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli.
Esaïe 10.16
32 Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Nombres 14.1-14.45 Psaumes 78.22 Nombres 16.1-16.17 Jean 12.37 Nombres 21.1-21.6
33 Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha.
Nombres 14.29 Nombres 14.35 Nombres 26.64-26.65 Job 5.6-5.7 Ecclésiaste 12.8
34 Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii.
Osée 5.15 Nombres 21.7 Juges 3.12-3.15 Juges 10.7-10.10 Jérémie 22.23
35 Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao.
Deutéronome 32.4 Exode 15.13 Esaïe 41.14 Deutéronome 32.15 Psaumes 78.7
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao.
Ezéchiel 33.31 Esaïe 29.13 Psaumes 106.12-106.13 Esaïe 57.11 Osée 11.12
37 Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Actes 8.21 Psaumes 78.8 Psaumes 51.10 Osée 10.2 Psaumes 119.80
38 Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.
Nombres 14.18-14.20 Esaïe 48.9 Exode 34.6-34.9 Nombres 16.44-16.48 Ezéchiel 20.13-20.14
39 Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.
Genèse 6.3 Job 7.7 Jacques 4.14 Job 7.16 Psaumes 103.14-103.16
40 Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani!
Ephésiens 4.30 Esaïe 63.10 Psaumes 95.8-95.10 Psaumes 78.17 Esaïe 7.13
41 Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli.
Nombres 14.22 Nombres 14.4 2 Rois 19.22 Hébreux 3.8-3.11 Psaumes 89.18
42 Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.
Juges 8.34 Exode 14.12 Exode 13.9 Psaumes 78.21-78.22 Psaumes 136.10-136.15
43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.
Exode 3.19-3.20 Psaumes 105.27-105.38 Psaumes 135.9 Deutéronome 4.34 Néhémie 9.10
44 Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa.
Psaumes 105.29 Apocalypse 16.3-16.6 Exode 7.17-7.21
45 Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu.
Psaumes 105.30-105.31 Exode 8.21-8.24 Exode 8.2-8.15 Apocalypse 16.3
46 Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao.
Psaumes 105.34-105.35 Exode 10.12-10.15 Amos 7.1-7.2 Joël 2.25 Joël 1.4-1.7
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu.
Psaumes 105.32-105.33 Exode 9.18-9.34
48 Akaacha ng’ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme.
Exode 9.28 Exode 9.19
49 Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya.
Exode 15.7 Psaumes 11.6 Sophonie 3.8 Esaïe 42.25 Job 20.23
50 Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao;
Ezéchiel 9.10 Ezéchiel 7.4 Romains 8.32 2 Pierre 2.4-2.5 Exode 9.3-9.6
51 Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu.
Psaumes 105.23 Psaumes 135.8 Psaumes 106.22 Psaumes 105.36 Psaumes 136.10
52 Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.
Psaumes 77.20 Néhémie 9.12 Psaumes 105.37 Jean 10.11-10.42 Esaïe 63.11-63.14
53 Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao.
Exode 14.19-14.20 Exode 14.27-14.28 Exode 15.10 Psaumes 136.15 Exode 14.15
54 Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume.
Exode 15.17 Psaumes 44.3 Exode 15.13 Esaïe 11.9 Ephésiens 1.14
55 Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.
Psaumes 44.2 Josué 13.7 Néhémie 9.22-9.25 Josué 6.1-6.21 Deutéronome 6.10-6.12
56 Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.
Juges 2.11-2.12 Deutéronome 31.16-31.20 Néhémie 9.25-9.26 Deutéronome 32.15-32.21 Psaumes 78.40-78.41
57 Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa.
Osée 7.16 Ezéchiel 20.27-20.28 Psaumes 78.8 Psaumes 78.10-78.37 Psaumes 78.41
58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
Deutéronome 32.21 Lévitique 26.30 Deutéronome 12.2 1 Rois 12.31 1 Rois 11.7
59 Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.
Psaumes 106.40 Zacharie 11.8 Psaumes 14.2-14.5 Psaumes 11.4 Deutéronome 32.19
60 Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
Josué 18.1 1 Samuel 4.4-4.11 Jérémie 26.6-26.9 1 Samuel 1.3 Jérémie 7.12-7.14
61 Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
Psaumes 132.8 Juges 18.30 Psaumes 63.2 1 Samuel 4.21-5.2 Psaumes 24.7
62 Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; Akaughadhibikia urithi wake.
Psaumes 89.38 1 Samuel 4.10-4.11 1 Samuel 4.2 Esaïe 64.9
63 Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Jérémie 7.34 Jérémie 16.9 Psaumes 78.21 Jérémie 25.10 Esaïe 4.1
64 Makuhani wao walianguka kwa upanga, Wala wajane wao hawakuomboleza.
Job 27.15 1 Samuel 4.17 Ezéchiel 24.23 1 Samuel 4.11 1 Samuel 2.33-2.34
65 Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;
Psaumes 44.23 Esaïe 42.13-42.14 Esaïe 51.9 Psaumes 7.6 Psaumes 73.20
66 Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, Akawatia aibu ya milele.
1 Samuel 5.6 Job 40.12 1 Samuel 6.4 Jérémie 23.40
67 Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.
1 Samuel 6.21-7.1 2 Samuel 6.17 2 Samuel 6.2
68 Bali aliichagua kabila ya Yuda, Mlima Sayuni alioupenda.
Psaumes 87.2 1 Samuel 16.1 Genèse 49.8-49.10 Ruth 4.17-4.22 2 Chroniques 6.6
69 Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.
Colossiens 1.16-1.17 Apocalypse 20.11 1 Chroniques 29.19 1 Rois 9.8 2 Chroniques 2.9
70 Akamchagua Daudi, mtumishi wake, Akamwondoa katika mazizi ya kondoo.
1 Samuel 16.11-16.12 Exode 3.1 1 Rois 19.19-19.20 2 Samuel 6.21 Exode 3.10
71 Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake.
2 Samuel 5.2 1 Samuel 2.7-2.8 Psaumes 28.9 Esaïe 40.11 1 Chroniques 11.2
72 Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.
1 Rois 9.4 2 Corinthiens 3.5-3.6 Zacharie 11.15-11.17 2 Samuel 8.15 1 Rois 15.5

Cette Bible est dans le domaine public.