Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 7.8
Bible en Swahili de l’est


1 Je! Mtu hana wakati wake wa vita juu ya nchi? Na siku zake, je! Si kama siku za mwajiriwa?
Job 14.5-14.6 Psaumes 39.4 Job 14.13-14.14 Jean 11.9-11.10 Matthieu 20.1-20.15
2 Kama mtumishi atamaniye sana kile kivuli, Kama mwajiriwa anayetazamia mshahara wake;
Lévitique 19.13 Jérémie 6.4 Deutéronome 24.15 Malachie 3.5 Psaumes 143.6
3 Ni vivyo nami nimepewa miezi ya ubatili iwe fungu langu, Nami nimeandikiwa masiku yenye kuchokesha.
Psaumes 6.6 Job 29.2 Ecclésiaste 1.14 Job 16.7 Psaumes 39.5
4 Hapo nilalapo chini, nasema, Nitaondoka lini? Lakini usiku huwa mrefu; Nami nimejawa na kujitupa huku na huku hata kupambazuke.
Deutéronome 28.67 Job 7.13-7.14 Psaumes 6.6 Psaumes 109.23 Psaumes 77.4
5 Mwili wangu unavikwa mabuu na madongoa ya udongo; Ngozi yangu hufumba, kisha ikatumbuka tena.
Job 17.14 Esaïe 14.11 Job 2.7-2.8 Psaumes 38.5-38.7 Actes 12.23
6 Siku zangu hupita upesi kuliko chombo cha kufumia, Nazo zapita pasipokuwa na matumaini.
Job 9.25 Job 17.15 Job 17.11 Esaïe 38.12-38.13 1 Pierre 1.24
7 Kumbuka ya kwamba maisha yangu ni upepo; Jicho langu halitaona mema tena.
Psaumes 78.39 Jacques 4.14 Job 10.9 Néhémie 1.8 Psaumes 89.50
8 Jicho lake huyo anionaye halitaniangalia tena; Macho yako yatanielekea, lakini sitakuwapo.
Job 20.9 Psaumes 37.36 Job 14.3 Psaumes 90.8-90.9 Job 8.18
9 Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa.
2 Samuel 12.23 Job 16.22 Job 14.10-14.14 Job 30.15 Job 10.21
10 Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena.
Job 8.18 Job 20.9 Psaumes 103.16 Job 27.23 Job 27.21
11 Kwa hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitanena kwa mateso ya roho yangu; Nitalia kwa uchungu wa nafsi yangu.
Psaumes 40.9 Job 10.1 1 Samuel 1.10 Job 21.25 Esaïe 38.15
12 Je! Mimi ni bahari, au je! Ni nyangumi? Hata ukawaweka walinzi juu yangu?
Job 7.17 Job 38.6-38.11 Ezéchiel 32.2-32.3 Job 41.1-41.34 Lamentations 3.7
13 Hapo nisemapo, kitanda changu kitanituza moyo, Malazi yangu yatanipunguzia kuugua kwangu;
Psaumes 6.6 Job 9.27-9.28 Job 7.3-7.4 Psaumes 77.4
14 Ndipo unitishapo kwa ndoto, Na kunitia hofu kwa maono;
Daniel 2.1 Genèse 40.5-40.7 Genèse 41.8 Juges 7.13-7.14 Matthieu 27.19
15 Hata nafsi yangu huchagua kunyongwa, Na kuchagua kifo kuliko maumivu yangu haya.
2 Samuel 17.23 Matthieu 27.5
16 Ninadhoofika; sitaishi sikuzote; Usinisumbue, kwani siku zangu ni uvuvio.
Job 10.1 1 Rois 19.4 Job 14.6 Job 9.21 Psaumes 39.13
17 Je! Mtu ni kitu gani, hata ukamtukuza, Na kumtia moyoni mwako,
Hébreux 2.6 Psaumes 144.3 Psaumes 8.4 Job 7.12 1 Samuel 24.14
18 Na kumwangalia kila asubuhi, Na kumjaribu kila dakika?
1 Pierre 1.7 Daniel 12.10 Job 14.3 Exode 32.34 Jérémie 9.7
19 Je! Hata lini hukomi kuniangalia; Wala kunisumbua hata nimeze mate?
Job 9.18 Job 14.6 Psaumes 6.3 Psaumes 94.3 Psaumes 13.1-13.3
20 Kwamba nimefanya dhambi, nikufanyieje Ee mlinda wanadamu? Mbona umeniweka niwe shabaha yako, Hata nimekuwa mzigo kwa nafsi yangu?
Lamentations 3.12 Psaumes 36.6 Job 33.27 Job 13.26 Job 31.33
21 Nawe, je! Mbona hunisamehe makosa yangu, Na kuniondolea maovu yangu? Kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; Nawe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwapo.
Job 10.14 Daniel 12.2 Job 13.23-13.24 Psaumes 103.15 Osée 14.2

Cette Bible est dans le domaine public.