Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 6.6
Bible en Swahili de l’est


Achèvement de la muraille

1 Basi ikawa, walipoarifiwa Sanbalati, na Tobia, na Geshemu, Mwarabu na adui zetu hao wengine, kwamba nimeujenga ukuta, wala hayakusalia mavunjiko ndani yake; (ijapokuwa hata wakati ule sijaisimamisha milango katika malango);
Néhémie 2.10 Néhémie 2.19 Néhémie 4.1 Néhémie 3.3 Néhémie 3.1
2 Sanbalati na Geshemu wakatuma wajumbe kwangu, wakasema, Njoo, tukutane huko vijijini katika nchi tambarare ya Ono. Walakini wakakusudi kunifanyia mabaya.
1 Chroniques 8.12 Psaumes 37.12 2 Samuel 3.27 Jérémie 41.2 Ezéchiel 33.31
3 Na mimi nikatuma wajumbe kwao, nikasema, Hii ni kazi kubwa ninayoifanya mimi, hata nisiweze kushuka; mbona kazi ikome, hapo ninapoiacha, niwashukie?
Jean 9.4 1 Timothée 4.15-4.16 Matthieu 10.16 Ecclésiaste 9.10 Luc 14.30
4 Nao wakaniletea maneno kama hayo mara nne; nikawajibu maneno kama yale.
Luc 18.5 Proverbes 14.15 1 Corinthiens 15.58 Juges 16.6 Proverbes 7.21
5 Ndipo Sanbalati akamtuma kwangu mtumwa wake vile vile mara ya tano, na barua wazi mkononi mwake;
2 Thessaloniciens 2.10 2 Rois 18.26-18.28 Ephésiens 6.11 2 Corinthiens 11.13-11.15 2 Corinthiens 2.11
6 nayo yakaandikwa humo, Habari imeenea katika mataifa, naye Geshemu asema neno lilo hilo, ya kwamba wewe na Wayahudi mwakusudi kuasi; ndiyo sababu waujenga huo ukuta; nawe wataka kuwamiliki, ndivyo wasemavyo.
Néhémie 2.19 Jean 19.13 Jérémie 9.3-9.6 Romains 3.8 Matthieu 5.11
7 Nawe umewaweka manabii ili wakuhubirie huko Yerusalemu, kusema, Yuko mfalme katika Yuda; basi sasa ataarifiwa mfalme sawasawa na maneno haya. Njoo sasa basi, na tufanye shauri pamoja.
Actes 23.15 2 Samuel 15.10-15.12 Proverbes 26.24-26.26 1 Rois 1.18 Néhémie 6.12-6.13
8 Ndipo mimi nikatuma kwake wajumbe, kusema, Hakukufanyika mambo kama hayo uyasemayo, lakini kwa moyo wako wewe mwenyewe umeyabuni.
Job 13.4 Psaumes 52.2 Daniel 11.27 Psaumes 36.3 Actes 24.12-24.13
9 Kwani hao wote walitaka kutuogofisha, wakisema, Italegea mikono yao katika kazi, isifanyike. Lakini sasa nitaitia mikono yangu nguvu.
Psaumes 138.3 Philippiens 4.13 Jérémie 38.4 1 Samuel 30.6 2 Corinthiens 12.9
10 Nikaingia nyumbani kwa Shemaya, mwana wa Delaya, mwana wa Mehetabeli, aliyekuwa amefungwa; naye akasema, Tukutane nyumbani mwa Mungu, ndani ya hekalu, tukaifunge milango ya hekalu; kwa maana watakuja kukuua; naam, wakati wa usiku watakuja kukuua.
Jérémie 36.5 Malachie 1.10 Ezéchiel 3.24 Psaumes 37.12 Psaumes 120.2-120.3
11 Nami nikasema, Je! Mtu kama mimi nikimbie? Naye ni nani, akiwa kama nilivyo mimi, atakayeingia hekaluni ili kuponya maisha yake? Sitaingia.
Proverbes 28.1 Psaumes 112.8 Luc 13.31-13.33 Philippiens 2.17 Actes 20.24
12 Nikatambua, na tazama, siye Mungu aliyemtuma; lakini amefanya unabii huu kinyume changu; nao Tobia na Sanbalati ndio waliomwajiri.
Ezéchiel 13.22 1 Timothée 3.3 Actes 20.33 Ezéchiel 13.19 2 Pierre 2.3
13 Kwa sababu hii aliajiriwa, ili mimi niogope, nikafanye hivyo na kutenda dhambi, kisha wao wawe nazo habari mbaya, ili wanishutumie.
Jérémie 20.10 Jérémie 18.18 Néhémie 6.6 Proverbes 29.5 Jacques 4.17
14 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, Tobia na Sanbalati sawasawa na hayo matendo yao, na yule nabii mke Noadia, na hao manabii waliosalia, waliotaka kuniogofya.
Néhémie 13.29 2 Timothée 4.14-4.15 Jérémie 14.18 Psaumes 63.1 Ezéchiel 13.16-13.17
15 Basi huo ukuta ukamalizika siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli, katika muda wa siku hamsini na mbili.
Néhémie 4.1-4.2 Esdras 6.15 Daniel 9.25 Psaumes 1.3
16 Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu.
Psaumes 126.2 Néhémie 4.1 Néhémie 2.10 Josué 5.1 Néhémie 4.7
17 Tena siku zile wakuu wa Yuda walimletea Tobia nyaraka nyingi, nazo nyaraka za Tobia zikawafikilia.
Néhémie 5.7 Matthieu 24.10-24.12 Néhémie 13.28 Néhémie 3.5 Michée 7.1-7.6
18 Kwa maana walikuwa watu wengi katika Yuda waliomwapia, kwa sababu alikuwa mkwewe Shekania, mwana wa Ara; naye Yehohanani mwanawe amemwoa binti Meshulamu, mwana wa Berekia.
Esdras 2.5 Néhémie 3.4 Néhémie 7.10 Néhémie 3.30
19 Tena waliyanena mema yake mbele yangu, nayo maneno yangu humwambia yeye. Tobia naye akaniletea mimi nyaraka za kuniogofisha.
Esaïe 37.10-37.14 Actes 4.18-4.21 Jean 15.19 1 Jean 4.5 Jean 7.7

Cette Bible est dans le domaine public.