Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Néhémie 5.1
Bible en Swahili de l’est


Attitude désintéressée de Néhémie

1 Ndipo kukatokea kilio kikuu cha watu, na wake zao, juu ya ndugu zao Wayahudi.
Esaïe 5.7 Deutéronome 15.7-15.11 Actes 7.26 Job 34.28 Job 31.38-31.39
2 Maana, walikuwako watu waliosema, Sisi, na wana wetu na binti zetu, tu wengi; na tupate ngano, tule, tukaishi.
Psaumes 128.2-128.4 Genèse 42.2 Psaumes 127.3-127.5 Genèse 41.57 Malachie 2.2
3 Tena walikuwako wengine waliosema, Tumeweka rehani mashamba yetu, na mizabibu yetu, na nyumba zetu; tupate ngano, kwa sababu ya njaa.
Deutéronome 15.7 Genèse 47.15-47.25 Lévitique 25.35-25.39 Malachie 3.8-3.11
4 Tena walikuwako wengine waliosema, Tumekopa fedha ili kulipa kodi ya mfalme kwa kuweka rehani mashamba yetu, na mizabibu yetu.
Esdras 4.13 Esdras 4.20 1 Rois 9.21 Néhémie 9.37 Esdras 7.24
5 Walakini miili yetu ni kama miili ya ndugu zetu, na watoto wetu kama watoto wao; kumbe! Mnawatia utumwani wana wetu na binti zetu kuwa watumishi, na baadhi ya binti zetu wamekwisha kutiwa utumwani; wala hatuwezi kujiepusha na hayo; maana watu wengine wana mashamba yetu na mizabibu yetu.
2 Rois 4.1 Lévitique 25.39-25.43 Esaïe 58.7 Genèse 37.27 Exode 21.1-21.11
6 Nami nilikasirika sana, niliposikia kilio chao, na maneno hayo.
Exode 11.8 Néhémie 13.8 Néhémie 13.25 Ephésiens 4.26 Nombres 16.15
7 Ndipo nikafanya shauri na nafsi yangu, nikagombana na wakuu na mashehe, nikawaambia, Mnatoza watu riba, kila mtu ndugu yake. Nikakutanisha mkutano mkubwa ili kushindana nao.
Exode 22.25 Lévitique 25.36 Deutéronome 23.19-23.20 2 Chroniques 19.6-19.7 Psaumes 15.5
8 Nikawaambia, Sisi kwa kadiri ya uwezo wetu tumewakomboa ndugu zetu Wayahudi, waliouzwa kwa makafiri; na ninyi mnataka kuwauza ndugu zenu, tena kuwauza ili sisi tuwanunue? Wakanyamaza kimya, wasiweze kusema neno lo lote.
Lévitique 25.47-25.49 2 Corinthiens 8.12 Matthieu 25.15 Matthieu 22.12 Matthieu 25.29
9 Tena nalisema, Neno hili mnalolitenda si jema; je! Haiwapasi ninyi kwenda katika kicho cha Mungu wetu, kwa sababu ya mashutumu ya makafiri adui zetu?
Lévitique 25.36 2 Samuel 12.14 Genèse 42.18 1 Pierre 2.12 Romains 2.24
10 Na mimi pia, na ndugu zangu, na watumishi wangu, twawakopesha fedha na ngano ili kupata faida? Tafadhali na tuliache jambo hili la riba.
Exode 22.25-22.27 2 Corinthiens 6.1 Psaumes 15.5 2 Corinthiens 5.11 Philémon 1.8-1.9
11 Naomba, warudishieni leo hivi mashamba yao, na mashamba yao ya mizabibu, na mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, na lile fungu la mia la fedha, na la ngano, na la divai, na la mafuta, mnalowatoza.
Esaïe 58.6 Néhémie 5.3-5.4 Luc 3.8 Lévitique 6.4-6.5 1 Samuel 12.3
12 Ndipo wakasema, Tutawarudishia, wala hatutataka kitu kwao; tutafanya hivyo, kama ulivyosema. Kisha nikawaita makuhani, nikawaapisha, ya kwamba watafanya kama ahadi hiyo.
Esdras 10.5 2 Chroniques 28.14-28.15 Jérémie 34.8-34.10 Esdras 10.12 2 Rois 23.2-23.3
13 Tena nikakung’uta nguo yangu, nikasema, Mungu na amkung’ute vivyo hivyo kila mtu nyumbani mwake, na kazini mwake, asiyeitimiza ahadi hiyo; naam, na akung’utwe vivyo hivyo, na kuwa hana kitu. Mkutano wote wakasema, Amina; wakamhimidi Bwana. Nao watu wakafanya kama ahadi hiyo.
Actes 18.6 Matthieu 10.14 1 Chroniques 16.36 1 Rois 11.29-11.31 1 Samuel 15.28
14 Tena tangu wakati huo nilipowekwa kuwa liwali wao katika nchi ya Yuda, tangu mwaka wa ishirini hata mwaka wa thelathini na mbili wa Artashasta mfalme, yaani, miaka kumi na miwili, mimi na ndugu zangu hatukula chakula cha liwali.
Néhémie 13.6 Néhémie 2.1 2 Thessaloniciens 3.8-3.9 1 Corinthiens 9.18 Esdras 4.13-4.14
15 Lakini maliwali wa kwanza walionitangulia, wakawalemea watu, wakawatwalia chakula na mvinyo, zaidi ya shekeli arobaini za fedha; tena watumwa wao nao wakatawala juu ya watu; lakini mimi sikufanya hivyo, kwa kuwa nalimcha Mungu.
Néhémie 5.9 Job 31.23 Matthieu 5.47 Proverbes 16.6 1 Samuel 8.15
16 Naam, hata kazi ya ukuta huu tena nikaishika sana, wala hatukununua mashamba; na watumishi wangu wote wakakusanyika huko kazini.
2 Corinthiens 12.16-12.18 Nombres 16.15 Galates 6.9 1 Thessaloniciens 2.5-2.6 Luc 8.15
17 Pamoja na hayo wakawako mezani pangu, katika Wayahudi na mashehe, watu mia na hamsini, zaidi ya wale waliotujia kutoka kwa makafiri waliotuzunguka.
1 Rois 18.19 2 Samuel 9.7 Romains 12.13 1 Pierre 4.9-4.10 Esaïe 32.8
18 Basi, maandalio yaliyoandaliwa kwa siku moja yalikuwa ng’ombe mmoja, na kondoo wazuri sita; tena nikaandaliwa kuku, na mara moja katika siku kumi akiba ya mvinyo ya namna zote; wala kwa hayo yote sikukidai chakula cha liwali, kwa kuwa utumwa ulikuwa mzito juu ya watu hao.
1 Rois 4.22-4.23 Psaumes 37.21 Néhémie 5.14-5.15 Psaumes 37.26
19 Unikumbukie, Ee Mungu wangu, kwa mema, yote niliyowafanyia watu hawa.
Néhémie 13.31 Néhémie 13.22 Néhémie 13.14 Jérémie 29.11 Psaumes 18.23-18.25

Cette Bible est dans le domaine public.