Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 14.3
Bible en Swahili de l’est


Prospérité et victoires de David

1 Naye Hiramu, mfalme wa Tiro, akatuma wajumbe kwa Daudi, akampelekea na mierezi, na waashi, na maseremala, ili wamjengee nyumba.
2 Chroniques 2.3 2 Samuel 5.11-5.16 Esdras 3.7 1 Rois 5.8-5.12 2 Samuel 7.2
2 Daudi akajua ya kwamba Bwana amemweka imara ili amiliki juu ya Israeli, kwa kuwa milki yake imeinuka kwa ajili ya watu wake Israeli.
Nombres 24.7 Psaumes 89.20-89.37 1 Chroniques 17.17 2 Chroniques 2.11 Esther 4.14
3 Tena Daudi akazidi kuoa wake huko Yerusalemu; akazidi Daudi kuzaa wana na binti.
2 Samuel 5.13 Malachie 2.14 1 Rois 11.3 Matthieu 19.4-19.5 Matthieu 19.8
4 Na haya ndiyo majina ya watoto aliozaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani;
1 Chroniques 3.5-3.9 1 Rois 1.13 1 Rois 3.5-3.11 Luc 3.31 2 Samuel 12.24-12.25
5 na Ibhari, na Elishua, na Elpeleti;
1 Chroniques 3.6 2 Samuel 5.15
6 na Noga, na Nefegi, na Yafia;
7 na Elishama, na Eliada, na Elifeleti.
2 Samuel 5.16 1 Chroniques 3.8
8 Na waliposikia hao Wafilisti ya kwamba Daudi ametiwa mafuta ili awe mfalme juu ya Israeli wote, Wafilisti wote wakapanda kumtafuta Daudi; naye Daudi akasikia, akatoka nje kupigana nao.
Psaumes 2.1-2.6 1 Chroniques 11.3 1 Samuel 21.11 2 Samuel 5.3 Apocalypse 11.15-11.18
9 Basi hao Wafilisti walikuwa wamekuja na kuteka nyara katika bonde la Warefai.
1 Chroniques 11.15 1 Chroniques 14.13 Esaïe 17.5 2 Samuel 5.18 2 Samuel 23.13
10 Daudi akamwuliza Mungu, kusema, Je! Nipande juu ya Wafilisti! Utawatia mikononi mwangu? Naye Bwana akamwambia, Panda; kwa kuwa nitawatia mikononi mwako.
Proverbes 3.6 1 Samuel 30.8 2 Samuel 2.1 2 Samuel 5.23 1 Samuel 23.2-23.4
11 Basi wakapanda mpaka Baal-perasimu, Daudi naye akawapiga huko; Daudi akasema, Bwana amewafurikia adui zangu kwa mkono wangu, kama mafuriko ya maji. Basi wakapaita mahali pale jina lake Baal-perasimu.
Esaïe 28.21 Exode 14.28 Psaumes 18.13-18.15 Job 30.14 Psaumes 144.10
12 Nao wakaiacha miungu yao huko; naye Daudi akaamuru, ikateketezwa kwa moto.
Exode 32.20 Deutéronome 7.25 1 Samuel 5.2-5.6 2 Rois 19.18 Exode 12.12
13 Lakini hao Wafilisti wakateka nyara tena mara ya pili bondeni.
1 Chroniques 14.9 2 Samuel 5.22-5.25 1 Rois 20.22
14 Na Daudi akamwuliza Mungu tena; naye Mungu akamwambia, Hutapanda kuwafuata; uwageukie mbali, ukawajie huko kuielekea miforsadi.
Josué 8.2-8.7 Psaumes 27.4 Jean 9.6-9.7 1 Chroniques 14.10
15 Kisha itakuwa utakapoisikia sauti ya kwenda katika vilele vya miforsadi, ndipo utakapokwenda nje vitani; kwa maana ndipo Mungu ametoka mbele yako, awapige jeshi la Wafilisti.
Esaïe 13.4 1 Samuel 14.9-14.22 2 Rois 7.6 Actes 2.2 Juges 7.15
16 Daudi akafanya kama vile Mungu alivyomwamuru; wakawapiga jeshi la Wafilisti toka Geba mpaka Gezeri.
2 Samuel 5.25 Jean 15.14 1 Chroniques 6.67 Genèse 6.22 Josué 16.10
17 Sifa za Daudi zikafika nchi zote; naye Bwana akawaletea mataifa yote hofu yake.
Deutéronome 2.25 Exode 15.14-15.16 2 Chroniques 26.8 Josué 6.27 Josué 9.24

Cette Bible est dans le domaine public.