Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nahum 3.12
Bible en Swahili de l’est


Causes de la destruction de Ninive

1 Ole wake mji wa damu! Umejaa mambo ya uongo na unyang’anyi; mateka hayaondoki.
Nahum 2.12 Sophonie 3.1-3.3 Ezéchiel 24.6-24.9 Habakuk 2.12 Osée 4.2
2 Kelele za mjeledi, kelele za magurudumu yafanyayo kishindo; na farasi wenye kupara-para, na magari ya vita yenye kuruka-ruka;
Jérémie 47.3 Juges 5.22 Nahum 2.3-2.4 Job 39.22-39.25 Esaïe 9.5
3 mpanda farasi akipanda, na upanga ukimeta-meta, na mkuki ukimemetuka; na wingi wa waliouawa, na chungu kubwa ya mizoga; mizoga haina mwisho; wanajikwaa juu ya mizoga yao.
Habakuk 3.11 Esaïe 37.36 Ezéchiel 39.4 Nahum 2.4 2 Rois 19.35
4 Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake.
Esaïe 47.9 Esaïe 47.12-47.13 Ezéchiel 16.25-16.29 Apocalypse 18.2-18.3 Esaïe 23.15-23.17
5 Tazama, mimi ni juu yako, asema Bwana wa majeshi; nami nitafunua marinda yako mbele ya uso wako; nami nitawaonyesha mataifa uchi wako, na falme aibu yako.
Nahum 2.13 Jérémie 13.26 Jérémie 13.22 Ezéchiel 16.37 Esaïe 47.2-47.3
6 Nami nitatupa uchafu uchukizao juu yako, kukufanya uwe mchafu, nami nitakufanya kuwa kitu cha kutazamwa kwa dharau.
Job 9.31 Jérémie 51.37 Malachie 2.9 Nahum 1.14 Hébreux 10.33
7 Hata itakuwa, wote wakutazamao watakukimbia, wakisema, Ninawi umeharibika; ni nani atakayeuhurumia? Nikutafutie wapi wafariji?
Esaïe 51.19 Jérémie 15.5 Jérémie 51.9 Apocalypse 18.10 Lamentations 2.13
8 Je! Wewe u mwema kuliko No-amoni, uliowekwa kati ya mito, uliozungukwa na maji; ambao boma lake lilikuwa bahari, na bahari ilikuwa ukuta wake.
Amos 6.2 Ezéchiel 30.14-30.16 Esaïe 19.5-19.10 Ezéchiel 31.2-31.3 Jérémie 46.25-46.26
9 Kushi na Misri walikuwa nguvu zake, nazo zilikuwa hazina mpaka; Putu na Walibia walikuwa wasaidizi wake.
Ezéchiel 30.5 Ezéchiel 27.10 2 Chroniques 12.3 Esaïe 20.5 Genèse 10.6
10 Hata hivyo alichukuliwa mbali, alikwenda utumwani; watoto wake wachanga walisetwa kwenye maachano ya njia kuu zote; watu wake wenye heshima wakapigiwa kura, na wakuu wake wote wakafungwa kwa minyororo.
Esaïe 20.4 Abdias 1.11 Osée 13.16 Joël 3.3 Esaïe 13.16
11 Tena utalewa, utafichwa; tena utatafuta ngome kwa sababu ya adui.
Esaïe 2.10 Esaïe 49.26 Apocalypse 6.15-6.17 Nahum 1.10 Psaumes 75.8
12 Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva kwanza; ikitikisika zaanguka katika kinywa chake alaye.
Apocalypse 6.13 Habakuk 1.10 Esaïe 28.4
13 Tazama, watu wako walio ndani yako ni wanawake; malango ya nchi yako yamekuwa wazi kabisa mbele ya adui zako; moto umeteketeza mapingo yako.
Jérémie 51.30 Esaïe 19.16 Jérémie 50.37 Nahum 2.6 Esaïe 45.1-45.2
14 Teka maji yawe tayari kwa kuzingirwa kwako; Zitie nguvu ngome zako; Ingia katika udongo, yakanyage matope, Itie nguvu tanuru ya kuokea matofali.
Nahum 2.1 2 Chroniques 32.3-32.4 Esaïe 8.9 Esaïe 22.9-22.11 2 Chroniques 32.11
15 Huko moto utakuteketeza; Upanga utakukatilia mbali; Utakumeza kama tunutu alavyo; Jifanye kuwa wengi kama tunutu! Jifanye kuwa wengi kama nzige!
Joël 1.4 Nahum 2.13 Nahum 3.13 Joël 2.25 Sophonie 2.13
16 Umeongeza wafanya biashara wako kuwa wengi kuliko nyota za mbinguni; tunutu huharibu; kisha huruka juu na kwenda zake.
Genèse 15.5 Néhémie 9.23 Jérémie 33.22 Genèse 22.17
17 Watu wako waliotiwa taji ni kama nzige, na majemadari wako ni kama makundi ya mapanzi, watuao katika vitalu siku ya baridi, lakini jua lipandapo huruka juu na kwenda zao, na mahali pao walipo hapajulikani.
Jérémie 51.27 Apocalypse 9.7
18 Wachungaji wako wanalala usingizi, Ee mfalme wa Ashuru; watu wako wenye heshima wamepumzika; watu wako wametawanyika juu ya milima, wala hapana mtu wa kuwakusanya.
1 Rois 22.17 Psaumes 76.5-76.6 Jérémie 50.18 Jérémie 51.57 Esaïe 13.14
19 Jeraha yako haipunguziki; jeraha yako ni nzito sana; wote wasikiao habari zako wapiga makofi juu yako; kwa maana ni nani ambaye uovu wako haukupita juu yake daima?
Lamentations 2.15 Michée 1.9 Job 27.23 Esaïe 37.18 Jérémie 46.11

Cette Bible est dans le domaine public.