Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lévitique 17.5
Bible en Swahili de l’est


La consommation de viande et de sang

1 Bwana akamwambia Musa, akisema,
2 Sema na Haruni, na wanawe, na wana wote wa Israeli, ukawaambie; Neno hili ndilo aliloliamuru Bwana, akisema,
3 Mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli atakayechinja ng’ombe, au mwana-kondoo, au mbuzi, ndani ya marago, au atakayemchinja nje ya marago,
Deutéronome 12.26-12.27 Lévitique 17.15 Deutéronome 12.20-12.22 Deutéronome 12.11-12.15 Lévitique 17.8
4 wala hamleti mlangoni pa hema ya kukutania, ili amtoe kuwa matoleo kwa Bwana mbele ya hema ya Bwana; mtu huyo atahesabiwa kuwa ana hatia ya damu; amemwaga damu; na mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake;
Genèse 17.14 Lévitique 18.29 Lévitique 17.14 Romains 4.6 Psaumes 32.2
5 ili kusudi wana wa Israeli walete sadaka zao, wazichinjazo mashambani, naam, wazilete kwa Bwana, mpaka mlango wa hema ya kukutania, kwa huyo kuhani, ili wazichinje ziwe sadaka za amani kwa Bwana.
2 Rois 17.10 Genèse 31.54 Genèse 21.33 2 Rois 16.4 2 Chroniques 28.4
6 Naye kuhani atainyunyiza damu yake juu ya madhabahu ya Bwana, mlangoni pa hema ya kukutania, na kuyateketeza mafuta yake, yawe harufu njema mbele za Bwana.
Nombres 18.17 Lévitique 3.2 Lévitique 3.16 Exode 29.18 Lévitique 3.11
7 Wala hawatatoa tena sadaka zao kwa wale majini, ambao huwafuata ili wafanye uasherati nao. Sheria hii itakuwa sheria ya milele kwao, kizazi baada ya kizazi.
Exode 34.15 1 Corinthiens 10.20 2 Chroniques 11.15 Deutéronome 32.17 Psaumes 106.37
8 Nawe utawaambia, Mtu awaye yote katika nyumba ya Israeli, au miongoni mwa wageni, wanaokaa nao, atoaye sadaka ya kuteketezwa au dhabihu,
Lévitique 1.2-1.3 2 Samuel 24.25 1 Samuel 7.9 1 Samuel 16.2 1 Rois 18.30-18.38
9 wala haileti mlangoni pa hema ya kukutania, ili aisongeze kwa Bwana basi mtu huyo atatengwa na watu wake.
Lévitique 17.4
10 Kisha mtu awaye yote wa nyumba ya Israeli, au miongoni mwa hao wageni wakaao kati yao, atakayekula damu, ya aina yo yote, nitakunja uso wangu juu ya mtu huyo alaye damu, nami nitamkatilia mbali na watu wake.
Lévitique 3.17 Genèse 9.4 Deutéronome 12.16 Deutéronome 12.23 1 Samuel 14.33
11 Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.
Hébreux 9.22 1 Jean 1.7 Apocalypse 1.5 Matthieu 26.28 Romains 5.9
12 Kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Hapana mtu miongoni mwenu aliye na ruhusa kula damu, wala mgeni aketiye kati yenu asile damu.
Exode 12.49
13 Mtu ye yote aliye wa wana wa Israeli, au wa hao wageni wakaao kati yenu, ambaye amemshika mnyama, au ndege ambaye huliwa, katika kuwinda kwake; atamwaga damu yake, na kuifunika mchanga.
Deutéronome 12.16 Ezéchiel 24.7 Deutéronome 15.23 Lévitique 7.26 Deutéronome 12.24
14 Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila awaye yote atakatiliwa mbali.
Genèse 9.4 Deutéronome 12.23 Lévitique 17.11-17.12
15 Tena kila mtu atakayekula nyamafu, au nyama aliyeraruliwa na wanyama, kama ni mzalia, kama ni mgeni, atafua nguo zake, na kuoga majini, naye atakuwa najisi hata jioni; ndipo atakapokuwa safi.
Exode 22.31 Deutéronome 14.21 Lévitique 22.8 Lévitique 15.5 Lévitique 11.25
16 Lakini kwamba hazifui, wala haogi mwili, ndipo atakapochukua uovu wake.
Lévitique 5.1 Esaïe 53.11 Lévitique 20.19-20.20 1 Pierre 2.24 Lévitique 19.8

Cette Bible est dans le domaine public.