Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 12.9
Bible en Swahili de l’est


Appel à la persévérance

1 Wakati huo Mikaeli atasimama, jemadari mkuu, asimamaye upande wa wana wa watu wako; na kutakuwa na wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo; na wakati huo watu wako wataokolewa; kila mmoja atakayeonekana ameandikwa katika kitabu kile.
Matthieu 24.21 Jérémie 30.7 Marc 13.19 Daniel 10.13 Daniel 10.21
2 Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele.
Jean 5.28-5.29 Matthieu 25.46 Ezéchiel 37.12 Esaïe 26.19 Ezéchiel 37.1-37.4
3 Na walio na hekima watang’aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang’aa kama nyota milele na milele.
Daniel 11.33 Matthieu 13.43 Daniel 11.35 Proverbes 4.18 1 Thessaloniciens 2.19-2.20
4 Lakini wewe, Ee Danielii, yafunge maneno haya, ukakitie muhuri kitabu, hata wakati wa mwisho; wengi wataenda mbio huko na huko, na maarifa yataongezeka.
Daniel 12.9 Daniel 8.26 Apocalypse 22.10 Daniel 8.17 Esaïe 8.16
5 Ndipo mimi, Danielii, nikatazama, na kumbe, wamesimama wengine wawili, mmoja ukingoni mwa mto upande huu, na mmoja ukingoni mwa mto upande wa pili.
Daniel 10.10 Daniel 10.16 Daniel 10.4-10.6
6 Na mmoja akamwuliza yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, Je! Itakuwa muda wa miaka mingapi hata mwisho wa mambo haya ya ajabu?
Daniel 8.13 Ezéchiel 9.2 Daniel 8.16 Zacharie 1.12-1.13 Apocalypse 10.2-10.5
7 Nami nikamsikia yule mtu aliyevikwa nguo za kitani, aliyekuwa juu ya maji ya mto, hapo alipoinua mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto kuelekea mbinguni; akaapa kwa yeye aliye hai milele na milele, ya kwamba itakuwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati; tena watakapokuwa wamekwisha kuvunja nguvu za hao watu watakatifu, ndipo mambo hayo yote yatakapotimizwa.
Daniel 7.25 Daniel 8.24 Apocalypse 10.5-10.7 Apocalypse 12.14 Apocalypse 11.2-11.3
8 Nami nikasikia, lakini sikuelewa; ndipo nikasema, Ee Bwana wangu, mwisho wa mambo haya utakuwaje?
Actes 1.7 Daniel 10.14 1 Pierre 1.11 Luc 18.34 Jean 12.16
9 Akasema, Enenda zako, Danielii; maana maneno haya yamefungwa, na kutiwa muhuri, hata wakati wa mwisho.
Daniel 12.4 Apocalypse 10.4 Esaïe 8.16 Daniel 8.26 Esaïe 29.11
10 Wengi watajitakasa, na kujifanya weupe, na kusafika; bali wabaya watatenda mabaya; wala hataelewa mtu mbaya awaye yote; bali wao walio na hekima ndio watakaoelewa.
Daniel 11.35 Apocalypse 22.11 Osée 14.9 Jean 8.47 Zacharie 13.9
11 Na tangu wakati ule ambapo sadaka ya kuteketezwa ya daima itaondolewa, na hilo chukizo la uharibifu litakaposimamishwa, itapata siku elfu na mia mbili na tisini.
Daniel 11.31 Matthieu 24.15 Daniel 9.27 Marc 13.14 Apocalypse 11.2
12 Heri angojaye, na kuzifikilia siku hizo elfu na mia tatu na thelathini na tano.
Apocalypse 20.4 Daniel 8.14 Esaïe 30.18 Romains 11.15
13 Lakini enenda zako hata utakapokuwa mwisho ule; maana wewe utastarehe, nawe utasimama katika kura yako mwisho wa siku hizo.
Apocalypse 14.13 Luc 2.29-2.30 Zacharie 3.7 2 Timothée 4.7-4.8 Luc 21.36

Cette Bible est dans le domaine public.