Mission d’Ézéchiel
 1 Akaniambia, Mwanadamu, simama kwa miguu yako, nami nitasema nawe.
Daniel 10.11  Ezéchiel 4.1  Ezéchiel 5.1  Actes 9.6  Ezéchiel 3.1  
 2 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami.
Ezéchiel 3.24  Daniel 8.18  1 Samuel 16.13  Nombres 11.25-11.26  Juges 13.25  
 3 Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo.
Jérémie 3.25  1 Samuel 8.7-8.8  Ezéchiel 16.1-16.63  Ezéchiel 20.1-20.49  Jérémie 7.2  
 4 Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi.
Ezéchiel 3.7  Jérémie 5.3  Psaumes 95.8  Esaïe 48.4  Jérémie 6.15  
 5 Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao.Ezéchiel 33.33  Ezéchiel 3.27  Ezéchiel 2.7  Matthieu 10.12-10.15  Jean 15.22  
 6 Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.
Jérémie 1.17  Jérémie 1.8  Michée 7.4  2 Samuel 23.6-23.7  Esaïe 9.18  
 7 Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
Ezéchiel 3.10  Jérémie 23.28  Ezéchiel 3.17  Jérémie 1.7  Jérémie 1.17  
 8 Bali wewe, mwanadamu, sikia neno hili ninalokuambia; usiwe wewe mwenye kuasi kama nyumba ile yenye kuasi; funua kinywa chako, ule nikupacho.
Apocalypse 10.9  Jérémie 15.16  Esaïe 50.5  1 Timothée 4.14-4.16  Lévitique 10.3  
 9 Nami nilipotazama, mkono ulinyoshwa kunielekea; na tazama, gombo la chuo lilikuwa ndani yake.
Ezéchiel 8.3  Ezéchiel 3.1  Daniel 10.10  Apocalypse 10.8-10.11  Apocalypse 5.1-5.5  
 10 Akalikunjua mbele yangu; nalo lilikuwa limeandikwa ndani na nje; ndani yake yalikuwa yameandikwa maombolezo, na vilio, na ole!
Apocalypse 8.13  Esaïe 3.11  Apocalypse 9.12  Apocalypse 11.14  Jérémie 36.29-36.32