Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 2
Bible en Swahili de l’est


Mission d’Ézéchiel

1 Akaniambia, Mwanadamu, simama kwa miguu yako, nami nitasema nawe.
Daniel 10.11 Ezéchiel 3.17 Ezéchiel 3.4 Ezéchiel 4.1 Ezéchiel 5.1
2 Naye aliposema nami, roho ikaniingia, ikanisimamisha; nikamsikia yeye aliyesema nami.
Ezéchiel 3.24 Daniel 8.18 Néhémie 9.30 Ezéchiel 36.27 Ezéchiel 3.14
3 Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo.
Jérémie 3.25 1 Samuel 8.7-8.8 Jérémie 36.2 Nombres 32.13-32.14 Nombres 20.10
4 Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi.
Ezéchiel 3.7 Jérémie 6.15 Jérémie 5.3 Psaumes 95.8 Esaïe 48.4
5 Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao.
Ezéchiel 33.33 Ezéchiel 3.27 Jean 15.22 Actes 13.46 Ezéchiel 2.7
6 Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.
Jérémie 1.8 Michée 7.4 Jérémie 1.17 2 Samuel 23.6-23.7 Esaïe 9.18
7 Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
Ezéchiel 3.10 Jérémie 1.17 Jérémie 23.28 Ezéchiel 3.17 Jérémie 1.7
8 Bali wewe, mwanadamu, sikia neno hili ninalokuambia; usiwe wewe mwenye kuasi kama nyumba ile yenye kuasi; funua kinywa chako, ule nikupacho.
Apocalypse 10.9 Jérémie 15.16 Esaïe 50.5 Ezéchiel 3.1-3.3 Ezéchiel 3.10
9 Nami nilipotazama, mkono ulinyoshwa kunielekea; na tazama, gombo la chuo lilikuwa ndani yake.
Ezéchiel 8.3 Daniel 10.10 Apocalypse 10.8-10.11 Apocalypse 5.1-5.5 Ezéchiel 3.1
10 Akalikunjua mbele yangu; nalo lilikuwa limeandikwa ndani na nje; ndani yake yalikuwa yameandikwa maombolezo, na vilio, na ole!
Apocalypse 8.13 Esaïe 3.11 Esaïe 30.8-30.11 Habakuk 2.2 Apocalypse 9.12

Cette Bible est dans le domaine public.