Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ezéchiel 15
Bible en Swahili de l’est


1 Neno la Bwana likanijia, kusema, 2 Mwanadamu, mzabibu una sifa gani kuliko mti mwingine, au tawi la mzabibu lililokuwa kati ya miti ya msituni? Esaïe 5.1-5.7 Osée 10.1 Psaumes 80.8-80.16 Jean 15.1-15.6 Jérémie 2.21
3 Je! Mti wake waweza kutwaliwa, ili kufanya kazi yo yote? Watu waweza kufanya chango kwa huo, ili kutundika chombo cho chote? Marc 9.50 Matthieu 5.13 Luc 14.34-14.35 Jérémie 24.8
4 Tazama, watupwa motoni kwa kuni moto umeziteketeza ncha zake zote mbili, nao umeteketea katikati, je! Wafaa kwa kazi yo yote? Jean 15.6 Esaïe 27.11 Hébreux 6.8 Ezéchiel 19.14 Esaïe 1.31
5 Tazama, ulipokuwa mzima, haukufaa kwa kazi yo yote; sembuse ukiisha kuliwa na moto, na kuteketea; je! Waweza kufaa kwa kazi yo yote? Jérémie 3.16
6 Basi Bwana MUNGU asema hivi; Kama mzabibu kati ya miti ya msituni, niliyoupa moto uwe kuni, ndivyo nitakavyowatoa wakaao Yerusalemu. Esaïe 5.1-5.6 Jérémie 44.21-44.27 Jérémie 24.8-24.10 Jérémie 7.20 Jérémie 21.7
7 Nami nitaukaza uso wangu juu yao; nao watatoka motoni, lakini moto utawateketeza; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoukaza uso wangu juu yao. Ezéchiel 14.8 Psaumes 34.16 Esaïe 24.18 Amos 9.1-9.4 1 Rois 19.17
8 Nami nitaifanya nchi kuwa ukiwa, kwa sababu wamekosa, asema Bwana MUNGU. Ezéchiel 6.14 Ezéchiel 33.29 Ezéchiel 17.20 Jérémie 25.10-25.11 Ezéchiel 14.13-14.21

Cette Bible est dans le domaine public.