Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 20.15
Bible en Swahili de l’est


1 Basi Pashuri, mwana wa Imeri, kuhani, aliyekuwa msimamizi mkuu katika nyumba ya Bwana, alimsikia Yeremia alipokuwa akitabiri maneno hayo.
1 Chroniques 24.14 2 Rois 25.18 Esdras 2.37-2.38 2 Chroniques 35.8 Néhémie 7.40-7.41
2 Ndipo Pashuri akampiga Yeremia, nabii, akamtia katika mkatale, uliokuwa pale penye lango la juu la Benyamini, lililokuwa katika nyumba ya Bwana.
Jérémie 37.13 Jérémie 1.19 2 Chroniques 16.10 Zacharie 14.10 1 Rois 22.27
3 Hata ikawa, asubuhi, Pashuri huyo akamtoa Yeremia katika mkatale. Ndipo Yeremia akamwambia, Bwana hakukuita jina lako Pashuri, bali Magor-misabibu.
Jérémie 20.10 Psaumes 31.13 Jérémie 46.5 Esaïe 8.3 Jérémie 6.25
4 Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitakufanya kuwa hofu kuu kwa nafsi yako, na kwa rafiki zako wote; nao wataanguka kwa upanga wa adui zao, na macho yako yataona hayo; nami nitatia Yuda yote katika mikono ya mfalme wa Babeli, naye atawachukua mateka mpaka Babeli, na kuwaua kwa upanga.
Jérémie 29.21 Jérémie 21.4-21.10 Jérémie 25.9 Jérémie 39.6-39.7 Job 18.11-18.21
5 Tena mali zote za mji huu, na mapato yake yote, na vitu vyake vya thamani vyote pia, naam, hazina zote za wafalme wa Yuda, nitavitia katika mikono ya adui zao, watakaowateka nyara, na kuwakamata, na kuwachukua mpaka Babeli.
Jérémie 15.13 Ezéchiel 22.25 Jérémie 17.3 2 Rois 25.13-25.17 Lamentations 1.10
6 Na wewe, Pashuri, na watu wote wanaokaa katika nyumba yako, mtakwenda utumwani; nawe utafika Babeli, na huko utakufa, na huko utazikwa, wewe, na rafiki zako wote, uliowatabiria maneno ya uongo.
Jérémie 14.14-14.15 Lamentations 2.14 Jérémie 20.4 Ezéchiel 22.28 Jérémie 23.14-23.17
7 Ee Bwana, umenihadaa, nami nimehadaika; wewe una nguvu kuliko mimi, ukashinda; nimekuwa kitu cha kuchekesha, mchana kutwa; kila mtu hunidhihaki.
Lamentations 3.14 Psaumes 22.6-22.7 Ezéchiel 3.14 Psaumes 69.9-69.12 1 Corinthiens 4.9-4.13
8 Maana kila ninenapo napiga kelele, nalia, Dhuluma na uharibifu! Kwa kuwa neno la Bwana limefanywa shutumu kwangu, na dhihaka, mchana kutwa.
Jérémie 6.10 2 Chroniques 36.16 Jérémie 18.16-18.17 Jérémie 20.7 Jérémie 15.1-15.4
9 Nami nikisema, Sitamtaja, wala sitasema tena kwa jina lake; basi, ndipo moyoni mwangu kumekuwamo kama moto uwakao, uliofungwa ndani ya mifupa yangu, nami nimechoka kwa kustahimili, wala siwezi kujizuia.
Psaumes 39.3 Job 32.18-32.20 Actes 4.20 Ezéchiel 3.14 Jérémie 6.11
10 Maana nimesikia mashutumu ya watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake.
Psaumes 41.9 Psaumes 31.13 Esaïe 29.21 Jérémie 18.18 1 Rois 19.2
11 Lakini Bwana yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe.
Jérémie 15.20 Jérémie 1.8 Jérémie 17.18 Jérémie 1.19 Psaumes 35.26
12 Lakini, Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.
Jérémie 11.20 Psaumes 62.8 Psaumes 54.7 Psaumes 59.10 Jérémie 17.10
13 Mwimbieni Bwana; msifuni Bwana; Kwa maana ameiponya roho ya mhitaji Katika mikono ya watu watendao maovu.
Psaumes 69.33 Psaumes 109.30-109.31 Psaumes 34.6 Esaïe 25.4 Psaumes 35.9-35.11
14 Na ilaaniwe siku niliyozaliwa, isibarikiwe siku ile aliyonizaa mama yangu.
Jérémie 15.10 Job 3.3-3.16
15 Na alaaniwe mtu yule aliyemletea baba yangu habari, akisema, Umezaliwa mtoto mwanamume; akimfurahisha.
Luc 1.14 Genèse 21.5-21.6 Jérémie 1.5
16 Mtu huyo na awe kama miji ile, ambayo Bwana aliiangamiza, asijute; na asikie kilio asubuhi, na kelele za fujo adhuhuri;
Jérémie 18.22 Jérémie 48.3-48.4 Deutéronome 29.23 Jérémie 4.19 Jonas 4.2
17 kwa sababu hakuniua nilipotoka tumboni, na hivyo mama yangu angekuwa kaburi langu, na mimba yake sikuzote nzito.
Job 10.18-10.19 Job 3.10-3.11 Ecclésiaste 6.3 Job 3.16
18 Nalitoka tumboni kwa sababu gani, kuona taabu na huzuni, hata siku zangu ziharibike katika aibu?
Job 3.20 Job 14.1 Lamentations 3.1 Psaumes 69.19 Psaumes 90.9-90.10

Cette Bible est dans le domaine public.