Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 58.12
Bible en Swahili de l’est


Le vrai jeûne

1 Piga kelele, usiache, Paza sauti yako kama tarumbeta; Uwahubiri watu wangu kosa lao, Na nyumba ya Yakobo dhambi zao.
Michée 3.8-3.12 Actes 20.26-20.27 Ezéchiel 20.4 Tite 2.15 Actes 7.51-7.52
2 Walakini wanitafuta kila siku; hupenda kujua njia zangu; kama vile taifa waliotenda haki, wasioacha sheria ya Mungu wao, hutaka kwangu amri za haki; hufurahi kumkaribia Mungu.
Esaïe 29.13 Tite 1.16 Matthieu 15.7-15.9 Marc 4.16-4.17 Jacques 1.21-1.22
3 Husema, Mbona tumefunga, lakini huoni? Mbona tumejitaabisha nafsi zetu, lakini huangalii? Fahamuni, siku ya kufunga kwenu mnatafuta anasa zenu wenyewe, na kuwalemea wote watendao kazi kwenu.
Malachie 3.14 Lévitique 16.29 Luc 18.9-18.12 Néhémie 5.7 Zacharie 7.5-7.7
4 Tazama, ninyi mwafunga mpate kushindana na kugombana, na kupiga kwa ngumi ya uovu. Hamfungi siku hii ya leo hata kuisikizisha sauti yenu juu.
Joël 2.13-2.14 Proverbes 21.27 1 Rois 21.9-21.13 Philippiens 1.14-1.15 Matthieu 6.16-6.18
5 Je! Kufunga namna hii ni saumu niliyoichagua mimi? Je! Ni siku ya mtu kujitaabisha nafsi yake? Ni kuinama kichwa kama unyasi, na kutanda nguo za magunia na majivu chini yake? Je! Utasema ni siku ya kufunga, na ya kukubaliwa na Bwana?
Zacharie 7.5 Daniel 9.3-9.19 Job 2.8 Esaïe 61.2 Lévitique 16.29
6 Je! Saumu niliyoichagua, siyo ya namna hii? Kufungua vifungo vya uovu, kuzilegeza kamba za nira, kuwaacha huru walioonewa, na kwamba mvunje kila nira?
Néhémie 5.10-5.12 Esaïe 58.9 Jérémie 34.8-34.11 1 Timothée 6.1 Michée 3.2-3.4
7 Je! Siyo kuwagawia wenye njaa chakula chako, na kuwaleta maskini waliotupwa nje nyumbani kwako? Umwonapo mtu aliye uchi, umvike nguo; wala usijifiche na mtu mwenye damu moja nawe?
Ezéchiel 18.7 Luc 3.11 Ezéchiel 18.16 Esaïe 58.10 1 Jean 3.17-3.18
8 Ndipo nuru yako itakapopambazuka kama asubuhi, na afya yako itatokea mara; na haki yako itakutangulia; utukufu wa Bwana utakufuata nyuma ukulinde.
Jérémie 33.6 Psaumes 37.6 Esaïe 52.12 Actes 10.35 Malachie 4.2
9 Ndipo utaita, na Bwana ataitika; utalia, naye atasema, Mimi hapa. Kama ukiiondoa nira; isiwepo kati yako, wala kunyosha kidole, wala kunena maovu;
Psaumes 50.15 Psaumes 12.2 Esaïe 65.24 Proverbes 6.13 Psaumes 91.15
10 na kama ukimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi yako, na kuishibisha nafsi iliyoteswa; ndipo nuru yako itakapopambazuka gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri.
Job 11.17 Psaumes 37.6 Esaïe 58.7-58.8 Proverbes 11.24-11.25 Esaïe 42.16
11 Naye Bwana atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.
Jérémie 31.12 Esaïe 49.10 Jean 4.14 Osée 13.5 Proverbes 11.25
12 Na watu wako watapajenga mahali palipokuwa ukiwa; utaiinua misingi ya vizazi vingi; nawe utaitwa, Mwenye kutengeneza mahali palipobomoka; na, Mwenye kurejeza njia za kukalia.
Esaïe 61.4 Amos 9.14 Amos 9.11 Esaïe 51.3 Ezéchiel 36.33
13 Kama ukigeuza mguu wako usihalifu sabato, usifanye anasa yako siku ya utakatifu wangu; ukiita sabato siku ya furaha, na siku takatifu ya Bwana yenye heshima; ukiitukuza, kwa kutokuzifanya njia zako mwenyewe, wala kuyatafuta yakupendezayo, wala kusema maneno yako mwenyewe;
Psaumes 84.10 Jérémie 17.21-17.27 Psaumes 84.2 Psaumes 92.1-92.2 Psaumes 27.4
14 ndipo utakapojifurahisha katika Bwana; nami nitakupandisha mahali pa nchi palipoinuka; nitakulisha urithi wa Yakobo baba yako; kwa maana kinywa cha Bwana kimenena hayo.
Deutéronome 32.13 Job 22.26 Habakuk 3.18-3.19 Esaïe 1.19-1.20 Esaïe 33.16

Cette Bible est dans le domaine public.