Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 53.2
Bible en Swahili de l’est


1 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?
Jean 12.38 Esaïe 51.9 Romains 10.16-10.17 Ephésiens 1.18-1.19 Romains 1.16-1.18
2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.
Esaïe 52.14 Esaïe 11.1 Philippiens 2.6-2.7 Marc 6.3 1 Pierre 2.14
3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Jean 1.10-1.11 Esaïe 53.10 Esaïe 49.7 Marc 14.34 Zacharie 11.8
4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
1 Pierre 2.24 Matthieu 8.17 Galates 3.13 1 Jean 2.2 Esaïe 53.5-53.6
5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
1 Pierre 2.24-2.25 1 Pierre 3.18 Romains 5.6-5.10 Matthieu 20.28 Romains 4.25
6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
1 Pierre 2.25 1 Pierre 3.18 Psaumes 119.176 Romains 4.25 Romains 3.10-3.19
7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.
Actes 8.32-8.33 Matthieu 26.63 Marc 14.61 1 Pierre 2.23 Jean 19.9
8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
Actes 8.33 Daniel 9.26 Jean 11.49-11.52 Matthieu 1.1 Esaïe 53.12
9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
Matthieu 27.57-27.60 1 Pierre 2.22 Hébreux 4.15 1 Jean 3.5 Marc 15.43-15.46
10 Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;
Esaïe 9.7 Hébreux 13.10-13.12 Matthieu 17.5 Zacharie 13.7 Luc 1.33
11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.
Romains 5.18-5.19 1 Jean 2.1 Jean 16.21 Esaïe 53.4-53.6 Esaïe 53.8
12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji.
Luc 22.37 Marc 15.27 Esaïe 53.6 Luc 23.32-23.34 Daniel 2.45

Cette Bible est dans le domaine public.