1 Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?Jean 12.38  Esaïe 51.9  Romains 10.16-10.17  Ephésiens 1.18-1.19  Romains 1.16-1.18  
 2 Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani.
Esaïe 52.14  Esaïe 11.1  Philippiens 2.6-2.7  Marc 6.3  1 Pierre 2.14  
 3 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.
Esaïe 53.10  Esaïe 49.7  Jean 1.10-1.11  Marc 14.34  Luc 18.31-18.33  
 4 Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa.
1 Pierre 2.24  Matthieu 8.17  Galates 3.13  1 Jean 2.2  Esaïe 53.5-53.6  
 5 Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
1 Pierre 2.24-2.25  1 Pierre 3.18  Romains 5.6-5.10  Matthieu 20.28  Romains 4.25  
 6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; Kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; Na Bwana ameweka juu yake Maovu yetu sisi sote.
1 Pierre 2.25  1 Pierre 3.18  Psaumes 119.176  Romains 4.25  Romains 3.10-3.19  
 7 Alionewa, lakini alinyenyekea, Wala hakufunua kinywa chake; Kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, Na kama vile kondoo anyamazavyo Mbele yao wakatao manyoya yake; Naam, hakufunua kinywa chake.
Actes 8.32-8.33  Matthieu 26.63  Marc 14.61  1 Pierre 2.23  Jean 19.9  
 8 Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu.
Actes 8.33  Daniel 9.26  Matthieu 1.1  Esaïe 53.12  Jean 19.7  
 9 Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.
Matthieu 27.57-27.60  1 Pierre 2.22  Hébreux 4.15  1 Jean 3.5  Esaïe 42.1-42.3  
 10 Lakini Bwana aliridhika kumchubua; Amemhuzunisha; Utakapofanya nafsi yake kuwa dhabihu kwa dhambi, Ataona uzao wake, ataishi siku nyingi, Na mapenzi ya Bwana yatafanikiwa mkononi mwake;
Esaïe 9.7  Hébreux 13.10-13.12  Matthieu 17.5  Zacharie 13.7  Luc 1.33  
 11 Ataona mazao ya taabu ya nafsi yake, na kuridhika. Kwa maarifa yake mtumishi wangu mwenye haki Atawafanya wengi kuwa wenye haki; Naye atayachukua maovu yao.
Romains 5.18-5.19  Esaïe 53.4-53.6  Esaïe 53.8  Jean 17.3  Esaïe 45.25  
 12 Kwa hiyo nitamgawia sehemu pamoja na wakuu, Naye atagawanya nyara pamoja nao walio hodari; Kwa sababu alimwaga nafsi yake hata kufa, Akahesabiwa pamoja na hao wakosao. Walakini alichukua dhambi za watu wengi, Na kuwaombea wakosaji.
Luc 22.37  Marc 15.27  Esaïe 53.6  Luc 23.32-23.34  Daniel 2.45