Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ecclésiaste 5.20
Bible en Swahili de l’est


1 Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya.
Proverbes 15.8 Exode 3.5 Hébreux 12.28-12.29 Josué 5.15 Osée 6.6-6.7
2 Usiseme maneno ya ujinga kwa kinywa chako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu yuko mbinguni, na wewe upo chini, Kwa hiyo maneno yako na yawe machache.
Proverbes 10.19 Matthieu 6.7 Esaïe 55.9 Genèse 18.27 Jacques 3.2
3 Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.
Proverbes 15.2 Proverbes 10.19 Job 11.2 Ecclésiaste 10.12-10.14
4 Wewe ukimwekea Mungu nadhiri, usikawie kuiondoa; kwa kuwa yeye hawi radhi na wapumbavu; basi, uiondoe hiyo uliyoiweka nadhiri.
Psaumes 66.13-66.14 Psaumes 76.11 Nombres 30.2 Psaumes 50.14 Matthieu 5.33
5 Ni afadhali usiweke nadhiri, Kuliko kuiweka usiiondoe.
Actes 5.4 Proverbes 20.25 Deutéronome 23.22
6 Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako?
Malachie 2.7 Aggée 1.9-1.11 Ecclésiaste 5.1-5.2 Genèse 48.16 Lévitique 5.4-5.6

Incertitude des richesses

7 Maana ndivyo ilivyo katika habari za wingi wa ndoto, na ubatili, na maneno mengi; walakini wewe umche Mungu.
Ecclésiaste 12.13 Ecclésiaste 7.18 Ecclésiaste 8.12 Ecclésiaste 5.3 Proverbes 23.17
8 Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu, Aliye juu kuliko walio juu huangalia; Tena wako walio juu kupita hao.
Psaumes 12.5 Ecclésiaste 4.1 Ecclésiaste 3.16 Psaumes 82.1 Luc 1.32
9 Lakini, pamoja na hayo, manufaa ya nchi kwa kila njia ni mfalme anayejibidiisha kwa ajili ya shamba.
Psaumes 115.16 Jérémie 40.10-40.12 1 Samuel 8.12-8.17 Proverbes 13.23 Genèse 1.29-1.30
10 Apendaye fedha hatashiba fedha, Wala apendaye wingi hatashiba maongeo. Hayo pia ni ubatili.
Matthieu 6.24 1 Timothée 6.10 Ecclésiaste 4.8 Ecclésiaste 2.11 Luc 12.15
11 Mali yakiongezeka, hao walao nao waongezeka na mwenyewe hufaidiwa nini, ila kuyatazama kwa macho yake tu?
1 Jean 2.16 Ecclésiaste 11.9 Genèse 13.2 1 Rois 4.22-4.23 Psaumes 119.36-119.37
12 Usingizi wake kibarua ni mtamu, kwamba amekula kidogo, au kwamba amekula kingi; lakini kushiba kwake tajiri hakumwachi kulala usingizi.
Proverbes 3.24 Jérémie 31.26 Psaumes 4.8 Psaumes 127.2
13 Kuna na balaa mbaya sana niliyoiona chini ya jua, nayo ni hii, mali alizoziweka mwenyewe kwa kujinyima;
Ecclésiaste 6.1-6.2 Genèse 19.14 Luc 12.16-12.21 Genèse 19.26 Genèse 19.31-19.38
14 na mali hizo zimepotea kwa bahati mbaya; naye akiwa amezaa mwana, hamna kitu mkononi mwake.
1 Rois 14.26 1 Samuel 2.36 Psaumes 109.9-109.12 Aggée 1.9 Matthieu 6.19-6.20
15 Alivyotoka tumboni mwa mamaye, atakwenda tena tupu-tupu kama alivyokuja; asichume kitu cho chote kwa ajili ya kazi yake, hata akichukue mkononi mwake.
Job 1.21 Psaumes 49.17 1 Timothée 6.7 Luc 12.20
16 Hiyo ndiyo balaa mbaya sana, ya kwamba kama vile alivyokuja, vivyo hivyo atakwenda zake; naye amefaidiwa nini mwenye kujitaabisha kwa ajili ya upepo?
Proverbes 11.29 Ecclésiaste 1.3 Marc 8.36 Ecclésiaste 5.13 1 Samuel 12.21
17 Siku zake zote hula gizani, mwenye fadhaa nyingi, mwenye ugonjwa na uchungu.
Psaumes 127.2 Psaumes 102.9 2 Rois 5.27 Actes 12.23 Psaumes 90.7-90.11
18 Tazama, mimi niliyoyaona kuwa ndiyo mema na ya kufaa, ni mtu kula na kunywa, na kujiburudisha kwa mema katika kazi yake yote anayoifanya chini ya jua, siku zote za maisha yake alizopewa na Mungu; maana hilo ndilo fungu lake.
Ecclésiaste 2.24 Ecclésiaste 2.10 Ecclésiaste 3.22 Ecclésiaste 8.15 Ecclésiaste 3.12-3.13
19 Tena, kwa habari za kila mwanadamu, ambaye Mungu amempa mali na ukwasi, akamwezesha kula katika hizo, na kuipokea sehemu yake, na kuifurahia amali yake; hiyo ndiyo karama ya Mungu.
Ecclésiaste 6.2 Ecclésiaste 3.13 1 Rois 3.13 Deutéronome 8.18 2 Chroniques 1.12
20 Kwa kuwa mtu hatazikumbuka mno siku za maisha yake; kwa sababu Mungu humtakabali katika furaha ya moyo wake.
Esaïe 65.21-65.24 Esaïe 65.13-65.14 Deutéronome 28.47 Deutéronome 28.8-28.12 Psaumes 37.16

Cette Bible est dans le domaine public.