Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 40.7
Bible en Swahili de l’est


Louange à Dieu pour son intervention

1 Nalimngoja Bwana kwa saburi, Akaniinamia akakisikia kilio changu.
Psaumes 37.7 Psaumes 27.13-27.14 Jacques 5.7-5.11 Daniel 9.18 Psaumes 130.2
2 Akanipandisha toka shimo la uharibifu, Toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, Akaziimarisha hatua zangu.
Psaumes 27.5 Psaumes 69.2 Psaumes 37.23 Actes 2.27-2.31 Matthieu 13.50
3 Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumaini Bwana
Psaumes 33.3 Psaumes 52.6 Apocalypse 14.3 Actes 2.31-2.41 Apocalypse 5.9-5.10
4 Heri aliyemfanya Bwana kuwa tumaini lake, Wala hakuwaelekea wenye kiburi, Wala hao wanaogeukia uongo.
Psaumes 125.5 Psaumes 34.8 Psaumes 118.8-118.9 Psaumes 2.12 Psaumes 84.11-84.12
5 Ee Bwana, Mungu wangu, umefanya kwa wingi Miujiza yako na mawazo yako kwetu; Hakuna awezaye kufananishwa nawe; Kama ningependa kuyatangaza na kuyahubiri, Ni mengi sana hayahesabiki.
Psaumes 139.17-139.18 Psaumes 71.15 Psaumes 136.4 Jérémie 29.11 Exode 15.11
6 Dhabihu na matoleo hukupendezwa nazo, Masikio yangu umeyazibua, Kafara na sadaka za dhambi hukuzitaka.
Psaumes 51.16 1 Samuel 15.22 Hébreux 10.5-10.12 Esaïe 1.11 Job 33.16
7 Ndipo niliposema, Tazama nimekuja, (Katika gombo la chuo nimeandikiwa,)
Hébreux 10.7-10.9 Luc 24.44 Jean 5.39 Luc 24.27 1 Corinthiens 15.3-15.4
8 Kuyafanya mapenzi yako, Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu; Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
Jean 4.34 Jérémie 31.33 Psaumes 119.47 Romains 7.22 Jérémie 15.16
9 Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa. Sikuizuia midomo yangu; Ee Bwana, unajua.
Psaumes 22.25 Psaumes 119.13 Psaumes 22.22 Luc 4.16-4.22 Josué 22.22
10 Sikusitiri haki yako moyoni mwangu; Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sikuficha fadhili zako wala kweli yako Katika kusanyiko kubwa.
Romains 1.16-1.17 1 Thessaloniciens 1.8 Romains 10.3 Apocalypse 22.17 Romains 15.8-15.9
11 Nawe, Bwana, usinizuilie rehema zako, Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima.
Psaumes 43.3 Psaumes 57.3 Psaumes 61.7 Proverbes 20.28 Psaumes 23.6
12 Kwa maana mabaya yasiyohesabika Yamenizunguka mimi. Maovu yangu yamenipata, Wala siwezi kuona. Yamezidi kuliko nywele za kichwa changu, Na moyo wangu umeniacha.
Psaumes 38.4 Psaumes 73.26 Psaumes 69.4 Psaumes 116.3 Psaumes 19.12
13 Ee Bwana, uwe radhi kuniokoa, Ee Bwana, unisaidie hima.
Psaumes 38.22 Psaumes 70.1-70.5 Matthieu 26.36-26.44 Psaumes 25.17-25.18 Psaumes 22.19
14 Waaibike, wafedheheke pamoja, Wanaoitafuta nafsi yangu waiangamize. Warudishwe nyuma, watahayarishwe, Wapendezwao na shari yangu.
Psaumes 35.4 Psaumes 71.13 Psaumes 35.26 Esaïe 41.11 Matthieu 21.38-21.41
15 Wakae hali ya ukiwa, na iwe aibu yao, Wanaoniambia, Ewe! Ewe!
Psaumes 35.21 Psaumes 35.25 Psaumes 69.24-69.25 Psaumes 73.19 Luc 19.43-19.44
16 Washangilie, wakufurahie, Wote wakutafutao. Waupendao wokovu wako Waseme daima, Atukuzwe Bwana.
Psaumes 35.27 Psaumes 22.26 Esaïe 65.13-65.14 Actes 19.17 Psaumes 119.81
17 Nami ni maskini na mhitaji, Bwana atanitunza. Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu, Ee Mungu wangu, usikawie.
Esaïe 41.17 Psaumes 70.5 Psaumes 34.6 1 Pierre 5.7 Hébreux 13.6

Cette Bible est dans le domaine public.