Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 16.9
Bible en Swahili de l’est


Récompense et certitude du juste

1 Mungu, unihifadhi mimi, Kwa maana nakukimbilia Wewe.
Psaumes 56.1 Psaumes 17.8 Psaumes 31.23 2 Timothée 1.12 Esaïe 26.3-26.4
2 Nimemwambia Bwana, Ndiwe Bwana wangu; Sina wema ila utokao kwako.
Psaumes 31.14 Psaumes 91.2 Psaumes 73.25 Zacharie 13.9 Psaumes 50.9-50.10
3 Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao.
Malachie 3.17 Tite 3.8 Hébreux 6.10 Psaumes 119.63 Ephésiens 1.1
4 Huzuni zao zitaongezeka Wambadilio Mungu kwa mwingine; Sitazimimina sadaka zao za damu, Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.
Exode 23.13 Psaumes 32.10 Josué 23.7 Jonas 2.8 Psaumes 97.7
5 Bwana ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unaishika kura yangu.
Lamentations 3.24 Psaumes 73.26 Psaumes 23.5 Psaumes 142.5 Psaumes 119.57
6 Kamba zangu zimeniangukia mahali pema, Naam, nimepata urithi mzuri.
Jérémie 3.19 Psaumes 78.55 Ephésiens 1.18 Philippiens 2.9-2.11 Apocalypse 3.21
7 Nitamhimidi Bwana aliyenipa shauri, Naam, mtima wangu umenifundisha usiku.
Psaumes 77.6 Psaumes 42.8 Psaumes 73.24 Psaumes 17.3 Esaïe 50.4
8 Nimemweka Bwana mbele yangu daima, Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa.
Psaumes 73.23 Actes 2.25-2.28 Psaumes 110.5 Psaumes 121.5 Psaumes 109.31
9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahi, Nao utukufu wangu unashangilia, Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.
Psaumes 30.12 Psaumes 57.8 Job 19.26-19.27 1 Thessaloniciens 4.13-4.14 Esaïe 26.19
10 Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.
Psaumes 49.15 Actes 13.35-13.38 Apocalypse 20.13 Actes 2.27-2.31 Apocalypse 1.18
11 Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako ziko furaha tele; Na katika mkono wako wa kuume Mna mema ya milele.
Actes 2.28 Apocalypse 7.15-7.17 Psaumes 21.4-21.6 Psaumes 36.7-36.8 Matthieu 7.14

Cette Bible est dans le domaine public.