Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esther 2.7
Bible en Swahili de l’est


Choix d’Esther comme reine

1 Baada ya hayo, hasira yake mfalme Ahasuero ilipotulia, alimkumbuka Vashti, na vile alivyotenda, na yale yaliyoamriwa juu yake.
Esther 7.10 Esther 1.12-1.21 Daniel 6.14-6.18
2 Basi watumishi wa mfalme waliomhudumu walimwambia, Mfalme na atafutiwe mabikira vijana wazuri;
1 Rois 1.2 Esther 6.14 Esther 1.14 Esther 1.10 Genèse 12.14
3 naye mfalme aweke wasimamizi katika majimbo yote ya ufalme wake, ili wakusanye pamoja mabikira vijana wazuri wote waende Shushani ngomeni, kwenye nyumba ya wanawake mikononi mwa Hegai, msimamizi-wa-nyumba wa mfalme, mwenye kuwalinda wanawake; tena wapewe vifaa vya utakaso.
Esther 1.1-1.2 Esther 2.12-2.15 Esther 2.8-2.9 Esaïe 3.18-3.23
4 Naye yule msichana atakayempendeza mfalme na awe malkia badala ya Vashti. Neno hilo likampendeza mfalme, naye akafanya hivyo.
2 Samuel 16.21-16.23 Matthieu 14.6 2 Samuel 13.4-13.6 2 Samuel 17.4 Esther 3.9-3.10
5 Basi palikuwa na Myahudi mmoja huko Shushani ngomeni; jina lake Mordekai, bin Yairi, bin Shimei, bin Kishi, wa kabila ya Benyamini;
1 Samuel 9.1 2 Samuel 16.5 Esther 5.1 Esther 2.3 Esther 1.2
6 ambaye kwamba amechukuliwa mateka kutoka Yerusalemu miongoni mwa wafungwa waliochukuliwa pamoja na Yekonia, mfalme wa Yuda; ambaye Nebukadreza, mfalme wa Babeli,alimchukua.
2 Rois 24.14-24.15 2 Chroniques 36.20 2 Rois 24.6 Jérémie 24.1 Jérémie 22.24
7 Naye alikuwa amemlea Hadasa, yaani, Esta, binti wa mjomba wake, kwa kuwa hana baba wala mama. Naye msichana huyu alikuwa wa umbo mzuri na uso mwema; nao walipokufa baba yake na mama yake, yule Mordekai alimtwaa kuwa binti yake yeye.
Esther 2.15 Ephésiens 6.4 Daniel 1.6-1.7 Esther 1.11 Genèse 48.5
8 Basi ikawa, wakati iliposikiwa amri ya mfalme na mbiu yake, wasichana wengi wakakusanyika huko Shushani ngomeni mikononi mwa Hegai; Esta naye aliingizwa katika nyumba ya mfalme, mikononi mwa Hegai mwenye kuwalinda wanawake.
Esther 2.3 Esther 2.15
9 Yule mwanamwali akampendeza, akapokea fadhili kwake; naye akampa upesi vifaa vya utakaso, pamoja na posho zake, na vijakazi saba walio haki yake, wa nyumbani mwa mfalme. Pia akamhamisha yeye na vijakazi wake akawaweka mahali pazuri katika nyumba ya wanawake.
Esther 2.12 Esther 2.3 Genèse 39.21 Daniel 1.9 Néhémie 2.8
10 Walakini Esta hakudhihirisha kabila yake wala jamaa yake, kwa maana ndivyo alivyomwagiza Mordekai asiwadhihirishe.
Esther 2.20 Matthieu 10.16 Esther 3.8 Esther 2.7 Esther 7.4
11 Na yule Mordekai akawa akitembea kila siku mbele ya ua wa nyumba ya wanawake, ili ajue hali yake Esta, na hayo yatakayompata.
1 Samuel 17.18 Actes 15.36 Genèse 37.14 Esther 2.13-2.14
12 Basi ilipowadia zamu yake mwanamwali mmojawapo aingie kwa mfalme Ahasuero, hali akiisha kufanyiwa sawasawa na sheria ya wanawake miezi kumi na miwili; yaani, ndivyo zilivyotimia siku zao za utakaso, miezi sita kwa mafuta ya manemane, na miezi sita kwa manukato na vifaa vya utakaso wa wanawake;
Cantique 3.6 Esaïe 57.9 Proverbes 7.17 Luc 7.37-7.38 1 Thessaloniciens 4.4-4.5
13 mwanamwali huingia hivyo kwa mfalme; kila akitakacho hupewa kwenda nacho kutoka katika nyumba ya wanawake ili kuingia katika nyumba ya mfalme.
14 Huenda jioni, na asubuhi hurudi nyumba ya pili ya wanawake, mikononi mwa Shaashgazi, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda masuria. Wala haingii tena kwa mfalme, isipokuwa amempendeza mfalme, naye akaitwa kwa jina.
Esther 4.11 Esaïe 43.1 Genèse 34.19 Esaïe 62.4-62.5 Esaïe 45.4
15 Hata ilipowadia zamu yake Esta, binti Abihaili, mjomba wake Mordekai, ambaye alimtwaa kuwa binti yake, ili aingie kwa mfalme, yeye hakutaka kitu, ila vile vilivyoagizwa na Hegai, msimamizi wake mfalme, mwenye kuwalinda wanawake. Naye huyu Esta alikuwa amepata kibali machoni pa wote waliomwona.
Esther 9.29 Actes 7.10 Esther 2.7-2.8 Cantique 8.10 Esther 2.3
16 Basi Esta alipelekwa kwa mfalme Ahasuero, katika nyumba ya kifalme, mwezi wa kumi, ndio mwezi wa Tebethi, mwaka wa saba wa kumiliki kwake.
Esther 8.9 Esther 2.3 Esdras 7.8 Esther 2.1
17 Mfalme akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamtia taji ya kifalme kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti.
Psaumes 113.7-113.8 1 Samuel 2.8 Ezéchiel 17.24 Luc 1.48-1.52 Esther 1.11
18 Ndipo mfalme alipowafanyia karamu kubwa maakida wake wote na watumishi wake, yaani, karamu yake Esta; akafanya msamaha katika majimbo yote, akatoa zawadi sawasawa na ukarimu wa mfalme.
Néhémie 8.11 Esther 1.3-1.5 Luc 14.8 Esther 9.22 Juges 14.10-14.17

Échec d’un complot grâce à Mardochée

19 Basi mabikira walipokusanyika mara ya pili, Mordekai alikuwa akiketi mlangoni pa mfalme.
Esther 2.21 Esther 2.3-2.4 Esther 5.13 Esther 3.2-3.3
20 Esta alikuwa hajadhihirisha jamaa yake wala kabila yake, kama vile Mordekai alivyomwagiza; kwa maana Esta alikuwa akiyashika maagizo ya Mordekai, vile vile kama wakati alipolelewa naye.
Esther 2.10 Ephésiens 6.1-6.3 Esther 2.7
21 Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero.
Esther 6.2 2 Samuel 16.11 1 Rois 16.9 2 Rois 12.20 2 Rois 9.22-9.24
22 Basi Mordekai akapata kulijua jambo hilo, naye akamjulisha Esta, malkia; naye Esta akamwambia mfalme habari hiyo kwa jina la Mordekai.
Esther 6.1-6.2 Romains 11.33 Actes 23.12-23.22 Philippiens 2.4 Ecclésiaste 10.20
23 Na jambo hilo lilipochunguzwa, na hakika ikapatikana, hao wote wawili wakatundikwa juu ya mti. Hayo pia yakaandikwa katika kitabu cha taarifa mbele ya mfalme.
Esther 10.2 Genèse 40.19 Genèse 40.22 Deutéronome 21.22-21.23 Esther 7.10

Cette Bible est dans le domaine public.