Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Chroniques 21.2
Bible en Swahili de l’est


Règne de Joram

1 Yehoshafati akalala na babaze, akazikwa pamoja na babaze katika mji wa Daudi; akatawala Yehoramu mwanawe mahali pake.
1 Rois 22.50 2 Chroniques 9.31 2 Chroniques 21.20 2 Chroniques 12.16 2 Rois 8.16-8.17
2 Naye alikuwa na ndugu, wana wa Yehoshafati, Azaria, na Yehieli, na Zekaria, na Azaria, na Mikaeli, na Shefatia; hao wote walikuwa wana wa Yehoshafati mfalme wa Israeli.
2 Chroniques 23.2 2 Chroniques 12.6 2 Chroniques 24.5 2 Chroniques 28.19 2 Chroniques 28.27
3 Baba yao akawapa zawadi kubwa, za fedha, na za dhahabu, na za tunu, pamoja na miji yenye maboma katika Yuda; lakini ufalme akampa Yehoramu, kwa sababu alikuwa mzaliwa wa kwanza.
2 Chroniques 11.23 2 Chroniques 11.5 Deutéronome 21.15-21.17 Genèse 25.6
4 Basi Yehoramu alipoinuliwa juu ya ufalme wa babaye, na kujitia nguvu, akawaua nduguze wote kwa upanga, na baadhi ya wakuu wa Israeli pia.
Juges 9.5 2 Chroniques 22.10 2 Chroniques 21.17 Genèse 4.8 2 Chroniques 22.8
5 Yehoramu alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, akatawala miaka minane huko Yerusalemu.
2 Rois 8.17-8.22
6 Akaiendea njia ya wafalme wa Israeli, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; kwa kuwa alikuwa amemwoa binti Ahabu; akafanya maovu machoni pa Bwana.
2 Chroniques 18.1 2 Rois 8.18 1 Rois 12.28-12.30 1 Rois 16.25-16.33 Néhémie 13.25-13.26
7 Walakini Bwana hakupenda kuiharibu nyumba ya Daudi, kwa sababu ya agano alilolifanya na Daudi, na kama alivyomwahidi kuwa atampa taa, yeye na wazao wake siku zote.
1 Rois 11.36 1 Rois 11.13 2 Samuel 7.12-7.17 Psaumes 132.11 2 Samuel 23.5
8 Zamani zake Edomu wakaasi chini ya mkono wa Yuda, wakajifanyia mfalme.
Genèse 27.40 2 Chroniques 21.10 2 Rois 8.20-8.22 1 Rois 22.47 2 Rois 3.9
9 Ndipo akavuka Yehoramu na maakida wake, na magari yake yote pamoja naye; akaondoka usiku, akawapiga Waedomi waliomzunguka yeye na hao maakida wa magari.
10 Hivyo Edomu wakaasi chini ya mkono wa Yuda, hata leo; wakaasi na Libna zamani zizo hizo chini ya mkono wake: kwa sababu alikuwa amemwacha Bwana, Mungu wa baba zake.
2 Chroniques 13.10 Deutéronome 32.21 2 Rois 19.8 2 Chroniques 15.2 Josué 21.13
11 Tena ndiye aliyefanya mahali pa juu milimani pa Yuda, na kuwaendesha katika uasherati wenyeji wa Yerusalemu, na kuwakosesha Yuda.
Lévitique 20.5 Lévitique 17.7 1 Rois 11.7 Daniel 3.5-3.6 Psaumes 106.39
12 Likamjia andiko kutoka kwa Eliya nabii, kusema, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako, asema hivi, Kwa sababu hukuziendea njia za Yehoshafati baba yako, wala njia za Asa mfalme wa Yuda;
2 Chroniques 14.2-14.5 2 Chroniques 17.3-17.4 Jérémie 36.23 1 Rois 22.43 Daniel 5.5
13 lakini umeiendea njia ya wafalme wa Israeli, ukawaendesha katika uasherati Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, kama walivyofanya nyumba ya Ahabu; tena umewaua ndugu zako wa nyumba ya baba yako, waliokuwa wema kuliko wewe;
2 Chroniques 21.4 2 Chroniques 21.11 2 Chroniques 21.6 1 Rois 16.30-16.33 1 Rois 16.25
14 tazama, Bwana atawapiga pigo kubwa watu wako, na watoto wako, na wake zako, na mali yako yote;
Michée 6.16 Exode 20.5 Lévitique 26.21 Osée 5.11
15 nawe utakuwa na ugonjwa mkuu kwa maradhi ya matumbo, yatakapotokea matumbo yako kwa sababu ya ugonjwa huo siku kwa siku.
2 Chroniques 21.18-21.19 Actes 1.18 Deutéronome 28.67 Deutéronome 28.59 Deutéronome 28.27
16 Bwana akawaamsha roho Wafilisti, na Waarabu waliowaelekea Wakushi juu ya Yehoramu,
2 Chroniques 17.11 2 Chroniques 33.11 1 Rois 11.23 1 Rois 11.14 2 Chroniques 22.1
17 nao wakakwea juu ya nchi ya Yuda, wakaipenya, wakaichukua mali yote iliyoonekama nyumbani mwa mfalme, na wanawe pia, na wakeze; asisaziwe mwana hata mmoja, ila Ahazia, aliyekuwa mdogo miongoni mwa wanawe.
2 Chroniques 22.1 2 Chroniques 22.6 2 Chroniques 25.23 Job 5.3-5.4 2 Chroniques 24.7
18 Na baada ya hayo yote Bwana akampiga matumbo kwa ugonjwa usioponyeka.
2 Chroniques 21.15 2 Rois 9.29 Actes 12.23
19 Ikawa baada ya siku, ikiisha miaka miwili, matumbo yake yakatokea kwa sababu ya ugonjwa wake, akafa akiugua vibaya. Wala watu wake hawakumfukizia mafukizo kama ya baba zake.
2 Chroniques 16.14 Jérémie 34.5
20 Alikuwa na umri wa miaka thelathini na miwili alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu miaka minane; akafariki bila kutamaniwa; wakamzika mjini mwa Daudi, ila si katika makaburi ya wafalme.
Jérémie 22.18 Jérémie 22.28 2 Chroniques 24.25 2 Chroniques 28.27 Proverbes 10.7

Cette Bible est dans le domaine public.