Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 7.8
Bible en Swahili de l’est


Une maison pour Dieu et pour David

1 Ikawa, mfalme alipokuwa akikaa katika nyumba yake, hapo Bwana alipomstarehesha, asiudhiwe na adui zake waliomzunguka pande zote,
Daniel 4.29-4.30 Psaumes 18.1 2 Chroniques 14.6 1 Chroniques 17.1-17.27 Josué 21.44
2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.
2 Samuel 5.11 2 Samuel 12.1 Aggée 1.4 Exode 26.1-26.14 Jean 2.17
3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe.
1 Rois 8.17-8.18 1 Chroniques 22.7 1 Chroniques 28.2 1 Samuel 16.7 Psaumes 20.4
4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,
Nombres 12.6 1 Chroniques 17.3 Amos 3.7
5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?
1 Chroniques 17.4 1 Chroniques 22.7-22.8 1 Rois 5.3-5.4 1 Chroniques 23.3-23.32 1 Rois 8.16-8.19
6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.
1 Rois 8.16 Exode 40.18-40.19 Josué 18.1 Actes 7.44 1 Chroniques 17.5-17.6
7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi?
2 Samuel 5.2 Lévitique 26.11-26.12 1 Chroniques 17.6 Jean 21.15-21.17 Deutéronome 23.14
8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli;
2 Samuel 6.21 1 Samuel 16.11-16.12 Psaumes 78.70-78.71 1 Samuel 10.1 1 Samuel 9.16
9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina kuu, kama jina la wakuu walioko duniani.
1 Chroniques 17.8 2 Samuel 5.10 Psaumes 18.37-18.42 Psaumes 113.7-113.8 2 Samuel 8.14
10 Tena nitawaagizia mahali watu wangu Israeli, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena, kama hapo kwanza;
Amos 9.15 Jérémie 24.6 Psaumes 80.8 Exode 15.17 Ezéchiel 37.25-37.27
11 naam, kama vilivyokuwa tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi, wawe juu ya watu wangu Israeli; nami nitakustarehesha mbele ya adui zako wote. Tena Bwana anakuambia ya kwamba Bwana atakujengea nyumba.
2 Samuel 7.27 2 Samuel 7.1 1 Samuel 12.9-12.11 Juges 2.14-2.16 1 Chroniques 17.10
12 Nawe siku zako zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake.
1 Rois 2.1 1 Rois 8.20 Actes 13.36 Deutéronome 31.16 1 Chroniques 17.11
13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa jina langu, nacho kiti cha enzi cha ufalme wake nitakifanya imara milele.
Esaïe 9.7 1 Rois 8.19 1 Rois 6.12 1 Rois 5.5 Psaumes 89.4
14 Mimi nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu; akitenda maovu nitamwadhibu kwa fimbo ya binadamu na kwa mapigo ya wanadamu;
Hébreux 1.5 Apocalypse 3.19 Jérémie 30.11 Deutéronome 8.5 1 Corinthiens 11.32
15 lakini fadhili zangu hazitamwondoka, kama vile nilivyomwondolea Sauli, niliyemwondoa mbele yako.
1 Samuel 15.23 1 Samuel 15.28 1 Samuel 16.14 1 Rois 11.13 2 Samuel 7.14
16 Na nyumba yako, na ufalme wako, vitathibitishwa milele mbele yako. Nacho kiti chako kitafanywa imara milele.
2 Samuel 7.13 Psaumes 89.36-89.37 Psaumes 45.6 Daniel 2.44 Esaïe 9.7
17 Kwa maneno hayo yote, na kwa maono hayo yote, ndivyo Nathani alivyonena na Daudi.
Actes 20.20 1 Chroniques 17.15 Actes 20.27 1 Corinthiens 15.3
18 Ndipo Daudi, mfalme, akaingia, akaketi mbele za Bwana, akasema, Mimi ni nani, Bwana MUNGU, na nyumba yangu ni nini, hata umenileta hata hapa?
Psaumes 8.4 1 Chroniques 17.16 1 Samuel 18.18 Exode 3.11 Genèse 32.10
19 Tena jambo hili lilikuwa dogo machoni pako, Ee Bwana MUNGU; hata umeleta habari ya nyumba yangu mimi, mtumwa wako, kwa miaka mingi inayokuja baadaye; na hayo kwa namna ya kibinadamu, Ee Bwana MUNGU.
Esaïe 55.8-55.9 1 Chroniques 17.17 Psaumes 36.7 2 Samuel 7.11-7.16 Ephésiens 3.19-3.20
20 Na mimi, Daudi, nikuambie nini tena zaidi? Iwapo wewe umemjua mtumwa wako, Ee Bwana MUNGU.
1 Samuel 16.7 Jean 21.17 Psaumes 139.1 Jean 2.25 Apocalypse 2.23
21 Kwa ajili ya neno lako, na kwa moyo wako mwenyewe, umetenda makuu hayo yote, ili umjulishe mtumwa wako.
Josué 23.14-23.15 Luc 12.32 Ephésiens 1.9 Luc 10.21 Ephésiens 3.11
22 Kwa hiyo, wewe ndiwe mkuu, Ee Bwana Mungu, kwa maana hakuna kama wewe, wala hapana Mungu mwingine ila wewe, kwa kadiri tulivyosikia kwa masikio yetu.
Exode 15.11 Deutéronome 3.24 Psaumes 86.8 1 Chroniques 16.25 Psaumes 86.10
23 Tena ni taifa lipi duniani lililo kama watu wako, kama Israeli, ambalo Mungu alikwenda kuwakomboa kwa ajili yake, wawe watu wake mwenyewe, akajifanyie jina, na kutenda mambo makuu kwa ajili yenu, na mambo ya kuogofya kwa ajili ya nchi yako, mbele ya watu wako, uliowakomboa kutoka Misri wawe wako, kutoka katika mataifa na miungu yao.
Deutéronome 10.21 Deutéronome 9.26 Psaumes 147.20 Psaumes 111.9 Deutéronome 33.29
24 Nawe ulijifanyia imara watu wako Israeli, wawe watu wako milele; nawe, Bwana, umekuwa Mungu wao.
Deutéronome 26.18 Psaumes 48.14 Genèse 17.7 Jérémie 32.38 Exode 15.2
25 Basi sasa, Ee Bwana Mungu, neno lile ulilolinena katika habari za mtumwa wako, na katika habari za nyumba yangu, ulifanye imara milele, ukatende kama ulivyosema.
Jérémie 11.4-11.5 Genèse 32.12 Psaumes 119.49 Ezéchiel 36.37
26 Jina lako na litukuzwe milele, kusema, Bwana wa majeshi ndiye Mungu juu ya Israeli; na nyumba ya mtumwa wako, Daudi, itakuwa imara mbele zako.
1 Chroniques 17.23-17.24 Matthieu 6.9 Psaumes 72.18-72.19 1 Chroniques 29.10-29.13 Psaumes 89.36
27 Kwa kuwa wewe, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli umenifunulia mimi, mtumwa wako, ukisema, Nitakujengea nyumba; kwa hiyo mimi, mtumwa wako, nimeona vema moyoni mwangu nikuombe dua hii.
Psaumes 10.17 1 Chroniques 17.25-17.26 Ruth 4.4 Psaumes 40.6 1 Samuel 9.15
28 Na sasa, Ee Bwana MUNGU, wewe ndiwe Mungu, na maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidia mtumwa wako jambo hili jema
Jean 17.17 Tite 1.2 Nombres 23.19 Exode 34.6
29 basi, sasa, uwe radhi, ukaibarikie nyumba ya mtumwa wako, ipate kudumu milele mbele zako; kwa maana wewe, Ee Bwana MUNGU, umelinena na kwa baraka yako nyumba ya mtumwa wako na ibarikiwe milele.
Nombres 6.24-6.26 2 Samuel 22.51 1 Chroniques 17.27 Psaumes 115.12-115.15

Cette Bible est dans le domaine public.