Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 99.5

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 99

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 98 Chapitre 100

Dieu, le Roi juste et saint

1 Bwana ametamalaki, mataifa wanatetemeka; Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.
2 Bwana katika Sayuni ni mkuu, Naye ametukuka juu ya mataifa yote.
3 Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa; Ndiye mtakatifu.
4 Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu; Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili; Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.
5 Mtukuzeni Bwana, Mungu wetu; Sujuduni penye kiti cha miguu yake; Ndiye mtakatifu.
6 Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake, Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake, Walipomwita Bwana aliwaitikia;
7 Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao. Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.
8 Ee Bwana, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu; Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe Ingawa uliwapatiliza matendo yao.
9 Mtukuzeni Bwana, Mungu wetu; Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu; Maana Bwana, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 99.5 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.