Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 75.1

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 75

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 74 Chapitre 76

Dieu, le juge souverain

1 Ee Mungu, twakushukuru. Twakushukuru kwa kuwa Jina lako li karibu; Watu huyasimulia matendo yako ya ajabu.
2 Nitakapoufikia wakati ulioamriwa, Mimi nitahukumu hukumu za haki.
3 Ingawa dunia na wote wakaao humo wataharuki, Mimi mwenyewe nimezisimamisha nguzo zake.
4 Naliwaambia waliojivuna, Msijivune; Na wasio haki, Msiiinue pembe.
5 Msiiinue pembe yenu juu, Wala msinene kwa shingo ya kiburi.
6 Maana siko mashariki wala magharibi, Wala nyikani itokako heshima.
7 Bali Mungu ndiye ahukumuye; Humdhili huyu na kumwinua huyu.
8 Maana mkononi mwa Bwana mna kikombe, Na mvinyo yake inatoka povu; Kumejaa machanganyiko; Naye huyamimina. Na sira zake wasio haki wa dunia Watazifyonza na kuzinywa.
9 Bali mimi nitatangaza matendo yako milele, Nitamwimbia Mungu wa Yakobo.
10 Pembe zote za wasio haki nitazikata, Na pembe za mwenye haki zitainuka.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 75.1 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.