Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 41.9

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 41

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 40 Chapitre 42

Prière d’un homme trahi par son ami

1 Heri amkumbukaye mnyonge; Bwana atamwokoa siku ya taabu.
2 Bwana atamlinda na kumhifadhi hai, Naye atafanikiwa katika nchi; Wala usimtie katika hali wamtakiayo adui zake.
3 Bwana atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani. Katika ugonjwa wake umemtandikia.
4 Nami nalisema, Bwana, unifadhili, Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.
5 Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya, Atakufa lini, jina lake likapotea?
6 Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo, Moyo wake hujikusanyia maovu, Naye atokapo nje huyanena.
7 Wote wanaonichukia wananinong’ona, Wananiwazia mabaya.
8 Neno la kisirani limemgandama, Na iwapo amelala hatasimama tena.
9 Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake.
10 Lakini Wewe, Bwana, unifadhili, Uniinue nipate kuwalipa.
11 Kwa neno hili nimejua ya kuwa wapendezwa nami, Kwa kuwa adui yangu hasimangi kwa kunishinda.
12 Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza, Umeniweka mbele za uso wako milele.
13 Na atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Tangu milele hata milele. Amina na Amina.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 41.9 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.