Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 76

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 76

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 75 Chapitre 77

Victoire de la puissance de Dieu

1 Katika Yuda Mungu amejulikana, Katika Israeli jina lake ni kuu.
2 Kibanda chake pia kiko Salemu, Na maskani yake iko Sayuni.
3 Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta, Ngao, na upanga, na zana za vita.
4 Wewe U mwenye fahari na adhama, Toka milima ya mateka.
5 Wametekwa wenye moyo thabiti; Wamelala usingizi; Wala hawakuiona mikono yao Watu wote walio hodari.
6 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.
7 Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe; Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira?
8 Toka mbinguni ulitangaza hukumu; Nchi iliogopa, ikakaa kimya.
9 Mungu aliposimama ili kuhukumu Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.
10 Maana hasira ya binadamu itakusifu, Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.
11 Wekeni nadhiri, mkaziondoe Kwa Bwana, Mungu wenu. Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, Yeye astahiliye kuogopwa.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; Na kuwatisha wafalme wa dunia.


Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 76.1 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.