Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Apocalypse 3.19
Bible en Swahili de l’est


Lettre à l’Église de Sardes

1 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.
1 Timothée 5.6 Apocalypse 1.4 Apocalypse 1.16 Apocalypse 4.5 Luc 15.24
2 Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.
Actes 18.23 1 Pierre 4.7 Actes 20.28-20.31 Apocalypse 16.15 Apocalypse 2.4
3 Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako.
Apocalypse 2.5 2 Pierre 3.10 Apocalypse 16.15 1 Thessaloniciens 5.2 Matthieu 25.13
4 Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili.
Apocalypse 6.11 Apocalypse 7.9 Jude 1.23 Apocalypse 4.4 Ecclésiaste 9.8
5 Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake.
Matthieu 10.32 Apocalypse 17.8 Apocalypse 20.15 Apocalypse 21.27 Apocalypse 20.12
6 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Apocalypse 2.7

Lettre à l’Église de Philadelphie

7 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye.
Esaïe 22.22 1 Jean 5.20 Job 12.14 Matthieu 16.19 Apocalypse 3.14
8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu.
1 Corinthiens 16.9 Jean 17.6 2 Corinthiens 2.12 Luc 12.9 Actes 14.27
9 Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda.
Apocalypse 2.9 Esaïe 49.23 Esaïe 60.14 Esaïe 43.4 1 Samuel 2.36
10 Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.
Apocalypse 17.8 2 Pierre 2.9 Apocalypse 6.10 Apocalypse 2.10 Apocalypse 1.9
11 Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.
Apocalypse 2.25 Apocalypse 2.10 Apocalypse 22.20 Jacques 1.12 Apocalypse 3.3
12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya.
Apocalypse 22.4 Apocalypse 21.2 Apocalypse 14.1 Galates 2.9 1 Rois 7.21
13 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Apocalypse 2.7

Lettre à l’Église de Laodicée

14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.
Apocalypse 1.5 2 Corinthiens 1.20 Colossiens 1.15 Apocalypse 3.7 Colossiens 1.18
15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.
Romains 12.11 Luc 14.27-14.28 1 Rois 18.21 Matthieu 24.12 Jacques 1.8
16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
Apocalypse 2.5 Jérémie 14.19 Zacharie 11.8-11.9 Jérémie 15.1-15.4
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
Romains 12.3 Proverbes 13.7 Osée 12.8 Apocalypse 2.9 Zacharie 11.5
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.
Apocalypse 16.15 Esaïe 55.1 Apocalypse 19.8 Matthieu 13.44 Jacques 2.5
19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Apocalypse 2.5 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.5-12.11 Proverbes 3.11-3.12 Jérémie 31.18
20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Jean 14.21-14.23 Luc 12.36-12.37 Apocalypse 19.9 Cantique 5.2-5.4 Luc 17.8
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
Matthieu 19.28 2 Timothée 2.12 Apocalypse 2.7 Matthieu 28.18 Jean 16.33
22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Apocalypse 2.7 Apocalypse 2.11 Apocalypse 3.13 Apocalypse 3.6 Apocalypse 2.17

Cette Bible est dans le domaine public.