Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Osée 9.15
Bible en Swahili de l’est


1 Usifurahi, Israeli, kwa sababu ya furaha, kama hao mataifa; kwa kuwa umezini juu ya Mungu wako, umependa ujira katika kila sakafu ya nafaka.
Osée 10.5 Osée 4.12 Jérémie 44.17 Osée 2.12 Ezéchiel 16.47-16.48
2 Sakafu na shinikizo hazitawalisha, na divai mpya itampungukia.
Osée 2.9 Michée 6.13-6.16 Joël 1.3-1.7 Joël 1.9-1.13 Esaïe 24.7-24.12
3 Hawatakaa katika nchi ya Bwana; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula kinajisi katika Ashuru.
Ezéchiel 4.13 Osée 8.13 Lévitique 25.23 Jérémie 2.7 Osée 7.11
4 Hawatammiminia Bwana divai, wala hazitampendeza sadaka zao; mkate wao utakuwa kama chakula cha matanga kwao; wote watakaokila watatiwa unajisi; kwa maana mkate wao utakuwa kwa shauku zao; hautaingia katika nyumba ya Bwana.
Osée 8.13 Jérémie 6.20 Deutéronome 26.14 Ezéchiel 24.17 Osée 3.4
5 Mtafanya nini katika siku ya mkutano wa idi, na katika siku ya karamu ya Bwana?
Esaïe 10.3 Jérémie 5.31 Osée 2.11 Joël 1.13
6 Kwa maana, tazama, wamekwenda zao ili kukimbia uharibifu, lakini Misri itawakusanya, Nofu itawazika; vitu vyao vya fedha viwapendezavyo, magugu yatavimiliki; miiba itakuwa katika hema zao.
Osée 10.8 Esaïe 5.6 Osée 8.13 Esaïe 7.23 Osée 7.16
7 Siku za kupatilizwa zimekuja, siku za kulipa zimefika; Israeli atayajua hayo; huyo nabii ni mpumbavu, huyo mtu mwenye roho ana wazimu; kwa sababu ya wingi wa uovu wako, na kwa sababu uadui umekuwa mkubwa.
Michée 7.4 Lamentations 2.14 Ezéchiel 13.3 Ezéchiel 14.9-14.10 Jérémie 10.15
8 Efraimu alikuwa mlinzi pamoja na Mungu wangu; na huyo nabii, mtego wa mwinda ndege u katika njia zake zote; katika nyumba ya Mungu wake umo uadui.
Ezéchiel 3.17 Osée 5.1 Esaïe 62.6 2 Rois 5.27 Lamentations 2.14
9 Wamejiharibu mno, kama katika siku za Gibea; ataukumbuka uovu wao, atazilipiza dhambi zao.
Osée 10.9 Osée 8.13 Juges 19.16-20.21 Esaïe 31.6 Esaïe 24.5

Passé et avenir d’Israël

10 Mimi nalimkuta Israeli kama zabibu nyikani; nami naliwaona baba zenu kama matunda ya mtini yaliyoiva kwanza, wakati wake wa kwanza; lakini walikwenda Baal-Peori, wakajiweka wakfu kwa kitu cha aibu, wakawa chukizo kama kitu kile walichokipenda.
Jérémie 11.13 Osée 4.14 Psaumes 106.28-106.29 Nombres 25.1-25.18 Jérémie 2.2-2.3
11 Naye Efraimu, utukufu wake utarukia mbali kama ndege, uzazi hautakuwako, wala aliye na mimba, wala achukuaye mimba.
Osée 9.14 Deutéronome 28.18 Osée 4.7 Osée 10.5 Job 18.18-18.19
12 Wajapolea watoto wao, mimi nitawanyang’anya watoto wao, asisalie hata mtu mmoja; naam, ole wao! Nitakapoondoka na kuwaacha.
Osée 7.13 Deutéronome 31.17 1 Samuel 28.15-28.16 Osée 9.16 Deutéronome 32.25
13 Efraimu amepandwa mahali pazuri, kama nilivyoona Tiro; lakini Efraimu atamtolea mwuaji watoto wake.
Ezéchiel 26.1-26.21 Ezéchiel 27.3 Osée 10.14 Osée 13.8 2 Rois 15.16
14 Wape, Ee Bwana; utawapa kitu gani? Wape tumbo lenye kuharibu mimba na maziwa makavu.
Luc 23.29 Matthieu 24.19 Luc 21.23 Osée 9.16 Osée 9.13
15 Uovu wao wote u katika Gilgali; maana huko naliwachukia; kwa sababu ya uovu wa matendo yao nitawafukuza watoke katika nyumba yangu; sitawapenda tena; wakuu wao wote ni waasi.
Osée 4.15 Osée 12.11 Esaïe 1.23 Osée 7.2 Ezéchiel 23.18
16 Efraimu amepigwa; mzizi wao umekauka; hawatazaa matunda; naam, wajapozaa, nitaliua tunda la tumbo lipendwalo sana.
Osée 9.11-9.13 Ezéchiel 24.21 Job 18.16 Osée 8.7 Malachie 4.1
17 Mungu wangu atawatupilia mbali, kwa sababu hawakumsikiliza; nao watakuwa watu wa kutanga-tanga kati ya mataifa.
Deutéronome 28.64-28.65 Osée 7.13 Deutéronome 32.26 Psaumes 31.14 2 Chroniques 18.13

Cette Bible est dans le domaine public.