Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 52
Bible en Swahili de l’est


Promesse de rétablissement

1 Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; Jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, mji mtakatifu; Kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako Asiyetahiriwa, wala aliye najisi.
Apocalypse 21.27 Esaïe 51.17 Esaïe 35.8 Néhémie 11.1 Matthieu 4.5
2 Jikung’ute mavumbi; uondoke, Uketi, Ee Yerusalemu; Jifungulie vifungo vya shingo yako, Ee binti Sayuni uliyefungwa.
Jérémie 51.45 Esaïe 29.4 Esaïe 61.1 Esaïe 51.14 Luc 4.18
3 Maana Bwana asema hivi, Mliuzwa bure; nanyi mtakombolewa bila fedha.
Psaumes 44.12 Esaïe 45.13 1 Pierre 1.18 Jérémie 15.13 Esaïe 50.1
4 Maana Bwana MUNGU asema hivi, Watu wangu hapo kwanza walishuka Misri ili wakae huko hali ya ugeni; na Mwashuri akawaonea bila sababu.
Genèse 46.6 Psaumes 25.3 Psaumes 69.4 Esaïe 14.25 Esaïe 36.1-36.22
5 Basi sasa, nafanya nini hapa, asema Bwana, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema Bwana, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa.
Romains 2.24 Psaumes 44.12 Esaïe 22.16 Esaïe 37.28 Lamentations 2.3
6 Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu kwa hiyo watajua siku ile ya kuwa mimi ndimi ninenaye; tazama ni mimi.
Esaïe 49.23 Exode 34.5-34.7 Hébreux 6.14-6.18 Zacharie 10.9-10.12 Ezéchiel 20.44
7 Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima Miguu yake aletaye habari njema, Yeye aitangazaye amani, Aletaye habari njema ya mambo mema, Yeye autangazaye wokovu, Auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!
Esaïe 40.9 Romains 10.12-10.15 Nahum 1.15 Esaïe 24.23 Luc 2.10
8 Sauti ya walinzi wako! Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja; Maana wataona jicho kwa jicho, Jinsi Bwana arejeavyo Sayuni.
Esaïe 62.6 Actes 2.46-2.47 1 Corinthiens 13.12 Ezéchiel 3.17 Ezéchiel 33.7
9 Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja, Enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa; Kwa kuwa Bwana amewafariji watu wake, Ameukomboa Yerusalemu.
Esaïe 51.3 Psaumes 98.4 Esaïe 44.23 Esaïe 44.26 Esaïe 55.12
10 Bwana ameweka wazi mkono wake mtakatifu Machoni pa mataifa yote; Na ncha zote za dunia Zitauona wokovu wa Mungu wetu.
Esaïe 51.9 Luc 3.6 Psaumes 98.1-98.3 Actes 2.5-2.11 Actes 13.47
11 Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya Bwana.
2 Corinthiens 6.17 Esaïe 48.20 Apocalypse 18.4 Zacharie 2.6-2.7 Jérémie 50.8
12 Maana hamtatoka kwa haraka, wala hamtakwenda kwa kukimbia, kwa sababu Bwana atawatangulia; na Mungu wa Israeli atawafuata nyuma; awalinde.
Esaïe 58.8 Michée 2.13 Esaïe 45.2 Exode 12.33 Exode 14.19-14.20

La personne et l’activité du serviteur de l’Éternel

13 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.
Matthieu 28.18 Esaïe 42.1 Hébreux 1.3 Philippiens 2.7-2.11 Esaïe 53.10-53.11
14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu ye yote, na umbo lake zaidi ya wanadamu),
Esaïe 53.2-53.5 Matthieu 26.67 Psaumes 22.17 Luc 22.64 Esaïe 50.6
15 ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu.
Esaïe 49.7 Esaïe 49.23 Matthieu 28.19 Esaïe 55.5 Hébreux 12.24

Cette Bible est dans le domaine public.