Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 97.12
Bible en Swahili de l’est


Les jugements de Dieu

1 Bwana ametamalaki, nchi na ishangilie, Visiwa vingi na vifurahi.
Psaumes 96.10-96.11 Psaumes 93.1 Psaumes 99.1 Esaïe 66.19 Esaïe 49.1
2 Mawingu na giza vyamzunguka, Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
Psaumes 89.14 Exode 19.9 Romains 11.33 Proverbes 16.12 Hébreux 1.8-1.9
3 Moto hutangulia mbele zake, Nao huwateketeza watesi wake pande zote.
Psaumes 18.8 Habakuk 3.5 Psaumes 50.3 Daniel 7.10 Malachie 4.1
4 Umeme wake uliuangaza ulimwengu, Nchi ikaona ikatetemeka.
Psaumes 77.18 Psaumes 104.32 Matthieu 27.50-27.51 Matthieu 28.2-28.3 Psaumes 144.5-144.6
5 Milima iliyeyuka kama nta mbele za Bwana, Mbele za Bwana wa dunia yote.
Nahum 1.5 Josué 3.11 Juges 5.4-5.5 Zacharie 4.14 Psaumes 83.18
6 Mbingu zimetangaza haki yake, Na watu wote wameuona utukufu wake.
Psaumes 50.6 Psaumes 19.1 Esaïe 6.3 Psaumes 36.5-36.6 Psaumes 89.2
7 Na waaibishwe wote waabuduo sanamu, Wajivunao kwa vitu visivyofaa; Enyi miungu yote, msujuduni Yeye.
Hébreux 1.6 Esaïe 42.17 Jérémie 10.14 Lévitique 26.1 Exode 25.20
8 Sayuni imesikia na kufurahi, Binti za Yuda walishangilia, Kwa sababu ya hukumu zako, Ee Bwana.
Psaumes 48.11 Zacharie 9.9 Matthieu 21.4-21.9 Esaïe 51.3 Psaumes 58.10
9 Maana Wewe, Bwana, ndiwe Uliye juu, Juu sana kuliko nchi yote; Umetukuka sana juu ya miungu yote.
Psaumes 83.18 Psaumes 95.3 Exode 18.11 Psaumes 135.5 Psaumes 96.4
10 Enyi mmpendao Bwana, uchukieni uovu; Huwalinda nafsi zao watauwa wake, Na kuwaokoa na mkono wa wasio haki.
Proverbes 8.13 Romains 12.9 Psaumes 34.14 Daniel 3.28 Amos 5.15
11 Nuru imemzukia mwenye haki, Na furaha wanyofu wa moyo.
Proverbes 4.18 Job 22.28 Psaumes 112.4 Esther 8.16 Psaumes 126.5-126.6
12 Enyi wenye haki, mmfurahieni Bwana, Na kulishukuru jina lake takatifu.
Psaumes 30.4 Habakuk 3.17-3.18 Philippiens 4.4 Psaumes 32.11-33.1 Hébreux 12.10

Cette Bible est dans le domaine public.