Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 109.22
Bible en Swahili de l’est


Imprécation contre le méchant

1 Ee Mungu wa sifa zangu, usinyamaze,
Psaumes 28.1 Psaumes 83.1 Deutéronome 10.21 Jérémie 17.14 Psaumes 118.28
2 Kwa maana wamenifumbulia kinywa; Kinywa cha mtu asiye haki, cha hila, Wamesema nami kwa ulimi wa uongo.
Psaumes 52.4 2 Samuel 17.1 Psaumes 64.3-64.4 Actes 6.13 Psaumes 120.2-120.3
3 Naam, kwa maneno ya chuki wamenizunguka, Wamepigana nami bure.
Psaumes 69.4 Psaumes 35.7 Psaumes 88.17 Psaumes 35.20 Osée 11.12
4 Badala ya upendo wangu wao hunishitaki, Ijapokuwa naliwaombea.
Psaumes 38.20 Luc 23.34 Jean 10.32 Daniel 6.10 2 Samuel 15.31-15.32
5 Wamenichukuza mabaya badala ya mema, Na chuki badala ya upendo wangu.
Proverbes 17.13 Psaumes 38.20 Psaumes 55.12-55.15 Psaumes 35.7-35.12 Genèse 44.4
6 Uweke mtu mkorofi juu yake, Mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Zacharie 3.1 Matthieu 5.25 Jean 13.2 Matthieu 27.4 Jean 13.27
7 Katika kuhukumiwa ataonekana hana haki, Na sala yake itadhaniwa kuwa ni dhambi.
Proverbes 28.9 Proverbes 21.27 Proverbes 15.8 2 Samuel 15.7-15.8 Esaïe 1.15
8 Siku zake na ziwe chache, Usimamizi wake na atwae mtu mwingine.
Psaumes 55.23 Actes 1.16-1.26 Matthieu 27.5
9 Wanawe na wawe yatima, Na mkewe na awe mjane.
Exode 22.24 Jérémie 18.21 Lamentations 5.3
10 Kutanga na watange wanawe na kuomba, Watafute chakula mbali na mahame yao.
Psaumes 37.25 2 Rois 5.27 2 Samuel 3.29 Job 30.3-30.9 Job 24.8-24.12
11 Mdai na anase vitu vyote alivyo navyo, Wageni na wateke mapato ya kazi yake.
Job 5.5 Job 18.9-18.19 Juges 6.3-6.6 Job 20.18 Deutéronome 28.33-28.34
12 Asiwe na mtu wa kumfanyia fadhili, Wala mtu wa kuwahurumia yatima wake.
Luc 11.50-11.51 Esaïe 27.11 Matthieu 27.25 Jacques 2.13 Esaïe 13.18
13 Wazao wake waangamizwe, Jina lao likafutwe katika kizazi cha pili.
Proverbes 10.7 Psaumes 37.28 Job 18.19 Esaïe 14.20-14.22 Deutéronome 9.14
14 Uovu wa baba zake ukumbukwe mbele za Bwana, Na dhambi ya mamaye isifutwe.
Exode 20.5 Néhémie 4.5 Jérémie 18.23 2 Samuel 3.29 2 Rois 10.13-10.14
15 Ziwe mbele za Bwana daima, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.
Psaumes 34.16 Job 18.17 Psaumes 90.8 Jérémie 2.22 Amos 8.7
16 Kwa kuwa hakukumbuka kutenda fadhili, Bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, Hata akamfisha mtu aliyevunjika moyo,
Psaumes 34.18 Psaumes 10.14 Psaumes 69.20-69.29 Jacques 2.13 Genèse 42.21
17 Naye alipenda kulaani, nako kukampata. Hakupendezwa na kubariki, kukawa mbali naye,
Proverbes 14.14 Ezéchiel 35.6 Matthieu 7.2 Psaumes 52.4-52.5 Apocalypse 16.6
18 Alijivika laana kana kwamba ni vazi lake. Ikamwingilia moyoni kama maji, Na kama mafuta mifupani mwake.
Psaumes 73.6 Nombres 5.22 Colossiens 3.12 Nombres 5.27 Matthieu 27.3-27.5
19 Na iwe kwake kama vazi ajivikalo, Na kama mshipi ajifungao daima.
Psaumes 109.29 Psaumes 35.26 Psaumes 132.18 Psaumes 109.18
20 Ndiyo malipo ya washitaki wangu toka kwa Bwana, Na ya hao wanaoisingizia nafsi yangu mabaya.
1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Luc 19.27 Psaumes 110.1 Psaumes 94.23 2 Samuel 17.23
21 Na Wewe, MUNGU, Bwana, unitendee kwa ajili ya jina lako, Kwa kuwa fadhili zako ni njema uniokoe.
Psaumes 79.9-79.10 Psaumes 31.3 Psaumes 69.16 Psaumes 25.11 Psaumes 63.3
22 Kwa maana mimi ni mnyonge na mhitaji, Na moyo wangu umejeruhi ndani yangu.
Psaumes 40.17 Psaumes 86.1 Psaumes 102.17-102.20 Luc 22.44 Psaumes 102.4
23 Ninapita kama kivuli kianzacho kutoweka, Ninapeperushwa kama nzige.
Exode 10.19 Psaumes 102.10-102.11 Job 14.2 Exode 10.13 Ecclésiaste 8.13
24 Magoti yangu yamedhoofu kwa kufunga, Na mwili wangu umekonda kwa kukosa mafuta.
Hébreux 12.12 Psaumes 102.4-102.5 Psaumes 38.5-38.8 Job 19.20 Psaumes 22.14
25 Nami nalikuwa laumu kwao, Wanionapo hutikisa vichwa vyao.
Psaumes 22.6-22.7 Romains 15.3 Psaumes 69.19-69.20 Hébreux 13.13 Esaïe 37.22
26 Ee Bwana, Mungu wangu, unisaidie, Uniokoe sawasawa na fadhili zako.
Psaumes 119.86 Psaumes 40.12 Psaumes 69.16 Psaumes 57.1 Psaumes 69.13
27 Nao wakajue ya kuwa ndio mkono wako; Wewe, Bwana, umeyafanya hayo.
Job 37.7 Exode 8.19 Psaumes 17.13-17.14 Actes 2.32-2.36 Actes 4.16
28 Wao walaani, bali Wewe utabariki, Wameondoka wao wakaaibishwa, Bali mtumishi wako atafurahi.
Nombres 23.20 Jean 16.22 Psaumes 109.17 Hébreux 12.2 Nombres 23.23
29 Washitaki wangu watavikwa fedheha, Watajivika aibu yao kama joho.
Psaumes 35.26 Psaumes 132.18 Job 8.22 Psaumes 140.9 Psaumes 109.17-109.19
30 Nitamshukuru Bwana kwa kinywa changu, Naam, nitamsifu katikati ya mkutano.
Psaumes 35.18 Psaumes 111.1 Psaumes 22.22-22.25 Psaumes 107.32 Psaumes 138.1
31 Maana atasimama mkono wa kuume wa mhitaji Amwokoe na wanaoihukumu nafsi yake.
Psaumes 16.8 Psaumes 121.5 Psaumes 73.23 Psaumes 110.5 Exode 22.22-22.24

Cette Bible est dans le domaine public.