Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 11.14
Bible en Swahili de l’est


Intervention n° 1 de Tsophar

1 Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu, na kusema,
Job 2.11 Job 20.1
2 Je! Huu wingi wa maneno usijibiwe? Na mtu aliyejaa maneno, je! Ahesabiwe kuwa na haki?
Job 18.2 Proverbes 10.19 Psaumes 140.11 Job 16.3 Job 8.2
3 Je! Majivuno yako yawanyamazishe watu wawe kimya? Nawe hapo ufanyapo dhihaka, je! Hapana mtu atakayekutahayarisha?
Job 17.2 2 Thessaloniciens 3.14 Job 13.4 Jude 1.18 Jérémie 15.17
4 Kwa kuwa wewe wasema, Mafunzo yangu ni safi, Nami ni safi machoni pako.
Job 10.7 Job 6.10 Job 7.20 Job 6.29-6.30 Job 9.2-9.3
5 Lakini, laiti Mungu angenena, Na kuifunua midomo yake juu yako;
Job 38.1-38.2 Job 23.3-23.7 Job 42.7 Job 40.1-40.5 Job 40.8
6 Tena akuonyeshe hizo siri za hekima, Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake! Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.
Esdras 9.13 Job 28.28 Psaumes 106.43-106.46 Daniel 2.47 1 Corinthiens 2.9-2.11
7 Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu? Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?
Romains 11.33 Ecclésiaste 3.11 Job 5.9 Psaumes 145.3 Job 37.23
8 Ni juu mno kama mbingu; waweza kufanya nini wewe? Ni wenye kina kuliko kuzimuni; waweza kujua nini wewe?
Job 22.12 Esaïe 55.9 Job 35.5 Job 26.6 Amos 9.2
9 Cheo chake ni kirefu kuliko dunia, Ni kipana zaidi ya bahari.
Psaumes 139.9-139.10 Psaumes 65.5-65.8 Job 28.24-28.25
10 Yeye akipita, na kufunga watu, Na kuwaita hukumuni, ni nani basi awezaye kumzuia?
Job 9.12-9.13 Job 12.14 Apocalypse 3.7 Job 5.18 Psaumes 31.8
11 Kwani yeye awajua watu baradhuli; Huona na uovu pia, hata asipoufikiri.
Hébreux 4.13 Psaumes 10.14 Ecclésiaste 5.8 Job 22.13-22.14 Psaumes 10.11
12 Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu, Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda-mwitu.
Ecclésiaste 3.18 Job 39.5-39.8 Psaumes 73.22 Job 6.5 Job 5.13
13 Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu, Na kumnyoshea mikono yako;
Psaumes 88.9 Psaumes 78.8 1 Samuel 7.3 Psaumes 143.6 Luc 12.47
14 Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe, Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako;
Job 22.23 Jacques 4.8 Psaumes 101.2 Job 22.5 Ezéchiel 18.30-18.31
15 Hakika ndipo utakapopata kuinua uso pasipo ila; Naam, utathibitika, wala hutakuwa na hofu;
Job 22.26 Psaumes 27.1 Job 10.15 Genèse 4.5-4.6 1 Jean 3.19-3.22
16 Kwa kuwa utasahau mashaka yako; Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita;
Esaïe 65.16 Ecclésiaste 5.20 Jean 16.21 Esaïe 12.1-12.2 Job 6.15
17 Na maisha yako yatakuwa meupe kuliko adhuhuri; Lijapokuwa ni giza, litakuwa kama alfajiri.
Psaumes 37.6 Esaïe 58.8-58.10 Osée 6.3 Psaumes 92.14 Psaumes 112.4
18 Nawe utakuwa salama, kwa sababu kuna matumaini; Naam, utatafuta-tafuta kando yako, na kupumzika katika salama.
Psaumes 4.8 Proverbes 3.24-3.26 Psaumes 3.5 Lévitique 26.5-26.6 Colossiens 1.27
19 Tena utalala, wala hapana atakayekutia hofu; Naam, wengi watakutafuta uso wako.
Psaumes 45.12 Job 42.8-42.9 Apocalypse 3.9 Genèse 26.26-26.31 Esaïe 45.14
20 Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho.
Deutéronome 28.65 Job 31.16 Job 17.5 Amos 5.19-5.20 Job 34.22

Cette Bible est dans le domaine public.