Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esdras 10.13
Bible en Swahili de l’est


Renvoi des femmes étrangères

1 Basi hapo Ezra alipokuwa akiomba na kuungama, akilia, na kujiangusha kifudifudi mbele ya nyumba ya Mungu, wakamkusanyikia katika Israeli wote kusanyiko kubwa sana la wanaume, na wanawake, na watoto; maana watu hao walikuwa wakilia sana.
Daniel 9.20 Psaumes 119.136 2 Chroniques 20.9 1 Rois 8.30 1 Jean 1.8-1.10
2 Hata Shekania, mwana wa Yehieli, mmoja wa wana wa Elamu, akajibu, akamwambia Ezra, Sisi tumemkosa Mungu wetu, nasi tumeoa wanawake wageni wa watu wa nchi hizi; lakini kungaliko tumaini kwa Israeli katika jambo hili.
Néhémie 13.27 Esdras 9.2 Exode 34.12 Esdras 10.26 1 Jean 1.7-1.9
3 Haya basi! Na tufanye agano na Mungu wetu, kuachana na wake zetu, na wale waliozaliwa nao, tukilifuata shauri la bwana wangu, na shauri la hao wanaoitetemekea amri ya Mungu wetu; mambo haya na yatendeke kwa kuifuata torati.
Deutéronome 7.2-7.3 Esdras 9.4 2 Rois 11.17 Néhémie 9.38 Néhémie 8.14
4 Inuka; maana shughuli hii yakuhusu wewe; na sisi tu pamoja nawe; uwe na moyo mkuu, ukaitende.
1 Chroniques 28.10 Esaïe 35.3-35.4 Hébreux 12.12-12.13 1 Chroniques 22.16 Josué 7.10-7.26
5 Ndipo Ezra akaondoka, akawaapisha wakuu wa makuhani, na Walawi, na Israeli wote, ya kwamba watafanya kama hayo. Basi wakaapa.
Néhémie 13.25 Néhémie 5.12 Proverbes 1.5 Esdras 10.3 Proverbes 27.9
6 Kisha Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu, akaingia katika chumba cha Yehohanani, mwana wa Eliashibu; hata, alipofika huko, hakula mkate, wala hakunywa maji; kwa maana alilia kwa sababu ya kosa lile la watu wa uhamisho.
Deutéronome 9.18 Néhémie 3.1 Néhémie 12.22 Jean 4.31-4.34 Néhémie 13.5
7 Wakapiga mbiu katika Yuda yote na Yerusalemu, ya kwamba wana wote wa uhamisho wakusanyike pamoja huko Yerusalemu;
Esdras 1.1 2 Chroniques 30.5
8 na ya kwamba mtu awaye yote asiyekuja katika muda wa siku tatu, kwa shauri lile la wakuu na wazee, basi aondolewe mali zake zote, akatengwe yeye mwenyewe na mkutano wa uhamisho.
Jean 9.34 Lévitique 27.28 Jean 9.22 Esdras 7.26 Jean 16.2
9 Ndipo wanaume wote wa Yuda na Benyamini wakakusanyika katika muda wa siku tatu; ulikuwa mwezi wa kenda, siku ya ishirini ya mwezi; na watu wote wakaketi katika uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakitetemeka kwa sababu ya neno hilo, na kwa sababu ya mvua kubwa.
Esther 2.16 Jérémie 10.13 Jérémie 10.10 Esdras 7.8-7.9 1 Samuel 12.17-12.18
10 Kisha Ezra, kuhani, akasimama, akawaambia, Mmekosa, mmeoa wanawake wageni, kuiongeza hatia ya Israeli.
Nombres 32.14 Matthieu 23.32 Esdras 9.6 Josué 22.17-22.18 2 Chroniques 28.13
11 Sasa basi, ungameni mbele za Bwana, Mungu wa baba zenu, mkatende alipendalo; mkajitenge na watu wa nchi, tena na wanawake wageni.
Romains 12.2 Proverbes 28.13 Josué 7.19 Esdras 10.3 1 Corinthiens 2.12-2.14
12 Ndipo mkutano wote wakajibu, wakasema, kwa sauti kuu, Kama ulivyosema katika habari yetu, ndivyo vitupasavyo kutenda.
Esdras 10.3-10.4 Néhémie 13.23 Psaumes 78.57 Psaumes 78.37
13 Lakini watu hawa ni wengi, tena ni wakati wa mvua nyingi, nasi hatuwezi kusimama nje, tena kazi hii si kazi ya siku moja, wala ya siku mbili; maana tumekosa sana katika jambo hili.
Esdras 10.18-10.44 Matthieu 7.13-7.14
14 Basi maakida wetu na wawekwe kwa ajili ya mkutano wote, na watu wote walio katika miji yetu, waliooa wanawake wageni, na waje nyakati zilizoamriwa, tena pamoja nao na waje wazee wa kila mji, na makadhi wa miji hiyo, hata ghadhabu kali ya Mungu wetu itakapotuondokea mbali, jambo hili likamalizike.
2 Chroniques 29.10 2 Chroniques 30.8 Nombres 25.4 Esaïe 12.1 Deutéronome 13.17
15 Yonathani, mwana wa Asaheli, na Yazeya, mwana wa Tikwa, hawa peke yao ndio waliosimama kulipinga neno hilo; na Meshulamu, na Shabethai Mlawi, wakawasaidia.
Néhémie 11.16 Néhémie 12.33 Néhémie 3.6 Néhémie 10.20
16 Basi wana wa uhamisho wakafanya hivyo. Na Ezra, kuhani, akatengwa, pamoja na baadhi ya wakuu wa mbari za mababa, kwa hesabu ya mbari ya baba zao; na hao wote kwa majina yao. Wakaketi siku ya kwanza ya mwezi wa kumi, ili kulichunguza jambo hilo.
Jean 7.51 Deutéronome 13.14 Job 29.16
17 Wakamaliza mambo ya wanaume wote, waliokuwa wameoa wanawake wageni, siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza.
18 Basi, miongoni mwa makuhani walionekana wengine waliokuwa wameoa wanawake wageni; wa wana wa Yoshua, mwana wa Yosadaki, na nduguze; Maaseya, na Eliezeri, na Yaribu, na Gedalia.
Esdras 2.2 Esdras 3.2 Aggée 1.1 Zacharie 3.1 Esdras 5.2
19 Nao wakatoa ahadi ya kwamba wataachana na wake zao; na kwa kuwa walikuwa na hatia, wakatoa kondoo mume kwa hatia yao.
Lévitique 6.6 2 Rois 10.15 Lévitique 5.15-5.16 2 Chroniques 30.8 Lévitique 6.4
20 Na wa wana wa Imeri; Hanani, na Zebadia.
Esdras 2.37 1 Chroniques 24.14 Néhémie 7.40
21 Na wa wana wa Harimu; Maaseya, na Eliya, na Shemaya, na Yehieli, na Uzia.
1 Chroniques 24.8 Néhémie 7.42 Esdras 2.39
22 Na wa wana wa Pashuri; Elioenai, na Maaseya, na Ishmaeli, na Nethaneli, na Yozabadi, na Elasa.
1 Chroniques 9.12 Néhémie 7.41 Esdras 2.38
23 Na wa Walawi; Yozabadi, na Shimei, na Kelaya (ndiye Kelita), na Pethahia, na Yuda, na Eliezeri.
Néhémie 11.16 Néhémie 10.10 Esdras 8.33
24 Na wa waimbaji; Eliashibu. Na wa mabawabu; Shalumu, na Telemu, na Uri.
25 Na wa Israeli; wa wana wa Paroshi; Ramia, na Izia, na Malkiya, na Miyamini, na Eleazari, na Malkiya, na Benaya.
Esdras 2.3 Néhémie 7.8
26 Na wa wana wa Elamu; Matania, na Zekaria, na Yehieli, na Abdi, na Yeremothi, na Eliya.
Esdras 10.2 Esdras 2.7 Néhémie 7.12 Esdras 8.7 Esdras 2.31
27 Na wa wana wa Zatu; Elioenai, na Eliashibu, na Matania, na Yeremothi, na Zabadi, na Aziza.
Néhémie 7.13 Esdras 2.8
28 Na wa wana wa Bebai; Yehohanani, na Hanania, na Zakai, na Athlai.
Esdras 2.11 Néhémie 7.16 Esdras 8.11
29 Na wa wana wa Bani; Meshulamu, na Maluki, na Adaya, na Yashubu, na Sheali, na Yeremothi.
Esdras 2.10 Néhémie 7.15 Néhémie 10.4
30 Na wa wana wa Pahath-Moabu; Adna, na Kelali, na Benaya, na Maaseya, na Matania, na Besaleli, na Binui, na Manase.
Néhémie 7.11 Esdras 2.6 Esdras 8.4
31 Na wa wana wa Harimu; Eliezeri, na Ishiya, na Malkiya, na Shemaya, na Shimeoni,
Néhémie 3.11 Esdras 2.32 Néhémie 7.35
32 na Benyamini, na Maluki, na Shemaria.
33 Na wa wana wa Hashumu; Matenai, na Matata, na Zabadi, na Elifeleti, na Yeremai, na Manase, na Shimei.
Néhémie 7.22 Esdras 2.19
34 Na wa wana wa Bani; Maadai, na Amramu, na Ueli,
35 na Benaya, na Bedeya, na Keluhi,
36 na Wania, na Meremothi, na Eliashibu,
37 na Matania, na Matenai, na Yaasu.
38 Na wa wana wa Binui; Shimei,
39 na Shelemia, na Nathani, na Adaya,
40 na Maknadebai, na Shashai, na Sharai,
41 na Azareli, na Shelemia, na Shemaria,
42 na Shalumu, na Amaria, na Yusufu.
43 Na wa wana wa Nebo; Yeieli, na Matithia, na Zabadi, na Zebina, na Ido, na Yoeli, na Benaya.
Esdras 2.29 Néhémie 7.33
44 Hao wote walikuwa wameoa wanawake wageni; na wake zao wengine walikuwa wamezaa watoto.
Proverbes 5.3 Proverbes 5.20 Proverbes 2.16 Esdras 10.3

Cette Bible est dans le domaine public.