Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 1.30
Bible en Swahili de l’est


Règne de Salomon

Vieillesse de David et prétentions d’Adonija

1 Mfalme Daudi alikuwa mzee, mkongwe katika siku zake, nao wakamfunika nguo, lakini asipate moto.
Josué 23.1-23.2 Genèse 24.1 Psaumes 90.10 1 Chroniques 23.1 2 Samuel 5.4
2 Kwa hiyo watumishi wake wakamwambia, Bwana wangu mfalme na atafutiwe kijana mwanamwali; naye asimame mbele ya mfalme, amtunze; alale kifuani mwako, ili bwana wangu mfalme apate moto.
Deutéronome 10.8 2 Chroniques 29.11 Michée 7.5 1 Samuel 16.21-16.22 Genèse 16.5
3 Basi wakatafuta kijana mzuri mipakani mwote mwa Israeli, wakamwona Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.
Josué 19.18 1 Samuel 28.4 Esther 2.4 2 Rois 4.25 2 Rois 4.8
4 Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua.
Matthieu 1.25
5 Ndipo Adonia mwana wa Hagithi akatakabari, akasema, Mimi nitakuwa mfalme. Akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, na watu hamsini wapige mbio mbele yake.
2 Samuel 3.4 2 Samuel 15.1 1 Rois 1.11 Luc 14.11 1 Chroniques 3.2
6 Tena baba yake hakumchukiza wakati wo wote kwa kusema, Mbona umefanya hivi? Kisha, alikuwa mtu mzuri sana; naye alizaliwa baada ya Absalomu.
2 Samuel 3.3-3.4 1 Chroniques 3.2 Proverbes 22.15 Proverbes 29.15 Proverbes 23.13-23.14
7 Akashauriana na Yoabu, mwana wa Seruya, na Abiathari, kuhani; nao wakamsaidia Adonia, wakamfuata.
2 Samuel 20.25 1 Rois 2.22 2 Samuel 8.16 Psaumes 2.2 2 Samuel 15.24-15.29
8 Ila Sadoki, kuhani, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Nathani, nabii, na Shimei, na Rei, na mashujaa wa Daudi, hao hawakuwa pamoja na Adonia.
1 Rois 4.18 2 Samuel 20.25 2 Samuel 23.8-23.39 Zacharie 12.13 1 Chroniques 11.10-11.47
9 Adonia akachinja kondoo, na ng’ombe, na vinono, karibu na jiwe la Zohelethi, lililo karibu na chemchemi Rogeli; akawaita ndugu zake wote, wana wa mfalme, na watu wote wa Yuda, watumishi wa mfalme;
2 Samuel 17.17 2 Samuel 13.23-13.27 Proverbes 15.8 2 Samuel 15.11-15.12 Josué 15.7
10 ila Nathani, nabii, na Benaya, na mashujaa, na Sulemani nduguye, hakuwaita hao.
2 Samuel 12.24 1 Rois 1.8 2 Samuel 12.1-12.15 1 Rois 1.19

Désignation de Salomon comme roi

11 Ndipo Nathani akamwambia Bath-sheba, mamaye Sulemani, akasema, Je! Hukusikia ya kuwa Adonia, mwana wa Hagithi, anamiliki, na bwana wetu Daudi hana habari?
2 Samuel 3.4 2 Samuel 12.24-12.25 1 Chroniques 22.9-22.10 2 Samuel 7.12-7.17 1 Chroniques 29.1
12 Haya basi, nikupe shauri, tafadhali, upate kuiokoa roho yako, na roho ya mwanao Sulemani.
Proverbes 20.18 2 Chroniques 21.4 1 Rois 1.21 2 Chroniques 22.10 Matthieu 21.38
13 Enenda uingie ndani kwa mfalme Daudi, ukamwambie, Je! Hukuniapia mimi mjakazi wako, Ee mfalme, bwana wangu, kusema, Hakika yake Sulemani mwana wako atamiliki baada yangu, na kuketi katika kiti changu cha enzi? Mbona basi anamiliki Adonia?
1 Rois 1.30 1 Rois 1.17 Luc 1.32-1.33 1 Chroniques 29.23 1 Chroniques 22.6-22.13
14 Tazama, wakati ule utakapokuwa katika kusema na mfalme, mimi nami nitaingia nyuma yako, na kuyahakikisha maneno yako.
2 Corinthiens 13.1 1 Rois 1.17-1.27
15 Basi Bath-sheba akaingia ndani kwa mfalme, ndani ya chumba chake; naye mfalme alikuwa mzee sana; na Abishagi, Mshunami, alikuwa akimtumikia mfalme.
1 Rois 1.1
16 Bath-sheba akainama, akamsujudia mfalme. Naye mfalme akamwuliza, Wataka nini?
1 Samuel 24.8 Matthieu 20.32 Esther 7.2 1 Rois 1.23 Matthieu 20.21
17 Akamwambia, Bwana wangu, uliniapia mimi mjakazi wako kwa Bwana, Mungu wako, ya kwamba, bila shaka Sulemani mwanao atamiliki baada yangu, yeye ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi.
1 Rois 1.13 1 Rois 1.30 Genèse 18.12 1 Pierre 3.6
18 Na sasa, angalia, Adonia anamiliki; na wewe, bwana wangu mfalme, huna habari.
1 Rois 1.24 Actes 3.17 1 Rois 1.5 2 Samuel 15.10 1 Rois 1.27
19 Tena amechinja ng’ombe, na vinono, na kondoo tele, na kuwaita wana wa mfalme wote pia, na Abiathari, kuhani, na Yoabu, jemadari wa jeshi. Ila Sulemani, mtumishi wako, huyu hakumwita.
1 Rois 1.7-1.10 1 Rois 1.25
20 Ee mfalme, bwana wangu, macho ya Israeli wote yanakuelekea wewe, kwamba uwaambie ni nani atakayeketi katika kiti chako cha enzi baada yako, Ee mfalme, bwana wangu.
1 Chroniques 28.10 Psaumes 123.2 Zacharie 3.9 2 Chroniques 20.12 1 Chroniques 22.8-22.10
21 Ama sivyo itakuwa, bwana wangu mfalme atakapolala pamoja na baba zake, mimi na mwanangu Sulemani tutahesabiwa kuwa wahalifu.
1 Rois 2.10 Deutéronome 31.16 1 Rois 2.15 1 Rois 2.22-2.24 2 Samuel 7.12
22 Basi tazama, alipokuwa katika kusema na mfalme, Nathani, nabii, aliingia.
Genèse 24.15 Daniel 9.20 Job 1.16-1.18
23 Wakamwambia mfalme wakasema, Tazama, Nathani, nabii. Naye alipoingia ndani mbele ya mfalme, akamsujudia kifudifudi.
1 Pierre 2.17 1 Rois 1.16 Romains 13.7
24 Nathani akasema, Ee mfalme, bwana wangu, je! Wewe umesema ya kwamba, Adonia atamiliki baada yangu, ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi?
1 Rois 1.5 1 Rois 1.13-1.14 1 Rois 1.17-1.18
25 Maana leo ameshuka, na kuchinja ng’ombe, na vinono, na kondoo tele, naye amewaita wana wote wa mfalme, na majemadari wa jeshi, na Abiathari, kuhani; na tazama, wanakula na kunywa mbele yake, wakisema, Na aishi mfalme Adonia!
1 Samuel 10.24 1 Rois 1.19 1 Rois 1.9 1 Chroniques 29.13 Luc 19.38
26 Walakini mimi, mimi mtumishi wako, na Sadoki, kuhani, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Sulemani, mtumishi wako, hakutuita sisi.
1 Rois 1.8 1 Rois 1.10 1 Rois 1.19 2 Samuel 7.2 2 Samuel 12.25
27 Je! Bwana wangu mfalme ndiye aliyelitenda jambo hili, bila kutujulisha sisi watumishi wako ni nani atakayeketi katika kiti cha enzi cha bwana wangu mfalme baada yake?
2 Rois 4.27 1 Rois 1.24 Jean 15.15
28 Ndipo mfalme Daudi akajibu, akasema, Niitieni Bath-sheba. Basi akaingia ndani kwa mfalme, akasimama mbele ya mfalme.
29 Naye mfalme akaapa, akasema, Bwana aishivyo, aliyenikomboa roho yangu katika shida zote,
2 Samuel 4.9 1 Rois 2.24 1 Samuel 14.45 Psaumes 138.7 Psaumes 72.14
30 hakika yake nitafanya leo kama vile nilivyokuapia kwa Bwana, Mungu wa Israeli, nikasema, Kwa yakini Sulemani mwanao atamiliki baada yangu, naye ndiye atakayeketi katika kiti changu cha enzi badala yangu.
1 Rois 1.13 1 Rois 1.17
31 Ndipo Bath-sheba akainama kifudifudi, akamsujudia mfalme, akasema, Bwana wangu mfalme Daudi na aishi milele.
Daniel 3.9 Daniel 2.4 Néhémie 2.3 Daniel 5.10 Daniel 6.6
32 Naye mfalme Daudi akasema, Niitie Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada. Nao wakaingia ndani mbele ya mfalme.
1 Rois 1.8 1 Rois 1.38 1 Rois 1.26
33 Naye mfalme akawaambia, Twaeni pamoja nanyi watumishi wa bwana wenu, mkampandishe Sulemani mwanangu juu ya nyumbu wangu mimi mkamtelemshe mpaka Gihoni;
2 Chroniques 32.30 1 Rois 1.38 2 Chroniques 33.14 2 Samuel 20.6-20.7 Lévitique 19.19
34 kisha Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na wamtie mafuta huko, awe mfalme juu ya Israeli; kapigeni panda, mkaseme, Mfalme Sulemani na aishi!
1 Rois 1.25 2 Samuel 15.10 1 Samuel 10.1 2 Rois 9.3 1 Rois 19.16
35 Kisha pandeni juu nyuma yake, naye atakuja ili aketi katika kiti changu cha enzi; kwa maana atakuwa mfalme badala yangu; ndiye niliyemweka awamiliki Israeli na Yuda.
1 Chroniques 28.4-28.5 1 Chroniques 23.1 1 Rois 2.15 1 Rois 2.12 Psaumes 2.6
36 Basi Benaya, mwana wa Yehoyada, akamjibu mfalme, akasema, Amina; Bwana, Mungu na bwana wangu mfalme, na aseme vivyo hivyo.
Matthieu 28.20 Jérémie 11.5 Psaumes 18.2 Psaumes 89.20 Matthieu 6.13
37 Kama vile Bwana alivyokuwa pamoja na bwana wangu mfalme, kadhalika na awe pamoja na Sulemani, na kufanya kiti chake cha enzi kuwa kitukufu kuliko kiti cha enzi cha bwana wangu mfalme Daudi.
1 Samuel 20.13 1 Rois 1.47 Josué 1.17 Josué 1.5 2 Rois 2.9
38 Basi wakashuka Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Wakerethi, na Wapelethi, wakampandisha Sulemani juu ya nyumbu wa mfalme Daudi, wakampeleka mpaka Gihoni.
2 Samuel 8.18 1 Rois 1.8 2 Samuel 20.20-20.23 2 Samuel 15.18 1 Rois 1.26
39 Na Sadoki, kuhani, akatwaa ile pembe ya mafuta katika Hema, akamtia Sulemani mafuta. Nao wakapiga panda; na watu wote wakasema, Mfalme Sulemani na aishi!
Psaumes 89.20 1 Samuel 10.24 1 Rois 1.34 1 Chroniques 29.22 2 Chroniques 23.13
40 Kisha watu wote wakapanda juu nyuma yake, watu wakapiga mazomari, wakafurahi furaha kubwa mno, hata nchi ikapasuka kwa sauti zao.
Luc 19.37 Apocalypse 11.15-11.18 Psaumes 97.1 2 Rois 11.20 2 Rois 11.14
41 Basi Adonia, na wageni wote waliokuwa pamoja naye, wakasikia hayo walipokuwa wamekwisha kula. Naye Yoabu aliposikia sauti ya panda alisema, Za nini kelele hizi za mji uliotaharuki?
Matthieu 21.9-21.11 Luc 17.26-17.29 Actes 21.31 Matthieu 21.15 Job 15.21-15.22
42 Naye alipokuwa katika kunena, tazama Yonathani, mwana wa Abiathari kuhani, akafika. Naye Adonia akasema, Karibu; maana wewe u mtu mwema, unaleta habari njema.
2 Samuel 15.36 2 Samuel 18.27 2 Samuel 17.17 2 Samuel 15.27 1 Rois 22.18
43 Naye Yonathani akajibu, akamwambia Adonia, Hakika bwana wetu mfalme Daudi amemtawaza Sulemani.
44 Tena mfalme alipeleka pamoja naye Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, na Benaya, mwana wa Yehoyada, na Wakerethi, na Wapelethi, wakampandisha juu ya nyumbu wa mfalme.
45 Kisha Sadoki, kuhani, na Nathani, nabii, wakamtia mafuta huko Gihoni, ili awe mfalme. Nao wamepanda juu kutoka huko wakifurahi, hata mji ukavuma. Ndizo kelele zile mlizozisikia.
1 Rois 1.40 Daniel 5.26-5.28 1 Samuel 28.14 1 Samuel 4.5 1 Rois 14.6
46 Na tena, Sulemani ameketi katika kiti cha enzi cha ufalme.
1 Chroniques 29.23 Aggée 2.22 1 Rois 1.13 Psaumes 132.11
47 Na tena, watumishi wa mfalme walifika, ili wambariki bwana wetu mfalme Daudi, wakisema, Mungu wako na alikuze jina la Sulemani kuliko jina lako, na kukifanya kiti chake cha enzi kuwa kitukufu kuliko kiti chako. Naye mfalme akainama chini juu ya kitanda chake.
Genèse 47.31 1 Rois 1.37 Psaumes 20.1-20.4 Exode 12.32 2 Samuel 8.10
48 Na tena, mfalme akasema hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, ahimidiwe, aliyenipa leo hivi mtu wa kuketi katika kiti changu cha enzi, nayo macho yangu yakiwa yanaona hayo.
1 Rois 3.6 Psaumes 132.11-132.12 Psaumes 103.1-103.2 1 Chroniques 29.20 Genèse 14.20
49 Ndipo wageni wote waliokuwa pamoja na Adonia wakaogopa, wakaondoka, wakaenda zao kila mtu njia yake.
Proverbes 28.1 Daniel 5.4-5.6 Esaïe 21.4-21.5
50 Adonia naye akaogopa mbele ya Sulemani; akaondoka, akaenda, akazishika pembe za madhabahu.
1 Rois 2.28 Psaumes 118.27 Exode 38.2 Exode 21.14 Exode 27.2
51 Akaambiwa Sulemani, kusema, Tazama, Adonia amwogopa mfalme Sulemani; kwani, tazama, amezishika pembe za madhabahu, akisema, Mfalme Sulemani na aniapie leo kwamba hataniua mimi mtumwa wake kwa upanga.
52 Akasema Sulemani, Akionekana kuwa mtu wa kweli, hata unywele mmoja wake hautaanguka chini; lakini uovu ukionekana ndani yake, atakufa.
1 Samuel 14.45 2 Samuel 14.11 Actes 27.34 Luc 21.18 Proverbes 13.6
53 Basi mfalme Sulemani akatuma watu, wakamtelemsha toka madhabahuni. Naye akaja, akamwinamia mfalme Sulemani; naye Sulemani akamwambia, Enenda nyumbani kwako.
2 Samuel 14.24 1 Rois 2.36 2 Samuel 1.2 2 Samuel 14.28 Proverbes 24.21

Cette Bible est dans le domaine public.