Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 11.3

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 11

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 10 Chapitre 12

Confiance dans l’intervention de Dieu

1 Bwana ndiye niliyemkimbilia. Mbona mnaiambia nafsi yangu, Kimbia kama ndege mlimani kwenu?
2 Maana, tazama, wasio haki wanaupinda uta, Wanaitia mishale yao katika upote, Ili kuwapiga gizani wanyofu wa moyo.
3 Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?
4 Bwana yu katika hekalu lake takatifu. Bwana ambaye kiti chake kiko mbinguni, Macho yake yanaangalia; Kope zake zinawajaribu wanadamu.
5 Bwana humjaribu mwenye haki; Bali nafsi yake humchukia asiye haki, Na mwenye kupenda udhalimu.
6 Awanyeshee wasio haki mitego, Moto na kiberiti na upepo wa hari, Na viwe fungu la kikombe chao.
7 Kwa kuwa Bwana ndiye mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watamwona uso wake.

Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 11.3 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.