Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  /  Psaumes 101

La Bible Bible en Swahili de l’est

Psaumes 101

Un clic sur un verset envoie vers le comparateur de versions.

Chapitre 100 Chapitre 102

Règne d’un roi intègre

1 Rehema na hukumu nitaziimba, Ee Bwana, nitakuimbia zaburi.
2 Nitaiangalia njia ya unyofu; Utakuja kwangu lini? Nitakwenda kwa unyofu wa moyo Ndani ya nyumba yangu.
3 Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.
4 Moyo wa ukaidi utaondoka kwangu, Lililo ovu sitalijua.
5 Amsingiziaye jirani yake kwa siri, Huyo nitamharibu. Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno, Huyo sitavumilia naye.
6 Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, Hao wakae nami. Yeye aendaye katika njia kamilifu, Ndiye atakayenitumikia.
7 Hatakaa ndani ya nyumba yangu Mtu atendaye hila. Asemaye uongo hatathibitika Mbele ya macho yangu.
8 Asubuhi hata asubuhi nitawaharibu Wabaya wote wa nchi. Niwatenge wote watendao uovu Na mji wa Bwana.


Vous êtes actuellement sur une version optimisée pour mobile, si vous souhaitez basculer sur la version complète suivez le lien suivant : Psaumes 101.1 (Lemaîtstre de Sacy)

Cette Bible est dans le domaine public.