Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 7.8
Bible en Swahili de l’est


Défaite des Philistins

1 Na hao watu wa Kiriath-yearimu wakaja, wakalichukua sanduku la Bwana, wakalileta ndani ya nyumba ya Abinadabu huko kilimani, nao wakamtenga Eleazari, mwanawe, ili alilinde sanduku la Bwana.
2 Samuel 6.2-6.4 Esaïe 52.11 1 Chroniques 13.5-13.7 1 Samuel 6.21 Josué 18.14
2 Ikawa, tangu siku hiyo ambayo sanduku lilikaa Kiriath-yearimu wakati ulikuwa mwingi; kwa maana ulikuwa miaka ishirini; na nyumba yote ya Israeli wakamwombolezea Bwana.
2 Corinthiens 7.10-7.11 Jérémie 31.9 Jérémie 3.13 Zacharie 12.10-12.11 Matthieu 5.4
3 Basi Samweli akawaambia nyumba yote ya Israeli, akasema, Ikiwa mnamrudia Bwana kwa mioyo yenu yote, basi, iondoleeni mbali miungu migeni, nayo Maashtorethi yatoke kwenu, mkamtengenezee Bwana mioyo yenu, mkamtumikie yeye peke yake; naye atawaokoa katika mikono ya Wafilisti.
Luc 4.8 Deutéronome 13.4 Deutéronome 6.13 Matthieu 4.10 Esaïe 55.7
4 Ndipo wana wa Israeli wakayaondoa Mabaali na Maashtorethi, wakamtumikia Bwana peke yake.
Juges 10.15-10.16 Juges 2.13 1 Rois 11.33 Osée 14.8 Osée 14.3
5 Samweli akasema, Wakusanyeni Israeli wote Mispa, nami nitawaombea ninyi kwa Bwana.
Juges 20.1 1 Samuel 7.16 Joël 2.16 1 Samuel 7.12 Josué 15.38
6 Wakakusanyika huko Mispa, wakateka maji na kuyamimina mbele za Bwana; wakafunga siku ile, wakasema huko, Tumemfanyia Bwana dhambi. Samweli akawaamua wana wa Israeli huko Mispa.
Juges 10.10 2 Samuel 14.14 Psaumes 106.6 1 Samuel 1.15 Joël 2.12
7 Hata Wafilisti waliposikia ya kuwa wana wa Israeli wamekusanyika huko Mispa, mashehe wa Wafilisti walipanda juu ili kupigana na Israeli. Nao wana wa Israeli waliposikia, wakawaogopa Wafilisti.
1 Samuel 17.11 1 Samuel 13.6 Exode 14.10 2 Chroniques 20.3
8 Wana wa Israeli wakamwambia Samweli, Usiache kumlilia Bwana, Mungu wetu, kwa ajili yetu, kwamba atuokoe na mikono ya Wafilisti.
Esaïe 37.4 1 Samuel 12.19-12.24 Jacques 5.16 Esaïe 62.1 Esaïe 62.6-62.7
9 Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa nzima; Samweli akamlilia Bwana kwa ajili ya Israeli; Bwana akamwitikia.
Jérémie 15.1 Psaumes 99.6 1 Samuel 9.12 1 Samuel 16.2 Jacques 5.16
10 Hata Samweli alipokuwa akiitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakakaribia ili kupigana na Israeli; walakini Bwana akapiga ngurumo, mshindo mkubwa sana, juu ya Wafilisti siku ile, akawafadhaisha; nao wakaangamizwa mbele ya Israeli.
1 Samuel 2.10 Josué 10.10 Juges 5.20 2 Samuel 22.14-22.15 Zacharie 4.6
11 Nao watu wa Israeli wakatoka Mispa, wakawafuatia Wafilisti, wakawapiga, hata walipofika chini ya Beth-kari.
12 Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia.
Josué 4.9 Genèse 35.14 Actes 26.22 Genèse 31.45-31.52 1 Samuel 5.1
13 Hivyo Wafilisti walishindwa, wasiingie tena ndani ya mipaka ya Israeli; na mkono wa Bwana ulikuwa juu ya Wafilisti siku zote za Samweli.
Juges 13.1 1 Samuel 17.49-17.53 1 Samuel 28.3-28.5 Juges 13.5 1 Samuel 13.1-13.5
14 Nayo miji ile Wafilisti waliyokuwa wamewapokonya Waisraeli ilirudishwa tena kwa Israeli, tokea Ekroni mpaka Gathi; na Waisraeli wakauokoa mpaka wake mikononi mwa Wafilisti. Tena kulikuwa na amani kati ya Israeli na Waamori.
Juges 4.17 Deutéronome 7.16 Psaumes 106.34 Deutéronome 7.2
15 Naye huyo Samweli akawaamua Israeli siku zote za maisha yake.
1 Samuel 7.6 Juges 2.16 1 Samuel 25.1 Juges 3.10-3.11 1 Samuel 12.11
16 Naye huenda mwaka kwa mwaka kuzunguka mpaka Betheli, na Gilgali, na Mispa; akawaamua Israeli mahali hapo pote.
Psaumes 82.3-82.4 Juges 10.4 Juges 5.10 Psaumes 75.2 Juges 12.14
17 Na kurudi kwake kulikuwa mpaka Rama; maana ndipo ilipokuwa nyumba yake; nako ndiko alikowaamua Israeli; na huko akamjengea Bwana madhabahu.
1 Samuel 1.19 1 Samuel 1.1 1 Samuel 8.4 Juges 21.4-21.5 1 Samuel 11.15

Cette Bible est dans le domaine public.