Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Jean 3.4
Bible en Swahili de l’est


Caractéristiques des enfants de Dieu

1 Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.
Jean 1.12 Galates 3.26 Galates 4.5-4.6 2 Corinthiens 6.18 Jean 3.16
2 Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.
2 Corinthiens 3.18 1 Corinthiens 13.12 Colossiens 3.4 Romains 8.18 2 Pierre 1.4
3 Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.
2 Corinthiens 7.1 1 Jean 2.6 2 Pierre 3.14 Matthieu 5.48 Colossiens 1.5
4 Kila atendaye dhambi, afanya uasi; kwa kuwa dhambi ni uasi.
1 Jean 5.17 Romains 4.15 2 Corinthiens 12.21 Romains 3.20 Romains 7.7-7.13
5 Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.
2 Corinthiens 5.21 Hébreux 9.28 1 Jean 1.2 Jean 1.29 1 Pierre 2.22
6 Kila akaaye ndani yake hatendi dhambi; kila atendaye dhambi hakumwona yeye, wala hakumtambua.
3 Jean 1.11 1 Jean 2.4 1 Jean 3.9 1 Jean 4.8 1 Jean 3.2
7 Watoto wadogo, mtu na asiwadanganye; atendaye haki yuna haki, kama yeye alivyo na haki;
1 Jean 2.29 Romains 2.13 1 Jean 2.1 1 Pierre 1.15-1.16 1 Jean 2.26
8 atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.
Jean 8.44 Hébreux 2.14 Jean 16.11 Matthieu 13.38 1 Jean 3.5
9 Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu.
1 Jean 5.18 Jean 1.13 1 Jean 2.29 1 Jean 5.1 1 Pierre 1.23
10 Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.
1 Jean 4.8 1 Jean 4.21 1 Jean 4.6 3 Jean 1.11 1 Jean 4.3-4.4
11 Maana, hii ndiyo habari mliyoisikia tangu mwanzo, kwamba tupendane sisi kwa sisi;
2 Jean 1.5 Jean 15.12 1 Jean 4.21 1 Jean 1.5 1 Pierre 3.8
12 si kama Kaini alivyokuwa wa yule mwovu, akamwua ndugu yake. Naye alimwua kwa sababu gani? Kwa sababu matendo yake yalikuwa mabaya, na ya ndugu yake yalikuwa ya haki.
Hébreux 11.4 Jude 1.11 Proverbes 29.27 Psaumes 37.12 1 Pierre 4.4
13 Ndugu zangu, msistaajabu, ulimwengu ukiwachukia.
Jean 17.14 Jean 15.18-15.19 Luc 21.17 Jean 7.7 Marc 13.13
14 Sisi tunajua ya kuwa tumepita toka mautini kuingia uzimani, kwa maana twawapenda ndugu. Yeye asiyependa, akaa katika mauti.
Jean 5.24 1 Jean 5.2 Jean 13.35 1 Thessaloniciens 4.9 Jean 15.12
15 Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake.
Matthieu 5.21-5.22 Actes 23.14 Apocalypse 21.8 Jean 8.44 Galates 5.20-5.21
16 Katika hili tumelifahamu pendo, kwa kuwa yeye aliutoa uhai wake kwa ajili yetu; imetupasa na sisi kuutoa uhai wetu kwa ajili ya hao ndugu.
Jean 3.16 1 Jean 4.9-4.11 Jean 13.34 Ephésiens 5.2 Apocalypse 1.5
17 Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?
1 Jean 4.20 Hébreux 13.16 Esaïe 58.7-58.10 Proverbes 19.17 Deutéronome 15.7-15.11
18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli.
Jacques 2.15-2.16 Romains 12.9 Matthieu 25.41-25.45 Ezéchiel 33.31 1 Corinthiens 13.4-13.7
19 Katika hili tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, nasi tutaituliza mioyo yetu mbele zake,
Hébreux 10.22 1 Jean 3.21 Hébreux 11.13 Romains 8.38 Esaïe 32.17
20 ikiwa mioyo yetu inatuhukumu; kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu naye anajua yote.
Jérémie 17.10 1 Corinthiens 4.4 Hébreux 4.13 Psaumes 139.1-139.4 1 Jean 4.4
21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu;
1 Jean 2.28 Job 22.26 2 Corinthiens 1.12 1 Jean 5.14 Hébreux 4.16
22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.
Marc 11.24 Jean 9.31 1 Jean 5.14 Jean 15.7 Matthieu 21.22
23 Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri.
Jean 13.34 Jean 15.12 1 Jean 3.11 1 Pierre 1.22 1 Pierre 4.8
24 Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.
1 Corinthiens 3.16 1 Jean 4.12-4.13 Jean 17.21 1 Jean 2.6 2 Corinthiens 6.16

Cette Bible est dans le domaine public.