Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 26.10
Bible en Swahili de l’est


Les premières récoltes

1 Na itakuwa, ukiisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi, na kuimiliki, na kukaa ndani yake;
Deutéronome 13.1 Nombres 15.18 Deutéronome 5.31 Deutéronome 17.14 Nombres 15.2
2 twaa malimbuko ya ardhi, utakayoyavuna katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako; ukayatie katika kikapu, ukaende hata mahali pale atakapopachagua Bwana, Mungu wako, ili alikalishe jina lake huko.
Exode 23.16 Exode 23.19 Exode 34.26 Deutéronome 16.10 2 Chroniques 6.6
3 Ukamwendee kuhani atakayekuwapo siku zile, ukamwambie, Ninakiri leo kwa Bwana, Mungu wako, ya kuwa nimeingia katika nchi Bwana aliyowaapia baba zetu ya kwamba atatupa.
Hébreux 13.15 Genèse 17.8 Genèse 26.3 Hébreux 7.26 Hébreux 6.16-6.18
4 Naye kuhani atakipokea kikapu mkononi mwako, akiweke chini mbele ya madhabahu ya Bwana, Mungu wako.
Matthieu 5.23-5.24 Hébreux 13.10-13.12 Matthieu 23.19
5 Nawe ujibu, ukaseme mbele za Bwana, Mungu wako, Baba yangu alikuwa Mwarami karibu na kupotea, akashuka Misri, akakaa huko ugenini, nao ni wachache hesabu yao; akawa taifa kubwa huko, yenye nguvu na watu wengi.
Deutéronome 10.22 Genèse 46.27 Genèse 43.1-43.2 Actes 7.15 Genèse 45.7
6 Wamisri wakatuonea, wakatutesa, wakatutumikisha utumwa mzito.
Exode 1.11 Exode 1.14 Exode 1.22 Exode 5.9 Exode 5.19
7 Tukamlilia Bwana, Mungu wa baba zetu; Bwana akasikia sauti yetu, akaona na taabu yetu, na kazi yetu, na kuonewa kwetu.
Exode 3.9 2 Samuel 16.12 Psaumes 103.1-103.2 Ephésiens 3.20-3.21 Exode 2.23-3.4
8 Bwana akatutoa kutoka Misri kwa mkono wa nguvu, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa utisho mwingi, na kwa ishara, na kwa maajabu;
Deutéronome 4.34 Exode 12.51 Exode 12.37 Exode 12.41 Exode 14.16-14.31
9 naye ametuingiza mahali hapa, na kutupa nchi hii, nchi ijaayo maziwa na asali.
Exode 3.8 1 Samuel 7.12 Actes 26.22 Psaumes 105.44 Ezéchiel 20.15
10 Na sasa, tazama, nimeleta malimbuko ya mazao ya ardhi uliyonipa, Ee Bwana. Kisha ukiweke chini mbele za Bwana, Mungu wako, ukasujudu mbele za Bwana, Mungu wako;
1 Chroniques 29.14 1 Pierre 4.10-4.11 Esaïe 66.23 Psaumes 86.9 1 Corinthiens 10.31
11 ukayafurahie mema yote ambayo Bwana, Mungu wako, amekupa, na nyumba yako, wewe, na Mlawi, na mgeni aliye kati yako.
Deutéronome 12.7 Deutéronome 16.11 Deutéronome 12.12 Zacharie 9.17 Psaumes 63.3-63.5

Les dîmes de la troisième année

12 Utakapokwisha kutoa zaka, katika zaka zote za maongeo yako mwaka wa tatu, ambao ndio mwaka wa kutolea zaka, umpe zile zaka Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, wapate kula ndani ya malango yako na kushiba;
Lévitique 27.30 Nombres 18.24 Deutéronome 12.17-12.19 Deutéronome 14.22-14.29 Philippiens 4.18-4.19
13 nawe sema mbele ya Bwana, Mungu wako, Vitu vilivyo vitakatifu nimeviondoa katika nyumba yangu, nami mimewapa Mlawi, na mgeni, na yatima, na mjane, kwa mfano wa maagizo yako uliyoniusia yote; sikukosa maagizo yako yo yote, wala sikuyasahau;
Psaumes 119.176 Psaumes 119.141 Psaumes 119.153 1 Thessaloniciens 2.10 Psaumes 119.139
14 katika vitu hivyo sikula wakati wa kukaa matanga mimi, wala sikuviondoa nikiwa na unajisi, wala sikutoa kwa ajili ya wafu katika vitu hivyo; sauti ya Bwana, Mungu wangu, nimeisikiza, nimefanya yote, kama ulivyoniamuru.
Lévitique 7.20 Osée 9.4 Lévitique 21.11 Lévitique 21.1 Ezéchiel 24.17
15 Uangalie kutoka makazi yako matakatifu mbinguni, uwabarikie watu wako Israeli, na nchi uliyotupa kama ulivyowaapia baba zetu, nchi imiminikayo maziwa na asali.
Esaïe 63.15 Zacharie 2.13 1 Rois 8.27 1 Rois 8.43 Jérémie 31.23
16 Leo hivi akuamuru Bwana, Mungu wako, kuzifanya amri hizi na hukumu; basi uzishike na kuzifanya kwa moyo wako wote na roho yako yote.
1 Jean 5.2-5.3 Deutéronome 8.2 Deutéronome 12.32 Deutéronome 11.1 Jean 14.21-14.24
17 Umemwungama Bwana leo, kuwa ndiye Mungu wako, na kuwa yakupasa kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na maagizo yake, na hukumu zake, na kusikiza sauti yake;
Exode 24.7 Josué 22.5 1 Corinthiens 6.19-6.20 Esaïe 12.2 Esaïe 44.5
18 naye Bwana amekuungama hivi leo kuwa taifa iliyotengwa iwe yake yeye, kama alivyokuahidi, na kuwa yakupasa kushika maagizo yake yote;
Deutéronome 14.2 Deutéronome 7.6 Deutéronome 28.9 Exode 6.7 Tite 2.14
19 na kuwa atakutukuza juu ya mataifa yote aliyoyafanya, kwa sifa, na jina, na heshima, nawe upate kuwa taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, kama alivyosema.
Deutéronome 7.6 Deutéronome 28.1 1 Pierre 2.9 Deutéronome 4.7-4.8 Exode 19.6

Cette Bible est dans le domaine public.