Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Galates 1.14
Bible en Swahili de l’est


Salutation et reproche

1 Paulo, mtume, (si mtume wa wanadamu, wala kutumwa na mwanadamu, bali na Yesu Kristo, na Mungu Baba aliyemfufua kutoka kwa wafu),
Galates 1.11-1.12 Actes 9.6 Hébreux 13.20 Actes 22.10 2 Corinthiens 1.1
2 na ndugu wote walio pamoja nami, kwa makanisa ya Galatia;
Philippiens 4.21 1 Corinthiens 16.1 Actes 9.31 Philippiens 2.22 Actes 15.41
3 Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba, na kwa Bwana wetu Yesu Kristo;
2 Thessaloniciens 1.2 1 Corinthiens 1.3 Colossiens 1.2 Philippiens 1.2 2 Jean 1.3
4 ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu.
Galates 2.20 Matthieu 20.28 Ephésiens 2.2 2 Corinthiens 4.4 Romains 12.2
5 Utukufu una yeye milele na milele, Amina.
Romains 11.36 Jude 1.25 Romains 16.27 Apocalypse 4.9-4.11 1 Pierre 5.11
6 Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.
2 Corinthiens 11.4 Galates 5.7-5.8 Psaumes 106.13 Esaïe 29.13 Romains 10.3
7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.
Actes 15.24 Galates 5.10 2 Corinthiens 11.13 Romains 16.17-16.18 2 Corinthiens 2.17
8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.
1 Corinthiens 16.22 2 Corinthiens 11.13-11.14 Romains 9.3 Apocalypse 22.18-22.19 Matthieu 25.41
9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe.
Apocalypse 22.18-22.19 Deutéronome 12.32-13.11 Deutéronome 4.2 Romains 16.17 Proverbes 30.6
10 Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
1 Thessaloniciens 2.4 Actes 5.29 Jacques 4.4 Ephésiens 6.6 Romains 2.29

Paul et les autres apôtres : un même Évangile

11 Kwa maana, ndugu zangu, injili hiyo niliyowahubiri, nawajulisha ya kuwa siyo ya namna ya kibinadamu.
1 Corinthiens 2.9-2.10 1 Corinthiens 11.23 Ephésiens 3.3-3.8 1 Corinthiens 15.1-15.3 Galates 1.1
12 Kwa kuwa sikuipokea kwa mwanadamu wala sikufundishwa na mwanadamu, bali kwa ufunuo wa Yesu Kristo.
Galates 1.16 1 Corinthiens 11.23 2 Corinthiens 12.1 Galates 1.1 1 Corinthiens 2.10
13 Maana mmesikia habari za mwenendo wangu zamani katika dini ya Kiyahudi, kwamba naliliudhi kanisa la Mungu kupita kiasi, nikaliharibu.
Actes 8.3 Actes 9.21 Actes 26.4-26.5 1 Corinthiens 15.9 Actes 26.9-26.11
14 Nami naliendelea katika dini ya Kiyahudi kuliko wengi walio hirimu zangu katika kabila yangu, nikajitahidi sana katika kuyashika mapokeo ya baba zangu.
1 Pierre 1.8 Actes 26.9 Matthieu 15.2-15.3 Matthieu 15.6 Jérémie 9.14
15 Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake,
Jérémie 1.5 Esaïe 49.1 Esaïe 49.5 Actes 9.15 Romains 1.1
16 alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu;
Matthieu 16.17 Actes 9.15 1 Timothée 2.7 Galates 1.11-1.12 1 Corinthiens 15.50
17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski.
Actes 9.20-9.25 Galates 1.18 2 Corinthiens 11.32-11.33
18 Kisha, baada ya miaka mitatu, nalipanda kwenda Yerusalemu ili nionane na Kefa, nikakaa kwake siku kumi na tano.
Actes 9.26-9.29 Actes 9.22-9.23 Actes 22.17-22.18
19 Lakini sikumwona mtume mwingine, ila Yakobo, ndugu yake Bwana.
Matthieu 13.55 Matthieu 12.46 Marc 6.3 1 Corinthiens 9.5 Luc 6.15
20 Na hayo ninayowaandikia, angalieni, mbele za Mungu, sisemi uongo.
Romains 9.1 2 Corinthiens 11.31 2 Corinthiens 11.10-11.11
21 Baadaye nalikwenda pande za Shamu na Kilikia.
Actes 9.30 Actes 6.9 Actes 15.23 Actes 15.41 Actes 13.1
22 Lakini sikujulikana uso wangu na makanisa ya Uyahudi yaliyokuwa katika Kristo;
1 Thessaloniciens 2.14 Romains 16.7 Actes 9.31 2 Thessaloniciens 1.1 1 Thessaloniciens 1.1
23 ila wamesikia tu ya kwamba huyo aliyetuudhi hapo kwanza, sasa anaihubiri imani ile aliyoiharibu zamani.
Actes 6.7 1 Corinthiens 15.8-15.10 Actes 9.13 Actes 9.20 Actes 9.26
24 Wakamtukuza Mungu kwa ajili yangu.
Actes 11.18 2 Corinthiens 9.13 Luc 2.14 Nombres 23.23 2 Thessaloniciens 1.10

Cette Bible est dans le domaine public.