Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 1.33
Bible en Swahili de l’est


Naissance et jeunesse de Jésus

Objectif de l’auteur

1 Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,
Actes 1.1-1.3 Jean 20.31 2 Pierre 1.16-1.19 2 Timothée 4.17 1 Timothée 3.16
2 kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,
Jean 15.27 Hébreux 2.3 Actes 26.16 Marc 1.1 2 Pierre 1.16
3 nimeona vema mimi nami, kwa kuwa nimejitafutia usahihi wa mambo hayo yote tangu mwanzo, kukuandikia kwa taratibu, Theofilo mtukufu,
Actes 1.1 Actes 26.25 Actes 23.26 Actes 11.4 Actes 24.3
4 upate kujua hakika ya mambo yale uliyofundishwa.
Jean 20.31 Actes 18.25 2 Pierre 1.15-1.16 Romains 2.18 1 Corinthiens 14.19

Annonce de la naissance de Jean-Baptiste

5 Zamani za Herode, mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja, jina lake Zakaria, wa zamu ya Abiya, na mkewe alikuwa mmojawapo wa uzao wa Haruni, jina lake Elisabeti.
1 Chroniques 24.10 Matthieu 2.1 Néhémie 12.4 Néhémie 12.17 1 Chroniques 24.19
6 Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiendelea katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama.
Genèse 7.1 Genèse 17.1 1 Thessaloniciens 3.13 1 Rois 9.4 Philippiens 2.15
7 Nao walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili ni wazee sana.
Hébreux 11.11 Genèse 18.11 1 Samuel 1.2 Genèse 25.21 Juges 13.2-13.3
8 Basi ikawa, alipokuwa akifanya kazi ya ukuhani katika taratibu ya zamu yake mbele za Mungu,
1 Chroniques 24.19 2 Chroniques 8.14 2 Chroniques 31.2 Luc 1.5 Exode 28.41
9 kama ilivyokuwa desturi ya ukuhani, kura ilimwangukia kuingia katika hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba.
2 Chroniques 29.11 1 Chroniques 23.13 Exode 30.7-30.8 1 Samuel 2.28 Exode 37.25-37.29
10 Na makutano yote ya watu walikuwa wakisali nje saa ya kufukiza uvumba.
Lévitique 16.17 Apocalypse 8.3 Hébreux 9.24 Hébreux 4.14
11 Akatokewa na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia.
Exode 40.26-40.27 Apocalypse 8.3-8.4 Juges 13.9 Exode 30.1-30.10 Lévitique 16.13
12 Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.
Juges 6.22 Juges 13.22 Luc 2.9-2.10 Luc 1.29 Apocalypse 1.17
13 Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana.
Juges 13.3-13.5 Psaumes 127.3-127.5 1 Samuel 2.21 Psaumes 113.9 Actes 10.31
14 Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake.
Luc 1.58 Genèse 21.6 Proverbes 15.20 Proverbes 23.24 Proverbes 23.15
15 Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye.
Luc 7.33 Galates 1.15 Jérémie 1.5 Ephésiens 5.18 Actes 2.4
16 Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao.
Matthieu 21.32 Malachie 3.1 Daniel 12.3 Esaïe 49.6 Esaïe 40.3-40.5
17 Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa.
Malachie 4.5-4.6 Matthieu 11.14 Luc 1.76 Psaumes 78.8 Jean 1.21-1.30
18 Zakaria akamwambia malaika, Nitajuaje neno hilo? Maana mimi ni mzee, na mke wangu ni mkongwe wa siku nyingi.
Genèse 17.17 Luc 1.34 Genèse 15.8 Genèse 18.12 Luc 1.7
19 Malaika akamjibu akamwambia, Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu; nami nimetumwa niseme nawe, na kukupasha habari hizi njema.
Matthieu 18.10 Daniel 8.16 Luc 1.26 Daniel 9.21-9.23 Hébreux 4.14
20 Na tazama! Utakuwa bubu, usiweze kusema, mpaka siku ile yatakapotukia hayo, kwa sababu hukuyasadiki maneno yangu; nayo yatatimizwa kwa wakati wake.
Ezéchiel 3.26 Ezéchiel 24.27 Marc 9.19 2 Rois 7.2 Genèse 18.10-18.15
21 Na wale watu walikuwa wakimngojea Zakaria, wakastaajabia kukawia kwake mle hekaluni.
Nombres 6.23-6.27
22 Alipotoka hali hawezi kusema nao, walitambua ya kuwa ameona maono ndani ya hekalu, naye aliendelea kuwaashiria akakaa bubu.
Luc 1.62 Actes 12.17 Actes 19.33 Actes 21.40 Jean 13.24
23 Ikawa siku za huduma yake zilipokuwa zimetimia akaenda nyumbani kwake.
1 Chroniques 9.25 2 Rois 11.5-11.7
24 Hata baada ya siku zile mkewe Elisabeti alichukua mimba akatawa miezi mitano, akisema,
25 Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana katika siku zile alizoniangalia ili kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.
Esaïe 4.1 Genèse 30.22-30.23 Hébreux 11.11 1 Samuel 1.6 Genèse 21.1-21.2

Annonce de la naissance de Jésus

26 Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti,
Matthieu 2.23 Luc 1.19 Jean 7.41 Luc 2.4 Jean 1.45-1.46
27 kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu.
Matthieu 1.18 Esaïe 7.14 Matthieu 1.16 Jérémie 31.22 Luc 2.4-2.5
28 Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
Juges 6.12 Luc 1.30 Actes 18.10 Juges 5.24 Luc 1.42
29 Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
Actes 10.4 Luc 1.12 Luc 1.66 Luc 2.51 Actes 10.17
30 Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
Luc 1.13 Romains 8.31 Esaïe 41.14 Actes 27.24 Esaïe 43.1-43.4
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
Esaïe 7.14 Matthieu 1.21 Matthieu 1.25 Luc 2.21 Matthieu 1.23
32 Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake.
Esaïe 9.6-9.7 Esaïe 16.5 Psaumes 132.11 Marc 5.7 Luc 1.35
33 Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho.
Daniel 2.44 Hébreux 1.8 Daniel 7.27 Daniel 7.13-7.14 2 Samuel 7.16
34 Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?
Actes 9.6 Juges 13.8-13.12
35 Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.
Matthieu 1.18 Luc 1.27 Matthieu 1.20 Jean 1.49 Luc 1.31-1.32
36 Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa;
37 kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu.
Matthieu 19.26 Jérémie 32.17 Luc 18.27 Marc 10.27 Genèse 18.14
38 Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.
Psaumes 116.16 Romains 4.20-4.21 2 Samuel 7.25-7.29 Psaumes 119.38
39 Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda,
Luc 1.65 Josué 15.48-15.59 Josué 10.40 Josué 20.7 Josué 21.9-21.11
40 akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.
41 Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;
Actes 4.8 Luc 1.67 Luc 1.15 Apocalypse 1.10 Luc 1.44
42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
Juges 5.24 Luc 1.48 Luc 19.38 Luc 1.28 Actes 2.26-2.28
43 Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?
Jean 20.28 Psaumes 110.1 1 Samuel 25.41 Ruth 2.10 Jean 13.13
44 Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.
45 Naye heri aliyesadiki; kwa maana yatatimizwa aliyoambiwa na Bwana.
2 Chroniques 20.20 Jean 20.29 Jean 11.40 Luc 11.27-11.28 Luc 1.20
46 Mariamu akasema, Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
Psaumes 34.2-34.3 1 Samuel 2.1-2.10 Psaumes 35.9 Psaumes 103.1-103.2 Esaïe 61.10
47 Na roho yangu imemfurahia Mungu, Mwokozi wangu;
1 Timothée 1.1 Psaumes 35.9 Tite 2.10 1 Timothée 2.3 Zacharie 9.9
48 Kwa kuwa ameutazama Unyonge wa mjakazi wake. Kwa maana, tazama, tokea sasa Vizazi vyote wataniita mbarikiwa;
Psaumes 138.6 Luc 11.27 Luc 1.28 Malachie 3.12 1 Samuel 1.11
49 Kwa kuwa Mwenye nguvu amenitendea makuu, Na jina lake ni takatifu.
Psaumes 111.9 Psaumes 126.2-126.3 Psaumes 99.3 Esaïe 57.15 Genèse 17.1
50 Na rehema zake hudumu vizazi hata vizazi Kwa hao wanaomcha.
Psaumes 103.17-103.18 Exode 20.6 Psaumes 145.19 Psaumes 31.19 Psaumes 115.13
51 Amefanya nguvu kwa mkono wake; Amewatawanya walio na kiburi katika mawazo ya mioyo yao;
Psaumes 98.1 Esaïe 52.10 Esaïe 40.10 Esaïe 51.9 Daniel 4.37
52 Amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; Na wanyonge amewakweza.
Psaumes 107.40-107.41 Jacques 4.10 Ezéchiel 17.24 Ecclésiaste 4.14 Job 5.11-5.13
53 Wenye njaa amewashibisha mema, Na wenye mali amewaondoa mikono mitupu.
Luc 6.21 Psaumes 107.8-107.9 Matthieu 5.6 Jacques 2.5-2.6 Psaumes 34.10
54 Amemsaidia Israeli, mtumishi wake; Ili kukumbuka rehema zake;
Psaumes 98.3 Michée 7.20 Esaïe 44.21 Jérémie 31.20 Zacharie 9.9-9.11
55 Kama alivyowaambia baba zetu, Ibrahimu na uzao wake hata milele.
Genèse 17.19 Psaumes 105.6-105.10 Psaumes 132.11-132.17 Romains 11.28-11.29 Genèse 28.14
56 Mariamu akakaa naye kadiri ya miezi mitatu, kisha akarudi kwenda nyumbani kwake.

Naissance de Jean-Baptiste

57 Ikawa, siku za kuzaa kwake Elisabeti zilipotimia, alizaa mtoto mwanamume.
Luc 2.6-2.7 Luc 1.13 Nombres 23.19 Genèse 21.2-21.3
58 Wakasikia jirani zake na jamaa zake ya kwamba Bwana amemwongezea rehema zake, wakafurahi pamoja naye.
Luc 1.14 Romains 12.15 Psaumes 113.9 Luc 1.25 1 Corinthiens 12.26
59 Ikawa siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto; wakataka kumpa jina la babaye, Zakaria.
Luc 2.21 Philippiens 3.5 Lévitique 12.3 Genèse 17.12 Actes 7.8
60 Mamaye akajibu akasema La, sivyo; bali, ataitwa Yohana.
Luc 1.13 2 Samuel 12.25 Esaïe 8.3 Luc 1.63 Matthieu 1.25
61 Wakamwambia, Hapana mtu katika jamaa zako aitwaye jina hilo.
62 Wakamwashiria babaye wajue atakavyo kumwita.
Luc 1.22
63 Akataka kibao, akaandika ya kwamba, Jina lake ni Yohana. Wakastaajabu wote.
Luc 1.60 Luc 1.13 Esaïe 30.8 Habakuk 2.2 Proverbes 3.3
64 Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake pia, akaanza kunena akimsifu Mungu.
Luc 1.20 Exode 4.15-4.16 Ezéchiel 33.22 Daniel 4.34-4.37 Jérémie 1.9
65 Wakaingiwa na hofu wote waliokuwa wakikaa karibu nao; na mambo hayo yote yakatangazwa katika nchi yote ya milima milima ya Uyahudi.
Luc 1.39 Luc 7.16 Actes 5.5 Josué 10.6 Josué 10.40
66 Na wote walioyasikia wakayaweka mioyoni mwao, wakisema, Mtoto huyu atakuwa wa namna gani? Kwa sababu mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
Actes 11.21 Luc 2.19 Luc 2.51 Genèse 39.2 Genèse 37.11
67 Na Zakaria, baba yake, akajazwa Roho Mtakatifu, akatabiri, akisema,
Joël 2.28 Luc 1.41 Luc 1.15 Nombres 11.25 2 Samuel 23.2
68 Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, Kwa kuwa amewajia watu wake, na kuwakomboa.
Luc 7.16 Psaumes 106.48 Psaumes 41.13 Psaumes 111.9 1 Rois 1.48
69 Ametusimamishia pembe ya wokovu Katika mlango wa Daudi, mtumishi wake.
1 Samuel 2.10 Psaumes 18.2 2 Samuel 22.3 Ezéchiel 29.21 1 Samuel 2.1
70 Kama alivyosema tangu mwanzo Kwa kinywa cha manabii wake watakatifu;
Romains 1.2 Actes 3.21-3.24 1 Pierre 1.12 2 Samuel 23.2 2 Pierre 1.21
71 Tuokolewe na adui zetu Na mikononi mwao wote wanaotuchukia;
Psaumes 106.10 Ezéchiel 34.28 Esaïe 54.7-54.17 Ezéchiel 38.8 Sophonie 3.15-3.20
72 Ili kuwatendea rehema baba zetu, Na kulikumbuka agano lake takatifu;
Michée 7.20 Psaumes 106.45 Lévitique 26.42 Ezéchiel 16.60 Hébreux 6.13-6.18
73 Uapo aliomwapia Ibrahimu, baba yetu,
Genèse 22.16-22.18 Jérémie 11.5 Psaumes 105.9 Deutéronome 7.12 Hébreux 6.13
74 Ya kwamba atatujalia sisi, Tuokoke mikononi mwa adui zetu, Na kumwabudu pasipo hofu,
Sophonie 3.15-3.17 Esaïe 54.13-54.14 2 Timothée 1.7 Hébreux 9.14 Zacharie 9.8-9.10
75 Kwa utakatifu na kwa haki Mbele zake siku zetu zote.
Ephésiens 4.24 Ephésiens 2.10 Tite 2.11-2.14 1 Pierre 1.14-1.16 Jérémie 31.33-31.34
76 Nawe, mtoto, utaitwa nabii wake Aliye juu, Kwa maana utatangulia mbele za uso wa Bwana umtengenezee njia zake;
Malachie 3.1 Luc 1.32 Marc 1.2-1.3 Matthieu 3.3 Matthieu 14.5
77 Uwajulishe watu wake wokovu, Katika kusamehewa dhambi zao.
Jean 3.27-3.36 Luc 3.3 Luc 7.47-7.50 Actes 19.4 Jean 1.15-1.17
78 Kwa njia ya rehema za Mungu wetu, Ambazo kwa hizo mwangaza utokao juu umetufikia,
Malachie 4.2 Esaïe 11.1 2 Pierre 1.19 Zacharie 3.8 Colossiens 3.12
79 Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.
Esaïe 9.2 Matthieu 4.16 Actes 26.18 Romains 3.17 Psaumes 85.10-85.13
80 Yule mtoto akakua, akaongezeka nguvu rohoni, akakaa majangwani hata siku ya kutokea kwake kwa Israeli.
Luc 2.40 Matthieu 3.1 Luc 2.52 1 Samuel 3.19-3.20 Juges 13.24-13.25

Cette Bible est dans le domaine public.