Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 16.1
Bible en Swahili de l’est


Révolte de Koré, Dathan et Abiram

1 Basi Kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohathi, mwana wa Lawi, akatwaa watu, pamoja na Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi, waliokuwa wana wa Reubeni;
Jude 1.11 Exode 6.21 Exode 6.18 Nombres 27.3 Genèse 49.3-49.4
2 nao, pamoja na watu kadha wa kadha wa wana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, Wakuu wa mkutano, waliokuwa wateule wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa;
Nombres 26.9 1 Chroniques 5.24 1 Chroniques 12.30 Genèse 6.4 Ezéchiel 16.14
3 nao wakakusanyika kinyume cha Musa na Haruni, na kuwaambia, Ninyi inawatosha, kwa kuwa mkutano wote ni mtakatifu, kila mmoja miongoni mwao, Bwana naye yu kati yao; n’nini basi kujitukuza juu ya mkutano wa Bwana?
Psaumes 106.16 Exode 19.6 Nombres 14.14 Nombres 16.7 Matthieu 3.9-3.10
4 Musa aliposikia maneno haya, akapomoka kifudifudi;
Nombres 14.5 Nombres 20.6 Josué 7.6 Nombres 16.45
5 kisha akanena na Kora na mkutano wake wote, akawaambia, Asubuhi Bwana ataonyesha ni kina nani walio wake, kisha ni nani aliye mtakatifu, tena ni nani atakayemkaribisha kwake; maana, yeye atakayemchagua ndiye atakayemsongeza kwake.
Psaumes 65.4 Nombres 17.5 Lévitique 10.3 2 Timothée 2.19 Psaumes 105.26
6 Fanyeni neno hili; twaeni vyetezo, ninyi Kora na mkutano wake wote;
Lévitique 10.1 Nombres 16.46-16.48 1 Rois 18.21-18.23 Nombres 16.35-16.40 Lévitique 16.12-16.13
7 vitieni na moto, mkaweke na uvumba juu yake mbele za Bwana kesho; kisha itakuwa ya kwamba mtu Bwana atakayemchagua, yeye atakuwa mtakatifu; inawatosha ninyi, enyi wana wa Lawi.
Nombres 16.3 Ephésiens 1.4 2 Thessaloniciens 2.13 Nombres 16.5 Matthieu 21.23-21.27
8 Musa akamwambia Kora, Sikizeni basi, enyi Wana wa Lawi;
9 Je! Mwaona kuwa ni jambo dogo kwenu, kuwa Mungu wa Israeli amewatenga ninyi na mkutano wa Israeli, ili apate kuwakaribisha kwake; ili mfanye utumishi wa maskani ya Bwana, na kusimama mbele ya mkutano ili kuwatumikia;
Deutéronome 10.8 Esaïe 7.13 Ezéchiel 44.10-44.11 Nombres 16.13 1 Samuel 18.23
10 tena ya kuwa amekuleta uwe karibu, na ndugu zako wote wana wa Lawi pamoja nawe? Nanyi, je! Mwataka na ukuhani pia?
Luc 22.24 Philippiens 2.3 Nombres 3.10 Romains 12.10 Proverbes 13.10
11 Kwa sababu hii wewe na mkutano wako wote mmekusanyika kinyume cha Bwana; na Haruni, je! Yeye ni nani hata mkamnung’unikia?
Exode 16.7-16.8 Exode 17.2 1 Corinthiens 3.5 Nombres 16.3 Romains 13.2
12 Kisha Musa akatuma kuwaita Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu; nao wakasema, Hatuji sisi;
Esaïe 3.5 Proverbes 29.9 Jude 1.8 1 Pierre 2.13-2.14
13 je! Ni jambo dogo, wewe kutuleta kutoka nchi iliyojawa na maziwa na asali, ili kutuua jangwani, lakini pamoja na haya wajikuza mwenyewe uwe mkuu juu yetu kabisa?
Actes 7.35 Nombres 11.5 Exode 2.14 Exode 16.3 Exode 2.23
14 Kisha, hukutuleta katika nchi iliyojawa na maziwa na asali, wala hukutupa urithi wa mashamba, na mashamba ya mizabibu; je! Unataka kuwatoboa macho watu hawa? Hatuji.
Lévitique 20.24 Nombres 20.5 Exode 3.8 Exode 3.17 Nombres 36.8-36.10
15 Musa akakasirika sana, akamwambia Bwana. Usiikubali sadaka yao; mimi sikutwaa hata punda mmoja kwao, wala sikumwumiza hata mtu mmoja miongoni mwao.
Genèse 4.4-4.5 2 Corinthiens 7.2 1 Thessaloniciens 2.10 Actes 20.33-20.34 1 Corinthiens 9.15
16 Kisha Musa akamwambia Kora, Wewe na mkutano wako wote iweni hapa mbele ya Bwana kesho, wewe, na wao, na Haruni;
1 Samuel 12.3 1 Samuel 12.7 2 Timothée 2.14 Nombres 16.6-16.7
17 mkatwae kila mtu chetezo chake, na kutia uvumba juu yake, mkavilete mbele za Bwana, vyetezo mia mbili na hamsini; wewe pia, na Haruni, kila mtu na awe na chetezo chake.
1 Samuel 12.7
18 Basi wakavitwaa kila mtu chetezo chake, wakatia na moto ndani yake, wakatia na uvumba juu ya moto, na kusimama pale mlangoni pa hema ya kukutania, pamoja na Musa na Haruni.
19 Kisha Kora akakutanisha mkutano wote kinyume chao mlangoni pa hema ya kukutania; na utukufu wa Bwana ukatokea mbele ya mkutano wote.
Nombres 14.10 Nombres 16.42 Exode 16.7 Lévitique 9.23 Nombres 12.5
20 Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja.
Exode 32.10 Nombres 16.45 Apocalypse 18.4 Psaumes 73.19 Exode 33.5
22 Nao wakapomoka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?
Nombres 27.16 Zacharie 12.1 Ecclésiaste 12.7 Job 12.10 2 Samuel 24.17
23 Bwana akasema na Musa, na kumwambia,
24 Nena na mkutano, na kuwaambia, Ondokeni ninyi hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani, na Abiramu.
Nombres 16.21
25 Basi Musa akainuka na kuwaendea Dathani na Abiramu; na wazee wa Israeli wakaandamana naye.
Nombres 11.25 Nombres 11.16-11.17 Nombres 11.30
26 Akasema na mkutano, na kuwaambia, Nawasihi, ondokeni penye hema za hawa watu waovu, wala msiguse kitu chao cho chote, msiangamizwe katika dhambi zao zote.
Esaïe 52.11 2 Corinthiens 6.17 Apocalypse 18.4 Matthieu 10.14 Deutéronome 13.17
27 Basi wakaondoka hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani na Abiramu, pande zote; nao kina Dathani na Abiramu wakatoka nje wakasimama mlangoni mwa hema zao, pamoja na wake zao, na wana wao na watoto wao wadogo.
Job 9.4 Proverbes 18.12 Job 40.10-40.11 2 Rois 9.30-9.31 Proverbes 16.18
28 Musa akasema, Kwa jambo hili mtajua ya kwamba Bwana amenituma, ili nifanye kazi hizi zote; kwa kuwa mimi sikuzifanya kwa akili zangu mwenyewe.
Exode 3.12 Jean 5.36 Jérémie 23.16 Jean 6.38 Ezéchiel 13.17
29 Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi Bwana hakunituma mimi.
1 Rois 22.28 Esaïe 10.3 2 Chroniques 18.27 Jérémie 5.9 Job 35.15
30 Lakini Bwana akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao washukia shimoni wali hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau Bwana
Psaumes 55.15 Nombres 16.33 Job 31.3 Esaïe 28.21 Esaïe 43.19
31 Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka;
Deutéronome 11.6 Nombres 27.3 Nombres 26.10-26.11 Psaumes 106.17-106.18
32 nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote.
Nombres 26.11 1 Chroniques 6.22 Psaumes 85.1 Deutéronome 11.6 Psaumes 84.1
33 Basi wao, na wote waliokuwa nao, wakashukia shimoni wali hai; nayo nchi ikawafunika wakaangamia kutoka mle mkutanoni.
Jude 1.11 Esaïe 14.9 Psaumes 55.23 Psaumes 143.7 Ezéchiel 32.18
34 Nao Israeli wote waliokuwa kando-kando yao wakakimbia kwa ajili ya kilio chao; kwa kuwa walisema, Nchi isije kutumeza na sisi.
Apocalypse 6.15-6.17 Esaïe 33.3 Zacharie 14.5 Nombres 17.12-17.13
35 Kisha moto ukatoka kwa Bwana, ukawateketeza hao watu mia mbili hamsini waliofukiza uvumba.
Lévitique 10.2 Nombres 26.10 Nombres 16.17 Psaumes 106.18 Nombres 16.2
36 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
37 Mwambie Eleazari mwana wa Haruni kuhani, avitoe vile vyetezo hapo penye moto ukaumwage huo moto kule; kwani ni vitakatifu;
Nombres 16.7 Nombres 16.18 Lévitique 27.28
38 vile vyetezo vya hao waliofanya dhambi na kuzihasiri nafsi zao wenyewe, na vifanywe mbao za kufuliwa kuwa kifuniko cha madhabahu; kwa kuwa walivisongeza mbele za Bwana, navyo ni vitakatifu; vitakuwa ishara kwa wana wa Israeli.
Nombres 26.10 2 Pierre 2.6 Ezéchiel 14.8 Proverbes 20.2 Habakuk 2.10
39 Basi Eleazari kuhani akavitwaa vile vyetezo vya shaba, vilivyosongezwa na hao walioteketezwa; nao wakavifua viwe kifuniko cha madhabahu;
40 viwe ukumbusho kwa wana wa Israeli, ili mgeni awaye yote asiye wa kizazi cha Haruni, asikaribie kufukiza uvumba mbele za Bwana; asiwe mfano wa Kora, na mkutano wake; kama Bwana alivyonena naye, kwa mkono wa Musa.
Nombres 3.10 2 Chroniques 26.16-26.21 1 Rois 13.1-13.3 Nombres 3.38 Nombres 18.4-18.7
41 Lakini siku ya pili yake mkutano wote wa wana wa Israeli wakamnung’unikia Musa, na Haruni, wakasema, Ninyi mmewaua watu wa Bwana.
Nombres 14.2 Psaumes 106.25-106.48 Psaumes 106.13 Matthieu 5.11 Jérémie 43.3
42 Basi ilikuwa, hapo huo mkutano ulipokuwa umekutanika kinyume cha Musa, na kinyume cha Haruni, wakaangalia upande wa hema ya kukutania; na tazama, hilo wingu likaifunika hema, na utukufu wa Bwana ukaonekana.
Nombres 16.19 Lévitique 9.23 Nombres 20.6 Nombres 14.10 Exode 40.34-40.35
43 Na Musa na Haruni wakaenda hapo mbele ya hema ya kukutania.
44 Naye Bwana akanena na Musa, na kumwambia,
45 Ondokeni kati ya mkutano, ili niwaangamize mara moja. Wao wakapomoka kifudifudi.
Nombres 16.21-16.22 Nombres 16.24 1 Chroniques 21.16 Nombres 16.26 Matthieu 26.39
46 Musa akamwambia Haruni, Haya, shika chetezo chako, ukatie moto ndani yake, moto wa madhabahuni, kisha utie na uvumba juu ya moto, ukakichukue haraka, wende nacho katika huo mkutano, ukawafanyie upatanisho; kwa kuwa ghadhabu zimetoka kwa Bwana; hiyo tauni imeanza.
Lévitique 10.6 Nombres 8.19 Nombres 18.5 Nombres 11.33 Psaumes 106.29
47 Basi Haruni akakishika chetezo kama Musa alivyonena, akapiga mbio akaenda katikati ya mkutano; na tazama, tauni ilikuwa imeanza kati ya watu; akatia uvumba juu ya moto na kufanya upatanisho kwa ajili ya hao watu.
Nombres 16.46 Romains 12.21 Esaïe 53.10-53.12 Matthieu 5.44 Psaumes 106.29
48 Akasimama kati ya hao waliokufa na hao waliokuwa wakali hai; tauni ikazuiwa.
2 Samuel 24.25 Hébreux 7.24-7.25 1 Thessaloniciens 1.10 2 Samuel 24.16-24.17 Jacques 5.16
49 Basi waliokufa kwa tauni walikuwa kumi na nne elfu na mia saba, zaidi ya hao waliokufa katika jambo la Kora.
Nombres 25.9 Hébreux 10.28-10.29 Hébreux 2.1-2.3 Nombres 16.32-16.35 Hébreux 12.25
50 Haruni akamrudia Musa pale mlangoni pa hema ya kukutania; hiyo tauni ikazuiwa.
Nombres 16.43 1 Chroniques 21.26-21.30

Cette Bible est dans le domaine public.