Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Nombres 13.7
Bible en Swahili de l’est


Des espions en Canaan

1 Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,
2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.
Deutéronome 1.22-1.25 Nombres 32.8 Deutéronome 1.15 Nombres 11.16 Exode 18.25
3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na Bwana; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli.
Nombres 12.16 Deutéronome 1.19 Deutéronome 9.23 Nombres 32.8 Deutéronome 1.23
4 Na majina yao ni haya; katika kabila ya Reubeni, Shamua mwana Zakuri.
5 Katika kabila ya Simeoni, Shafati mwana wa Hori.
6 Katika kabila ya Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
Nombres 14.6 Nombres 14.30 Nombres 13.30 Nombres 34.19 1 Chroniques 4.15
7 Katika kabila ya Isakari, Igali mwana wa Yusufu.
8 Katika kabila ya Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni
Exode 24.13 Nombres 11.28 Exode 17.9-17.13 Josué 1.16 Deutéronome 32.44
9 Katika kabila ya Benyamini, Palti mwana wa Rafu.
10 Katika kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi.
11 Katika kabila ya Yusufu, yaani, katika kabila ya Manase, Gadi mwana wa Susi.
12 Katika kabila ya Dani, Amieli mwana wa Gemali.
13 Katika kabila ya Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli.
14 Katika kabila ya Naftali, Nabi mwana wa Wofsi.
15 Katika kabila ya Gadi, Geueli mwana wa Maki.
16 Hayo ndiyo majina ya hao watu waliotumwa na Musa waende kuipeleleza nchi. Na huyo Hoshea mwana wa Nuni, Musa akamwita jina lake Yoshua.
Nombres 13.8 Osée 1.1 Actes 7.45 Matthieu 1.21-1.23 Deutéronome 32.44
17 Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani,
Juges 1.9 Genèse 12.9 Juges 1.19 Genèse 13.1 Juges 1.15
18 mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;
Ezéchiel 34.14 Exode 3.8
19 na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;
20 nayo nchi ni ya namna gani, kwamba ni nchi ya unono au ya njaa, kwamba ina msitu au sivyo. Iweni na moyo mkuu, mkayalete matunda ya nchi. Basi wakati ule ulikuwa wakati wa kuiva zabibu za kwanza.
Deutéronome 31.23 Néhémie 9.25 Néhémie 9.35 Ezéchiel 34.14 Nombres 13.23-13.24
21 Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sini hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi.
Nombres 33.36 Nombres 20.1 Nombres 27.14 Josué 15.1 Nombres 34.3-34.4
22 Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri.
Psaumes 78.12 Psaumes 78.43 Esaïe 19.11 Josué 15.13-15.14 Esaïe 30.4
23 Wakafika bonde la Eshkoli, na huko wakakata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, wakalichukua kwa mti kati ya watu wawili; wakaleta makomamanga pia, na tini.
Nombres 32.9 Deutéronome 1.24-1.25 Nombres 13.24 Juges 16.4
24 Bonde lile liliitwa bonde la Eshkoli kwa sababu ya hicho kishada walichokata huko wana wa Israeli.
25 Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini.
Exode 34.28 Exode 24.18 Nombres 14.33-14.34
26 Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.
Nombres 32.8 Nombres 20.1 Nombres 33.36 Josué 14.6 Deutéronome 1.19
27 Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake.
Exode 3.8 Deutéronome 26.11-26.15 Exode 13.5 Josué 5.6 Exode 3.17
28 Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko.
Deutéronome 1.28 Deutéronome 9.1-9.2 Nombres 13.33 Deutéronome 2.10-2.11 Deutéronome 2.21
29 Amaleki anakaa katika nchi ya Negebu; na Mhiti, na Myebusi, na Mwamori wanakaa katika milima, na Mkanaani anakaa karibu na bahari; na kando ya ukingo wa Yordani.
Nombres 14.43 Nombres 14.45 Genèse 15.19-15.21 1 Samuel 30.1 Nombres 14.25
30 Kalebu akawatuliza watu mbele ya Musa, akasema, Na tupande mara, tukaitamalaki; maana twaweza kushinda bila shaka.
Nombres 14.24 Hébreux 11.33 Philippiens 4.13 Josué 14.6-14.8 Romains 8.31
31 Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.
Deutéronome 1.28 Josué 14.8 Nombres 32.9 Deutéronome 9.1 Hébreux 3.19
32 Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.
Amos 2.9 Nombres 14.36-14.37 Matthieu 23.13 Ezéchiel 36.13-36.14 1 Chroniques 20.6
33 Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.
Genèse 6.4 Deutéronome 1.28 Deutéronome 3.11 Deutéronome 9.2 Esaïe 40.22

Cette Bible est dans le domaine public.